Bodi ya Mikopo imefuata siasa katika kutoa mikopo na kusababisha matabaka

NewPage

JF-Expert Member
Mar 22, 2021
1,281
2,020
Kuna kiini macho kikubwa sana ambacho waTanzania hatujakigundua katika utoaji wa mikopo kutoka Bodi ya Mikopo.

Anayepewa mkopo huo ni Mwanafunzi lakini tathmini ya uhitaji wa kumpatia mkopo Mwanafunzi huyo anafanyiwa mzazi wake. Hii ni sawa na kusema kuwa Mzazi ndiye alipaswa kuomba huo mkopo kwa niaba ya mwanaye na sio Mwanafunzi mwenyewe.

Wazazi wengine ambao wanaonekana wana uwezo wamekuwa ni chanzo cha wanao kukosa mikopo hiyo. Sidhani kama mzazi mwenye uwezo angeruhusu mwanae kukopeshwa na hivyo mwanae anapoomba mkopo na kisha tathmini ya uwezo wa huyo mzazi inapotumika kumnyima huyo mtoto mkopo inakuwa ni uonevu na ubaguzi wa hali ya juu sana.

Wazazi ambao ni wafanyakazi wa Serikalini wengi watoto wao wamekuwa wakikosa mikopo sababu tu ya wao kuwa Serikalini. Hii imesababisha watoto hawa kusoma kwa shida sana - wazazi wamekuwa wakiomba wanao wahurumiwe na karo kulipwa kidogo kidogo ili angalau wanao wasome hizo shahada. Machuoni watato ambao wanasemwa ni wanatoka kwenye familia maskini wamekuwa wakipata mikopo kwa urahisi sana na hivyo kusoma kwa raha wakishuhudia wenzao wanaotoka familia zinazosemwa na za wazazi wenye uwezo wakisota.

Mkurugenzi wa mikopo wa Bodi Bi. Nyahende ameshindwa kabisa kutambua kuwa jambo hili linaleta ubaguzi katika jamii. Mtoto wa kakangu mie ambaye anasoma udaktari amenyimwa mkopo kwa sababu baba yake yupo Serikalini anasimulia kila leo kuhusu wenzao wanavyosoma kwa raha na bila stress kwa kuwa mikopo wanapata kiurahisi tu. Watoto hawa hawafanyiwi tathmini ya uhitaji wao wenyewe lakini vinatumika vigezo vya uwezo wa wazazi.

Ninashauri Bodi iangalie utaratibu mpya kuliko huu wa uwezo wa wazazi kwa sababu siku za mbeleni utakuja kuleta matabaka. Ni viongozi wachache tu ambao wanao wanapata mikopo kwa kuzingatia nafasi zao kubwa maofisini. Kaangalie mtoto wa Rais au wa Waziri wa Elimu kama kweli aliwahi kunyimwa mkopo? Bodi yenyewe mna upendeleo na ndiyo mnaoanzisha ubaguzi - ipo siku wanenu au kama sio wanenu hata wajukuuu wenu pia watakuja kubaguliwa! Mtoto wa kakangu amekosa mkopo lakini anamfahamu vema Badru na hata Madam Nyahende - tupo nchi hiii hii na historia hujiandika! Acha wapate watoto wenu wapate mikopo sasa lakini watoto wenu nao watakuja kuwa na watoto! MBOWE SIO GAIDI!
 
Hapo ndipo bodi ya mikopo inapojichanganya, kwani wazazi wa wanafunzi wakiwa wafanyakazi wanalipwa mishahara kiasi gani? Wafanyakazi wa kima cha chini au maafisa wa kawaida wanalipwa kiasi gani?

Badru na huyo Mkurugenzi mikopo wanadhani watumishi wote wanalipwa mishahara mizuri kama wanavyolipwa hapo bodi.watanzania wengi ni dhoofu hali siyo wafanyakazi/ wafanya biashara/wakulima wote ni majanga tu.Hata wale wazazi ambao walikuwa wanapeleka watoto wao shule za binafsi wengi wao walikuwa wanakopa Ofisini ili kuwekeza kwenye (kulipa ada za watoto wao), kwa kutegemea posho kama (extra duty na overtime)

Serikali ya awamu ya tano na sita posho nyingi zimefutwa, idadi ya watumishi wanaokopesheka imepungua Sana,(watumishi wanaishi kwa mishahara yao ) na watumishi wengi Wana mikopo kutoka taasisi za kifedha na riba yake ni kubwa Sana.
Ushauri:

1). Ni vema bodi ikazingatia vigezo ambavyo vipo kwenye kanuni na taratibu zilizotengenezwa baada ya kuunda sheria ya bodi ya mikopo badala ya kutegemea Sana kwenye kanuni na taratibu zilizongezwa baadae.(kanuni za msingi mikopo ilikuwa inatolewa kwa clusters (udaktari, engineers, Sayansi, walimu nk).

2). Bodi isiangalie kuwa wanafunzi hawa walisoma private school, wengine walipata ufadhili au wazazi wao wamefilisika,Wana madeni makubwa nk)

3). Bodi iwakopesha Waombaji wote(asilimia mbalimbali) kwa kuzingatia vigezo vya awali (Clusters) jumlisha na vigezo vya ziada (yatima, familia maskini-Tasaf nk)

4). Haipendezi, kwa wanafunzi wanaochukua programme ya udakatari wakanyimwa kabisa mikopo ambayo watakuja kulipa na ajira kwao ni guarantee serikalini au sekta binafsi pindi wanapohitimu vizuri, kama familia yao ilikuwa na ahuene siku za nyuma, kuna uwezekano leo hii uwezo wao imepungua

5). Basi wapatiwe hata asimilia 50; ya gharama zote na asslimia 50 wazazi wao wajipapase.
 
Hapo ndipo bodi ya mikopo inapojichanganya,kwani wazazi wa. wanafunzi wakiwa wafanyakazi wanalipwa mishahara kiasi gani? Wafanyakazi wa kima Cha chini au maafisa wa kawaida wanalipwa kiasi gani?

Badru na huyo Mkurugenzi mikopo wanadhani watumishi wote wanalipwa mishahara mizuri kama wanavyolipwa hapo bodi.watanzania wengi ni dhoofu hali siyo wafanyakazi/ wafanya biashara/wakulima wote ni majanga tu.Hata wale wazazi ambao walikuwa wanapeleka watoto wao shule za binafsi wengi wao walikuwa wanakopa Ofisini ili kuwekeza kwenye (kulipa ada za watoto wao) ,kwa kutegemea posho kama(extra duty na overtime)

Serikali ya awamu ya tano na sita posho nyingi zimefutwa, idadi ya watumishi wanaokopesheka imepungua Sana,(watumishi wanaishi kwa mishahara yao ) na watumishi wengi Wana mikopo kutoka taasisi za kifedha na riba yake ni kubwa Sana.
Ushauri:

1). Ni vema bodi ikazingatia vigezo ambavyo vipo kwenye kanuni na taratibu zilizotengenezwa baada ya kuunda sheria ya bodi ya mikopo badala ya kutegemea Sana kwenye kanuni na taratibu zilizongezwa baadae.(kanuni za msingi mikopo ilikuwa inatolewa kwa clusters (udaktari, engineers, Sayansi, walimu nk).

2). Bodi isiangalie kuwa wanafunzi hawa walisoma private school,wengine walipata ufadhili au wazazi wao wamefilisika,Wana madeni makubwa nk)

3). Bodi iwakopesha Waombaji wote( asilimia mbalimbali) kwa kuzingatia vigezo vya awali(Clusters) jumlisha na vigezo vya ziada (yatima,familia maskini-Tasaf nk)

4). Haipendezi, kwa wanafunzi wanaochukua programme ya udakatari wakanyimwa kabisa mikopo ambayo watakuja kulipa na ajira kwao ni guarantee serikalini au sekta binafsi pindi wanapohitimu vizuri,Kama familia yao ilikuwa na ahuene siku za nyuma ,Kuna uwezekano Leo hii uwezo wao imepungua

5). Basi wapatiwe hata asimilia 50; ya gharama zote na asslimia 50 wazazi wao wajipapase.
Umefafanua na kutoa mapendekezo mazuri sana lakini Badru na Nyahende wake hilo hawataliona!
 
Hapo ndipo bodi ya mikopo inapojichanganya,kwani wazazi wa. wanafunzi wakiwa wafanyakazi wanalipwa mishahara kiasi gani? Wafanyakazi wa kima Cha chini au maafisa wa kawaida wanalipwa kiasi gani?

Badru na huyo Mkurugenzi mikopo wanadhani watumishi wote wanalipwa mishahara mizuri kama wanavyolipwa hapo bodi.watanzania wengi ni dhoofu hali siyo wafanyakazi/ wafanya biashara/wakulima wote ni majanga tu.Hata wale wazazi ambao walikuwa wanapeleka watoto wao shule za binafsi wengi wao walikuwa wanakopa Ofisini ili kuwekeza kwenye (kulipa ada za watoto wao) ,kwa kutegemea posho kama(extra duty na overtime)

Serikali ya awamu ya tano na sita posho nyingi zimefutwa, idadi ya watumishi wanaokopesheka imepungua Sana,(watumishi wanaishi kwa mishahara yao ) na watumishi wengi Wana mikopo kutoka taasisi za kifedha na riba yake ni kubwa Sana.
Ushauri:

1). Ni vema bodi ikazingatia vigezo ambavyo vipo kwenye kanuni na taratibu zilizotengenezwa baada ya kuunda sheria ya bodi ya mikopo badala ya kutegemea Sana kwenye kanuni na taratibu zilizongezwa baadae.(kanuni za msingi mikopo ilikuwa inatolewa kwa clusters (udaktari, engineers, Sayansi, walimu nk).

2). Bodi isiangalie kuwa wanafunzi hawa walisoma private school,wengine walipata ufadhili au wazazi wao wamefilisika,Wana madeni makubwa nk)

3). Bodi iwakopesha Waombaji wote( asilimia mbalimbali) kwa kuzingatia vigezo vya awali(Clusters) jumlisha na vigezo vya ziada (yatima,familia maskini-Tasaf nk)

4). Haipendezi, kwa wanafunzi wanaochukua programme ya udakatari wakanyimwa kabisa mikopo ambayo watakuja kulipa na ajira kwao ni guarantee serikalini au sekta binafsi pindi wanapohitimu vizuri,Kama familia yao ilikuwa na ahuene siku za nyuma ,Kuna uwezekano Leo hii uwezo wao imepungua

5). Basi wapatiwe hata asimilia 50; ya gharama zote na asslimia 50 wazazi wao wajipapase.
Tatizo siyo bodi ni sera mbovu za CCM
 
Unaweza kukuta Bodi ya Wadhamini ya HESLB na Menejimenti yao kama akina Badru, Nyahende n.k yote ni MaCCM!
Huo ndiyo ukweli! Watoto wa makada wa CCM wanapewa kipaumbele katika kupata mikopo!
 
Mlipieni mtoto shule. Acheni kutegemea dezo na uwezo mnao.
Hujui tu madhira yake nakumbuku mwaka 2012 namaliza advance private, ada yake ilikuwa juu kidogo m 1.5 +, asilimia kubwa tulioapply loan board tulikosa kwa vigezo hivyohivyo anavyotoa mtoa uzi.

Kuna wengine walikuwa sponsored advance lakini waliishia mtaani baada ya kuwekwa kando kwa kudhaniwa wana uwezo wa kujilipia.
 
Hakuna siku nilijisikia huru kama nilipomaliza mkopo wao na kupata cheti cha clearance.

Yaani kama mzazi uko vizuri, ni bora umwepushe mwanao na hii mikopo ya HESLB

Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
 
Hujui tu madhira yake..nakumbuku mwaka 2012 namaliza advance private, ada yake ilikuwa juu kidogo m 1.5 +, asilimia kubwa tulioapply loan board tulikosa kwa vigezo hivyohivyo anavyotoa mtoa uzi.

Kuna wengine walikuwa sponsored advance lakini waliishia mtaani baada ya kuwekwa kando kwa kudhaniwa wana uwezo wa kujilipia.
Ni mbaya sana kufanyia tathmini kipato cha mzazi wakati anayekopeshwa ni mwingine na anayelipa ni sioa anayefanyiwa tathmini. Ujinga mkubwa!
 
Back
Top Bottom