Bodi ya mikopo hii imekaaje? Pamoja na kuanza kulipa tangu 2014 deni langu limeongezeka

Targaryen

JF-Expert Member
Feb 20, 2017
675
640
Niliomba status yangu 2014 kuanza kulipa deni langu na nikapewa ni Tshs.12M mwezi huo huo nikaanza kulipa cha ajabu mwezi huu nimeenda kuomba status yangu "statement ya deni langu" deni limekuwa kwa Tshs. 2M wakati nishaanza kulipa toka mwaka 2014 nimejua kuwa nimemaliza

Nimeamba wanieleweshe wamekokotoa vipi wamebaki kunipiga chenga.
 
Niliomba status yangu 2014 kuanza kulipa deni langu na nikapewa ni Tshs.12M mwezi huo huo nikaanza kulipa cha ajabu mwezi huu nimeenda kuomba status yangu "statement ya deni langu" deni limekuwa kwa Tshs. 2M wakati nishaanza kulipa toka mwaka 2014 nimejua kuwa nimemaliza

Nimeamba wanieleweshe wamekokotoa vipi wamebaki kunipiga chenga ***** zao

Sasa hapo umeibiwa nini, kutoka 12 hadi 2M si umejikomboa!!
 
Oooh yeah, kwamba deni ‘limekuwa kwa 2M’... kama ni hivyo basi ni ajabu hii!!

Kitu ambacho ni ngumu kuamini,aanze kulipa tangu 2014 halafu 2020 awe na deni zaidi?ama kuna wana asilimia nyingi za penalty kwa anayechelewa kulipa deni

Labda inawezekana na mimi sijamuelewa
 
Bodi ya mikopo sio makini katika kufatilia watu walio maliza chuo
Ili waweze kurejesha mikopo yao

Haiwezekani mpaka mtu ajipendekeze kwao ndo waanze kumkata

Hii inchi ina maajabu yke kuna watu wapo kweny system lakini cha ajabu hawakatwi na wao hawana hata habari.

Ila Mkuu jaribu kuwafatilia mpaka kieleweke, wanaweza kukuingiza mjini.
 
Hao HELSB ni takataka kama takataka nyingine tu za jalalani. Mwaka 2016 baada ya hii Serikali kandamizi na ya kidikteta uchwara ya CCM kupitisha ile sheria yao mbovu ya makato ya 15% , niliwatumia email yangu na taarifa zangu ili wanipe mrejesho wa maendeleo ya deni langu na ambalo nilishaanza kukatwa kitambo tu since 2010,

cha ajabu majibu ya deni walilonitumia, yalitofautiana kabisa na deni la kwenye salary slip! Tena kwa zaidi ya tsh. milioni na nusu!! Nikajiuliza hivi kuna Bodi mbili za Mikopo Nchini?

Baada ya kuugundua huo ukilaza wao, niliwapuuzia. Deni la kwenye salary slip lilipokwisha, sikujishughulisha tena kuwatafuta ili wanipe sijui clearance form ya kumaliza hilo deni! maana wangenibambika tu deni la hiyo rentation fees.

Mungu anijalie uzima na afya tele nije niwasomeshe wanangu kwa pesa yangu mwenyewe ili wasije wakaja kuingia kwenye mikono ya hawa wadhulumati.
 
Unafanyaje kuangalia status ya mikopo
Wasiliana na office ya zonal ..
Mfano iringa, dodoma zonal yao ni dodoma..
Address zao waweza zipata kupitia. Website yao..
Pia njia rahisi niliyokuwa natumia kuwasiliana nao ni email, na nacopy mkurugenzi wao,Hadi officer wa chin..
Imenisaidia Sana kupata statements za Uhakika

Nilikuwa na Deni la 9 millions nimeanzA kurejesha Jun 2016 nimemaliza April 2020 na kuna hela nimewazidishia Kama lak 6
hiv
 
Kuna watu mna moyo!! Yaani ukawafuata kabisaa eti uanze kuwalipa

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio kwamba tunawafuata..ila kwa waajiri wengi kwa Sasa ukisign mkataba wa ajira lazima wapeleke jina lako bodi ya mikopo kuhakiki Kama una den au la..

Kuna waraka walipewa na auditors wanazingatia Sana Hilo..kwa hyo whether you like au hapana itabidi ulipe tu Deni
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom