Valencia_UPV
JF-Expert Member
- Mar 31, 2016
- 6,223
- 7,406
Lipeni pesa wandugu, acheni janja janja za hapa na pale. Harusi mbona mnachangia mamilioni?
Presha ya Mzee wa kaya inawanyima usingizi....kuna yule bwana aliekataa uded unadhani alikuwa mjinga!?Ivi miaka yote hiyo Board ya mikopo walikuwa wapi kuwatafuta wadaiwa? tatizo sio wadeni sugu tatizo ni board.Kufanya kazi kwa mazoea
Alaf kuna majina yamerudiwa zaidi ya Mara 3, hii ina maana ya idadi wadaiwa ni ndogo tofauti na iliyotolewa na bodiKuweni serious japo kidogo, badala ya kulipa deni unarukaruka tu, wahimize na wenzio.
Wakuu,Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inatangaza orodha ya majina ya Wadaiwa Sugu ambao wamehitimu katika Vyuo mbalimbali vya Elimu ya Juu kuanzia mwaka wa masomo 1994/1995.
Wasugu hao wanapewa siku 30 kulipa madeni yao ndani ya muda huo kabla hatua za kisheria hazijachukuliwa na wahusika kulazimika kulipia gharama za kuwasaka na kuendesha kesi.
Chanzo: Tovuti ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu..
Kimsingi Bodi ya Mikopo (HESLB) haina takwimu za kutosha wala takwimu sahihi mathalani kwenye taasisi yetu tulitumiwa barua ya kuanza kukatwa mwaka 2013 ila cha ajabu kulikuwa na wenzetu wapatao 3 ambao hawakuwahi kukopa mpaka leo wanatumiwa barua za eti walipe mkopo. Hapo ndio utajua kuwa Bodi ya mikopo vilazaKwani mdaiwa sugu ni yupi? Nami kwenye list hiyo nimo ya wadaiwa sugu. Nilianza kukatwa marejosho na bodi mwaka mmoja baada ya kuhitimu chuo. sasa hivi nakaribia kumaliza mkopo wao afu naanikwa hadharani kama mdaiwa sugu.
Hii kaman sio kudhalilishana ni nini? Ninapanga kuwaburuza hawa jamaa mahakamani kwa kunivunjia heshima na hadhi yangu mbele ya jamii. Kama wapo wengine kama mimi tafadhali ni pm tuchukue hatua stahiki. Nimepitia haya majina kwa umakini sana, nimegundua kuwa wengi wa majina haya ni wale ambao tayari wameanza kulipa na Bodi inawakata.
Kuna watu wangu kadhaa wa karibu ninawafahamu wamemaliza vyuo miaka mingi kadhaa hawajawahi kulipa wala kukatwa japo walikopeshwa mikopo. Na bado kwenye orodha hii hawakuorodheshwa kabisa.
Kama kweli orodha hiii imetoka HESLB, basi nashawishika kuamini kwamba Bodi hii haina takwimu sahihi za nani anadaiwa na nani hadaiwi na nani kamaliza kulipa na nani anaendelea kulipa deni.
Kama ndivo,watapata hasara badala ya faida. NI hatari saana hii!
Hata leo ukiwauliza fulani anadaiwa kiasi gani, Bodi hawawezi kupatia jibu. Hili filamu linaelekea pazuri sana. Waliokula ya mbuzi safari hii lazima waote mapembe!Kimsingi Bodi ya Mikopo (HESLB) haina takwimu za kutosha wala takwimu sahihi mathalani kwenye taasisi yetu tulitumiwa barua ya kuanza kukatwa mwaka 2013 ila cha ajabu kulikuwa na wenzetu wapatao 3 ambao hawakuwahi kukopa mpaka leo wanatumiwa barua za eti walipe mkopo. Hapo ndio utajua kuwa Bodi ya mikopo ******
Eti bana kwanza Hiyo haipo kwenye mkataba..wapige faini yao watulie, hatukusaini kulipia gharama za kesi ..Unasemaje gharama za kesi zitalipwa na mdaiwa wakati kesi haijaamuliwa? Gharama za kesi hulipwa na anayeshindwa.
Download kwenye format ya PDF kisha nenda kwenye kitufe/kialama cha search hapo utaandika jina unalolitaka. Watakuletea yanayofanana utaenda next mpaka ulikute. Kama unatumia kompyuta bonyeza Ctrl+F kisha weka jina unalotaka.Nawezaje kuangalia kwenye ile list ya majina ambayo hayajawekwa alphabetically.
acha ujinga ww watu wamesoma na wanasota mtaan hawana ajira watalipa kwa kutumia nn?Teh teh teh huku ni kuuumbuliwa halafu hawa ndio wale wanaotetea watoto wapewe mkopo huku wao hawajalipa
Aibu sana
Asante mkuu nitafanya hivyo.Download kwenye format ya PDF kisha nenda kwenye kitufe/kialama cha search hapo utaandika jina unalolitaka. Watakuletea yanayofanana utaenda next mpaka ulikute. Kama unatumia kompyuta bonyeza Ctrl+F kisha weka jina unalotaka.
Nadhani ntakua nimekusaidia kiasi.
Karibu. Hapo kwenye Ctrl kisha ndio ubonyeze f. Jiangalie bwana ukaanze kulipa.Mimi ninawalipa ila bado naitwa sugu.Asante mkuu nitafanya hivyo.