fundimchundo
JF-Expert Member
- Jul 23, 2010
- 616
- 904
ITV leo asubuhi imemuonyesha Waziri wa Mifugo, Mhe. Luhaga Mpina akitoa maelekezo ya kuzuia vitendo vya KISHETANI vinavyofanywa na Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania kuchafua maziwa ya ng'ombe yanayouzwa na Wajasiriamali wanawake katika eneo la Ubungo kwa kuyamwagia mafuta ya taa, au rangi ili yasifae kutumika.
Maziwa hayo huwa yanauzwa yakiwa katika ndoo safi za plastic zenye mifuniko.
Najiuliza: Matendo ya Watendaji wa Bodi ya Maziwa ya kutumia pesa za Umma kwa kununua mafuta ya taa na kwenda kuyamwaga juu ya maziwa na hivyo kuwahujumu Wajasiriamali, tena akina mama, hakina ujinai ndani yake?
Maziwa hayo huwa yanauzwa yakiwa katika ndoo safi za plastic zenye mifuniko.
Najiuliza: Matendo ya Watendaji wa Bodi ya Maziwa ya kutumia pesa za Umma kwa kununua mafuta ya taa na kwenda kuyamwaga juu ya maziwa na hivyo kuwahujumu Wajasiriamali, tena akina mama, hakina ujinai ndani yake?