Bodi ya Ligi yatoa tamko kuhusu sakata la mechi ya Simba na Yanga

Kwahiyo kwa mara nyingine, Bodi ya LIgi wanathibitisha kwamba hapakuwa na mashauriano yoyote kati ya vilabu na TFF licha ya kutambua walitaka kupeleka mechi mbele kinyume na kanuni!!

Yaani, TFF walikosa kabisa busara ya kukutana na timu zote mbili ili kujadiliana na kutoa sababu zao ni kwanini mchezo upelekwe mbele kinyume na kanuni inayosema taarifa ay kupeleka mchezo mbele inatakiwa kutolewa angalau saa 24 kabla ya tarehe ya mchezo iliyopangwa mwanzo!!

Bila kujali TFF walipokea maelekezo kutoka kwa nani, ukweli ni kwamba ni wao ndio wanaotakiwa kubebeshwa msalaba!!

Inawezekana Mama SSH (PLEASE, THIS'S JUST MY ASSUMPTION) alitaka kwenda kuosha macho pale Benjamin Mkapa, nae akawasiliana na wizara husika ambayo nayo wakaiagiza TFF moja kwa moja au kupitia BMT!

Na kama sio SSH basi watu kama akina P. Mpango ambao wanajinasibisha na ushabiki wa timu hizi mbili! Inawezekana kuingiliana huku kwa ratib kulitokana na baadhi ya hawa Waheshimiwa kuwa kwenye uzinduzi wa kitabu cha Mzee Mwinyi, na ili yeyote miongoni mwao aweze kushiriki sehemu zote mbili, ikaonekana tukio la kupeleka mbele ni lile ambalo lilikuwa halijaanza... yaani Simba SC vs Yanga SC Match!

Kwavile si TFF wala wizara wangehoji nia hiyo ya SSH, ndipo TFF nao bila kufuata taratibu wakaamua kuagiza timu kuhusu mabadiliko hayo badala ya kujadiliana nao!

Kama hisia zangu kuhusu SSH au mtu mwingine yeyote anayekaribiana na yeye kimamlaka zinakaribia na ukweli, na endapo TFF wangeziita timu zote mbili kuwaeleza sababu ndo hiyo, I AM SURE, kwa kuheshimu Mamlaka ya Rais, pasingekuwa na timu ya kupinga, na kwahiyo kungekuwa na makubaliano ya pamoja ya kupeleka mchezo mbele!!
Mkuu umeongea ukweli , ila siku ya mechi bendi ilikuwa inajipanga kupiga gwaride sijajua kiongoz gani alikuwa anatarajiwa
 
Bado kuna mchawi anafichwa na mimi ndio namtafuta kweli, taarifa imeshindwa kujibu swali la msingi kwa nini mchezo ulisogezwa mbele? ili kama Yanga SC walikosea waadhibiwe, au kama Simba SC walikosea waadhibiwe, na kama kosa ni la TFF au Bodi ya ligi tujue.
Hapa mamlaka husika ndo zenye makosa yanga walifata kanuni na simba wakafata maagizo baadae wakageukia kanuni ...

Sema ata simba wenyewe mapungufu ni mengi
 
Nasoma huku natamani kucheka kwa uchungu. Bodi ya league sisi tumeambiwa tu tumefwata amri ya TFF. TFF sisi tuliambiwa tu lakini tunasikitika sana. Pumbavu wakubwa hawa. Kuna watu wanataka kumsingizia Mama lakini na uhakika sio Mama ingekuwa Mama kawaomba hakuna ambaye angempinga wote wangekubali kwa heshima ila hapa kuna watu wamejificha nyuma ya pazia na Bodi ya league na TFF hawataki kusema ukweli. Bodi wamejitoa wao wamewatupia mzigo TFF. TFF bado wanaomboleza na kusikitika wakimaliza matanga watasema. Dawa ya hawa mbwa wakipanga mechi watu wasiende uwanjani mara hii washabiki wa team zote watizame kwenye TV tu wasiende ndio dawa ya hawa kwa nia nzuri tu na mstakabali wa mpira TZ ili ujinga wa namna hii usirudiwe kwa team zote na sheria zote.
 
Bado kuna mchawi anafichwa na mimi ndio namtafuta kweli, taarifa imeshindwa kujibu swali la msingi kwa nini mchezo ulisogezwa mbele? ili kama Yanga SC walikosea waadhibiwe, au kama Simba SC walikosea waadhibiwe, na kama kosa ni la TFF au Bodi ya ligi tujue.
Pia taarifa ya Bodi inaonesha haikupata maelekezo kutoka serikalini. Huko serikalini nako, hawajui nani aliyetoa taarifa hiyo. Sasa jamii ya soka imshike shati nani kutokan na mauzauza yaliyotokea, yanayoshawishi kuwa watu wabukwa wapenzi wa timu fulani kati ya hizo mbili, wanaashiria kupanga njama hizo kwa masalahi wanayoyafahamu wao!
Heads must roll down this time arounds...the victims ;our soccer caretakers vested to over see the game!
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Mtuhumiwa kaanza kujieleza hadharani. Wanatakiwa wajiudhuru. Eti timu hazikukaguliwa, kama hazikugaliwa nani aliwaambia waamuzi wasikague? Mtatajana tu.
Mkuu, hii kitu imechezwa na TFF sasa baada ya kuona maji yamewafika shingoni wamekumbuka kumbe ni bodi ya ligi ndo jukumu lake hivo TFF wanataka kujikosha kwa kupeleka tatizo kwenye bodi ya ligi. Nawashukuru kwa kuuruka mtego huo. TFF walisema wamepokea maagizo toka wizarani lakini mpaka sasa wizara husika ipo kimya tu. FIFA hiyo inakuja muda si mrefu.
 
Back
Top Bottom