Master Legendary
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 549
- 785
WanaJF hii Bodi ya ajira inaanza majukumu yake lini maana yake TUCTA wametutosa wafanyakazi wamegeuka Chama cha siasa,wafanyakazi tunateswa sana na tofauti ya Mishahara serikalini haiwezekani Graduate katika Serikali hiyohiyo alipwe take home Laki 3 af mfagiaji Bandarini Form Four alipwe Laki saba, Mhandisi EWURA, TANAPA, TRA alipwe Milioni 4 halafu wa kwenye Hamashauri alipwe Laki tano.
Hii haikubaliki jamani uchungu wa kusoma ni uleule tunaomba hii bodi ipunguze hii tofauti ya Mishahara iwe ndogo iwe kama Kenya kwamba keki ya taifa ya Mishahara igawanywe kwa tofauti ndogo katika viwango sawa vya Elimu eg Graduate mwenye 1st Degree popote pale serikali Mshahara wake uanzie Mil 1.3 hadi Mil 1.5 hakuna kulipa chini au zaidi ya hapo na Maposhoposho yote yafutwe.
Hii itapunguza sana matabaka yaliyoko sasa ambapo Graduate huyohuyo mwingine ana uwezo wa kujenga nyumba ya Mil 200 kwa miaka mitatu wakati mwingine hata Kiwanja hana uwezo wa kununua,Matokeo yake wananyanyasana tu mtaani huyu anasalimia ndani ya Prado hata Kioo hashushi mwingine analoa jasho na kumaliza soli za viatu kwa kutembea.
Na hii ndiyo chanzo cha kukithiri kwa Rushwa na kujuana kwenye ajira katika baadhi ya Taasisi.
Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
Hii haikubaliki jamani uchungu wa kusoma ni uleule tunaomba hii bodi ipunguze hii tofauti ya Mishahara iwe ndogo iwe kama Kenya kwamba keki ya taifa ya Mishahara igawanywe kwa tofauti ndogo katika viwango sawa vya Elimu eg Graduate mwenye 1st Degree popote pale serikali Mshahara wake uanzie Mil 1.3 hadi Mil 1.5 hakuna kulipa chini au zaidi ya hapo na Maposhoposho yote yafutwe.
Hii itapunguza sana matabaka yaliyoko sasa ambapo Graduate huyohuyo mwingine ana uwezo wa kujenga nyumba ya Mil 200 kwa miaka mitatu wakati mwingine hata Kiwanja hana uwezo wa kununua,Matokeo yake wananyanyasana tu mtaani huyu anasalimia ndani ya Prado hata Kioo hashushi mwingine analoa jasho na kumaliza soli za viatu kwa kutembea.
Na hii ndiyo chanzo cha kukithiri kwa Rushwa na kujuana kwenye ajira katika baadhi ya Taasisi.
Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums