Bodi Benki Kuu Tanzania yabariki ukaguzi maghorofa pacha Dar

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Date::7/16/2008
Bodi Benki Kuu Tanzania yabariki ukaguzi maghorofa pacha Dar
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

KATIKA hatua ya kuondoa utata kuhusu gharama halisi za ujenzi wa majengo pacha (Twin Tower), Bodi ya Wakurugenzi ya Benki Kuu Tanzania (BoT), imebariki ukaguzi wa kitalaam wa gharama za ujenzi huo.

Uamuzi huo ulifikiwa karibuni, wakati kukiwa na wingu kuhusu gharama halisi za ujenzi wa majengo hayo yenye ghorofa 18, huku ikidaiwa kuwa kuna harufu ya ufisadi.

Taarifa kutoka ndani ya BoT, ambazo zilithibitishwa na Gavana wa benki hiyo, Profesa Benno Ndulu, jana zilisema ukaguzi huo umewahi kufanywa pia katika nchi mbalimbali zenye majengo kama hayo barani Afrika.

Akizungumzia mchakato huo, Profesa Ndulu alisema kuwa uamuzi wa bodi pia unalenga kujiridhisha na gharama hizo na kuona kiasi ambacho kinaweza kuokolewa katika ujenzi huo. Ujenzi huo bado unaendelea.

"Ndiyo, Bodi ilikaa na kuamua ufanyike ukaguzi wa kitalaam kuhusu gharama halisi za ujenzi huo, lengo ni kufanya tathmini halisi na kujiridhisha," alisema Profesa Ndulu.

Alipoulizwa kuhusu matokeo ya uchunguzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), alijibu: "Wao walifanya kwa misingi yao na taarifa wanazo wao, ila na sisi Bodi imeamua kufanya uhakiki."

Profesa Ndulu alifafanua kuwa, hatua iliyopo sasa ni kutangaza zabuni kwa ajili ya kupata kampuni itakayofanya ukaguzi huo.

Alisema kinachofanyika sasa ni misingi ya utawala bora kwa kufuata taratibu za manunuzi katika kupata kampuni hiyo.

"Haiwezakani tu kuteua kampuni bila kufuata taratibu za manunuzi. Sasa hivi tupo katika utekelezaji wa mchakato wa taratibu za manunuzi ambazo ni kutangaza zabuni, tuko katika hatua nzuri," alisema Profesa Ndulu.

Hata hivyo, Gavana huyo alisema kuwa hatua mbalimbali za ujenzi huo zimeonyeshwa katika ripoti za ukaguzi wa hesabu za hadi Juni 2007 na kwamba inasubiriwa ripoti ya Juni 2008.

Alifafanua kwamba, kila hatua itaonyeshwa, lakini gharama za jumla zitajulikana baada ya kupatikana kampuni husika ya kufanya ukaguzi.

Gavana huyo alifafanua kuwa hakuna kitu kitachofichwa kwani lengo ni kumaliza utata wa gharama za ujenzi huo, ambao hata hivyo bado uchunguzi wake uko katika hatua za mwisho.

Profesa Ndulu aliongeza kwamba, hatua nyingine ambayo inatarajiwa kufanyika hivi karibuni ni uzinduzi wa ukumbi wa kisasa wa mikutano.

Ujenzi wa majengo pacha ni moja ya maeneo yanayohusishwa na tuhuma za ufisadi, ambazo zimeikumba na kuitikisa BoT katika kipindi cha kuanzia mwaka 2000.

Gharama hizo ambazo zinaelezwa kufikia Sh 600 bilioni ni kubwa, ikilinganishwa na gharama za ujenzi wa majengo kama hayo katika nchi za Ulaya na Marekani.
 

Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

...Alipoulizwa kuhusu matokeo ya uchunguzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), alijibu: "Wao walifanya kwa misingi yao na taarifa wanazo wao, ila na sisi Bodi imeamua kufanya uhakiki."

TUKUKURU iligundua nini?

Mnamuona huyu incompetent Ndullu.

Mnaona nchi yetu inavyoendeshwa.

Benki inajiamulia kutumia mahela kufanya kitu ambacho kimeshafanywa na taasisi nyingine yenye nguvu na mamlaka ya kufunga mafisadi. Just "kuondoa utata."

Sio uchunguzi wa kutafuta na kushitaki wezi, bali tu kupata picha nzuri ya kimahesabu ya ujenzi. Just 'kuondoa utata." Ndullu huyo.

Na mwandishi tuambie TUKUKURU iling'amua nini. Kama hujui wapigie simu ya dakika nne tu. Au kama ripoti haijatoka, sema hivyo kwa line moja tu.

Halafu Mr. Editor, muulizeni Ndullu kwa nini yeye hataki kujua ripoti ya Taasisi nyingine ya Serikali imesema nini kuhusu kitu hicho hicho anachotaka kuki investigate. Na kama yeye haoni kuwa na duplicate investigations on the same scandal is throwing our money down the toilet dumps. Why is that so hard to ask? Crummy press and incompetent governors. What a recipe!
 
Huyu Ndulu anafanya uchunguzi gani wakati miaka yote yuko katika bodi hiyo hiyo? mwisho si tunajua watakuja na majibu gani? hata yeye kama Balali ni wale wale tu, wezi wa pesa zetu.
 
TUKUKURU iligundua nini?

Mnamuona huyu incompetent Ndullu.

Mnaona nchi yetu inavyoendeshwa.

Benki inajiamulia kutumia mahela kufanya kitu ambacho kimeshafanywa na taasisi nyingine yenye nguvu na mamlaka ya kufunga mafisadi. Just "kuondoa utata."

Sio uchunguzi wa kutafuta na kushitaki wezi, bali tu kupata picha nzuri ya kimahesabu ya ujenzi. Just 'kuondoa utata." Ndullu huyo.

Na mwandishi tuambie TUKUKURU iling'amua nini. Kama hujui wapigie simu ya dakika nne tu. Au kama ripoti haijatoka, sema hivyo kwa line moja tu.

Halafu Mr. Editor, muulizeni Ndullu kwa nini yeye hataki kujua ripoti ya Taasisi nyingine ya Serikali imesema nini kuhusu kitu hicho hicho anachotaka kuki investigate. Na kama yeye haoni kuwa na duplicate investigations on the same scandal is throwing our money down the toilet dumps. Why is that so hard to ask? Crummy press and incompetent governors. What a recipe!

JK hana uwezo wa kuongoza ndiyo maana akamchagua huyu jamaa ambaye alikuwa naibu gavana wakati uozo wote wa EPA unatokea. Sasa hivi anavaa kofia mbili za uongozi ndani BoT kama Gavana na pia kama Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi kitu ambacho hakistahili kabisa hasa ukitilia maanani uozo uliotokea pale BoT wa shilingi 288 kukupuliwa na mafisadi.

Yeye kama mkuu wa bodi ya wakurugenzi anaamua wachunguze maamuzi ya management ambayo yeye alikuwa naibu gavana wa BOT!!!! Ni usanii wa hali ya juu halafu hata haoni umuhimu wa kutoa hadharani ripoti ya uchunguzi uliofanywa na TAKUKURU na TAKUKURU pia hawaoni umuhimu wa kuiweka ripoti hiyo hadharani!!! sasa sijui hao TAKUKURU walichunguza halafu ripoti yao iwekwe ndani ya makabati maana ni SIRIKALI!!!!! JK kalamba galasa lingine kwa Ndullu hana kichwa chochote, kichwa cha ndani ya darasa ni tofauti kabisa na kichwa cha kuongoza taasisi kubwa kama BoT.
 


...Sasa hivi anavaa kofia mbili za uongozi ndani BoT kama Gavana na pia kama Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi kitu ambacho hakistahili kabisa hasa ukitilia maanani uozo uliotokea pale BoT wa shilingi 288 kukupuliwa na mafisadi.


Bubu niliposoma hapo nilifikiri umekunywa Konyagi wakati unaandika. Nikakimbia website ya BOT kuhakikisha kwamba Gavana Ndullu ndie Mkuu wa Bodi ya Wakurugenzi.

Kwanza samahani kwa ku second guess ulichokiandika.

Sasa hapa nilipo nataka kutapika. Yani literally nina kitu kooni hapa, kama kimenikaba hivi.

Siamini.

Siwezi kuendelea kuand...
 
Bubu niliposoma hapo nilifikiri umekunywa Konyagi wakati unaandika. Nikakimbia website ya BOT kuhakikisha kwamba Gavana Ndullu ndie Mkuu wa Bodi ya Wakurugenzi.

Kwanza samahani kwa ku second guess ulichokiandika.

Sasa hapa nilipo nataka kutapika. Yani literally nina kitu kooni hapa, kama kimenikaba hivi.

Siamini.

Siwezi kuendelea kuand...

Enzi za Mtandao hizi ndugu yangu. Hapa JF lazima uandike kitu ambacho una uhakika nacho au kama hukijui kaa pembeni au ukachimbe kupata Dataz kama za FMES vinginevyo utaambuka.
 
Atakula Wapi Jamani Wakati Ashasema Yeye Safi Hizo Ndio Sehemu Za Kuulia Nyoka Pangoni
 
Bubu niliposoma hapo nilifikiri umekunywa Konyagi wakati unaandika. Nikakimbia website ya BOT kuhakikisha kwamba Gavana Ndullu ndie Mkuu wa Bodi ya Wakurugenzi.

Kwanza samahani kwa ku second guess ulichokiandika.

Sasa hapa nilipo nataka kutapika. Yani literally nina kitu kooni hapa, kama kimenikaba hivi.

Siamini.

Siwezi kuendelea kuand...

pole sana
but guys kama hamna facts au hamjajua whats wrong or right dont write/comment. Whats so wrong for him to be the Governor and the Chairman of the Board...... Tafuteni information ya Good Corporate Governance then be free to write....

BTW for the 100th time the current Governor was not in position when the towers or most stuff in question started. Tusibishane... leteni facts
gday
 
pole sana
but guys kama hamna facts au hamjajua whats wrong or right dont write/comment. Whats so wrong for him to be the Governor and the Chairman of the Board...... Tafuteni information ya Good Corporate Governance then be free to write....

BTW for the 100th time the current Governor was not in position when the towers or most stuff in question started. Tusibishane... leteni facts
gday

Mtz, Hivi huoni huu ni upuuzi mwingine kwamba waunde tena tume ya kuchunguza kitu ambacho TAKUKURU wameisha chunguza kwa nia tu ya kujiridhisha???

So what? na kwanini waanzishe uchunguzi wingine bila kujua taarifa ama majibu ya uchunguzi wa awali? yaani uchunguzi wa awali una mapungufu gani hadi waanishe mwingine? je garama zote za chunguzi zinatoka wapi? ufisadi mtupu aisee!
 
Mtz, Hivi huoni huu ni upuuzi mwingine kwamba waunde tena tume ya kuchunguza kitu ambacho TAKUKURU wameisha chunguza kwa nia tu ya kujiridhisha???

So what? na kwanini waanzishe uchunguzi wingine bila kujua taarifa ama majibu ya uchunguzi wa awali? yaani uchunguzi wa awali una mapungufu gani hadi waanishe mwingine? je garama zote za chunguzi zinatoka wapi? ufisadi mtupu aisee!

sidhani kama swali lilikuwa langu as my comment didnt verify what u r asking
my point was to clarify different issue than that. Maybe you need to redirect it elsewhere
sorry nakurudisha nyuma ila i was bit busy sikuweza kujibu on time
gday u all
 
Back
Top Bottom