Uchaguzi 2020 Bodaboda, Machinga na Mama N'tilie, Mungu awape nini tena juu ya Rais Magufuli?

Sep 8, 2020
67
133
Turudi nyuma kidogo. Wafanyabiashara wadogowadogo mnakumbuka mateso mliyoyapata tena kwenye ardhi yenu ya nyumbani Tanzania? Bodaboda, machinga na mama n'tilie. Mkabughudhiwa kufanya shughuli zenu kwenye maeneo flanflan ya nchi kama vile nyie sio binadamu na kwamba hamtakiwi. Yani kwenye ardhi ya Tanzania pakawa pana sehemu pakwenda kufanya biashara na pengine marufuku. Mkafukuzwa, kupokonywa bidhaa zenu na kutozwa misululu ya kodi na tozo kila siku bila huruma katu. Yani mkanyanyaswa vilivyo.

Kuingia kwa Rais John Pombe Magufuli mwaka 2015 akasema imetosha na hapana tena kunyanyasa wala kuonea wafanyabiashara wadogowadogo wala kuzuiliwa kufanya biashara maeneo flanflan, kutozwa hela na misululu ya kodi na kuonya uonevu wowote kwa wafanyabiashara wadogo na kwamba atakayejaribu atakiona.

Serikali ya Awamu ya 5 chini ya uratibu wake mwenyewe Rais John Pombe Magufuli akaanzisha utaratibu wa mmachinga kulipa elfu 20 tu kwa mwaka mzima kufanya biashara zake bila kusumbuliwa na kubughuziwa na mtu yeyote yule badala ya ile hali ya mmachinga na mama ntilie kumswekea msululu wa kodi na tozo anazotakiwa kulipa kila siku.

Kutoka utaratibu wa kulipa karibu kila siku ambao ukipiga mahesabu kwa mwaka mzima mmachinga au mama ntilie alifika kulipa mpaka zaidi ya Million, ikawa sasa unajipatia kitambulisho chako tu cha mjasiriamali kwa elfu 20 tu unafanya biashara zako kwa mwaka mzima bila fyoko na bughudha ya yeyote yule.

Hapo hujaenda kwenye mpango wa Serikali ya Rais Magufuli kutenga maeneo rasmi yenye ukubwa wa hekta 15,822.64 nchi nzima kwa ajili wajasiriamali wakiwemo mama lishe na wauza mbogamboga kufanya biashara zao na kuongeza upatikanaji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa wafanyabiashara wadogo ambapo mfuko wa Small Entrepreneur Loan Facility (SELF) ambao umetoa mikopo kwa wafanyabiashara wadogo yenye thamani ya shilingi billioni 26 na kutengeneza ajira 13,000 mpaka sasa.

Halafu aje mtu hapa kuanza kupiga longolongo, kunanga na kudanganya watu kuhusu mzigo na tabu hii ambayo Rais Magufuli ameitua kwa wafanyabiashara wadogo, tutamshangaa! Nani kama Magufuli eti? Kura zote kwa Dkt John Pombe Magufuli Oktoba 28.
 
Mkuu ungetumia neno Mama lishe na si mama n' tilie. Mi nadhani kuendelea kuwa na Aina hii ya wafanyabiashara wamachinga ni umasikini uliotukuka. Nadhani selikali ingewawezesha hawa wafanyabiashara kuwa na Mazingira rafiki tofauti na kukaa juani na mabarabarani.

Vitambulisho vina changamoto nyingi sana
i Havina picha ya mmiliki wa wa kitambulisho.
ii.Havina signatory ya mtoaji na mpokeaji.
iii. Havina namba mtole.
iv. Wauzaji haramu wa vitambulisho mf police nk.

Hakuna uwazi wa fedha iliyolipwa ni kiasi gani imekwenda wapi imefanya nini ama imewasidiaje hao wajaliamali wadogo.

Je ILE FEDHA ELFU 20 ILIYOLIPWA IMEWASAIDIAJE WAFANYABIASHARA WADOGO
wamewapa offisi nzuri za kufanyia biashara.

Wamewajengea Boda boda vijiwe????

Ama wamewatengenezea mazingira wezeshi ama rafiki kibiashara????

TUSIDANGANYWE NA CCM.
 
Ajabu ya hivi viumbe, majority ni MIMASKINI ya kutupwa... wao binafsi na koo zao lakini kila siku kushabikia upumbavu!
 
Turudi nyuma kidogo. Wafanyabiashara wadogowadogo mnakumbuka mateso mliyoyapata tena kwenye ardhi yenu ya nyumbani Tanzania? Bodaboda, machinga na mama n'tilie....

Why hiyo elf 20 serikali isingelipa na Hao watu wakafanya vitu free?

Na je hiyo elf 20 imeenda wapi? Imerekebisha nn ambacho kinawahusu Hao wafanyabiashara ndogo ndogo?

Coz wanalipa 20 na Wanakaa maeneo yale Yale ya miferejini
 
Ndio mlichobakiza pekee kucheza na umaskini na ujinga wa watanzania maana ndio mtaji wenu. Ila yana mwisho haya hawatabakia maskini Maisha yao yote. Huu ujinga huwezi waambia watu wanaojitambua na wasio na njaa so chezeni na umasikini wetu.
 
Ni kweli hatuwezi kumsahau, kwa mara ya kwanza tumelipishwa 20,000 kwa kitambulisho ambacho hata huwezi kusajilia namba ya simu. Benki huwezi kuombea mkopo.

Hiki kitambulisho chetu cha NIDA kingeweza kutumiwa ila ndio hivyo sisi wanyonge ndio mtaji wa wanasiasa.
 
Mleta mada! Usitetee umachinga na umamantilie! Kama mtu alikuwa mama ntilie 2015, haipaswi aendelee kuwa mamantilie 2020. Maendeleo ni kuona mama huyu akipanda juu na kufanya zaidi, ili aliyekuwa chini ya mamantilie ndio awe mamantilie mpya!!

Usitake watu wawe walewale miaka nenda miaka rudi!! Maendeleo ni mtu kuwa bora leo kuliko jana!!
 
Mtoa uzinafikiri anadhani hao aliowataja ni watu wenye akili ndogo na hivyo hawajui tatizo la kiuchumi lilikoanzia
 
Mkuu ungetumia neno Mama lishe na si mama n' tilie. Mi nadhani kuendelea kuwa na Aina hii ya wafanyabiashara wamachinga ni umasikini uliotukuka. Nadhani selikali ingewawezesha hawa wafanyabiashara kuwa na Mazingira rafiki tofauti na kukaa juani na mabarabarani.

Vitambulisho vina changamoto nyingi sana
i Havina picha ya mmiliki wa wa kitambulisho.
ii.Havina signatory ya mtoaji na mpokeaji.
iii. Havina namba mtole.
iv. Wauzaji haramu wa vitambulisho mf police nk.

Hakuna uwazi wa fedha iliyolipwa ni kiasi gani imekwenda wapi imefanya nini ama imewasidiaje hao wajaliamali wadogo.

Je ILE FEDHA ELFU 20 ILIYOLIPWA IMEWASAIDIAJE WAFANYABIASHARA WADOGO
wamewapa offisi nzuri za kufanyia biashara.

Wamewajengea Boda boda vijiwe????

Ama wamewatengenezea mazingira wezeshi ama rafiki kibiashara????

TUSIDANGANYWE NA CCM.
Mwaka huu watu wamestuka mapema sana! kazi ipo
 
Back
Top Bottom