Bobi Wine's message to Museveni about giving money to Ghetto Yuti

Sifahamu sana ukweli kuhusu siasa za UG na ukweli au uhalisia kuhusu tabia ya mseveni. Ila Aliyekuambia wauaji wakitoa cheki wanaghairi kuua ni nani? Kama unaamini atauwawa basi mshauri afe huku anapigana si ahongwe halafu ndo afe. Tena kufa huku hakuna public attention ts much more easy than vice versa.
Akishavuta cheki yake nani amuue anatulia tuli ananunua hisa kwenye kampuni ya Total.
Anaishi maisha mustarehe.anafungua Ngo yake ya kusaidia vijana maskini.
 
Nimewai siti ila amesharudi kupambania uhuru
Maneno ya kijinga sana haya. Maana yake wewe ni mtazamaji badala ya kuwa mshiriki au muhamasishaji. Amesema 'tatizo si watu waovu bali watu wema wanaokaa kimya maovu yakifanyika'.
 
Ndo tatizo letu waafrika wa kizazi hiki kufikiria "kuvuta cheki" kwa maslahi ya matumbo yetu, kama wazee wetu wangevuta cheki tungekuwa bado tuko kwenye mikono ya mabeberu, kina Mandela hawakushindwa kufanya vile ili washibe wao ila lengo lao lilikuwa kwa maslahi ya taifa/jamii, tofauti na kinachotokea hata hapa nchini, mtu hajali wananchi waliojipanga juani kwenda kumpigia kura ili awe mwakilishi wao kwa kumwamini kabisa, from nowhere mtu anakwambia nimeona niunge juhudi "za mtu mmoja" badala ya maelfu waliomchagua, kizazi hiki kimelaaniwa kwa kuendekeza njaa, naona na wewe unaunga mkono kwamba Bobi Wine apewe cheki na aunge mkono juhudi za Mseveni kuwakandamiza waganda, Afrika Mashariki tumeingia kwa haraka katika utumwa wa nafsi, "mental enslavement. Ngoja tutengeneze historia kwamba kuliwahi kuwa na kipindi cha kuunga mkono, tumuombe Bobi asiwe "Waitara, Mtatiro, Mtulia au Karanga" wa waganda, sijataja madiwani
Vijana wa sasa ni janga la kitaifa. Cheki, mkwanja, kutoka, ....... ndiyo mwisho wa fikra zenu. Vyuo vikuu sasa vingi lakini elimu kidogo.
 
Vijana wa sasa ni janga la kitaifa. Cheki, mkwanja, kutoka, ....... ndiyo mwisho wa fikra zenu. Vyuo vikuu sasa vingi lakini elimu kidogo.
Nina uhakika hujanielewa kabisa, halafu mi sio kijana, naelekea utu uzima sana, nisome tena kwa utuo
 
Back
Top Bottom