Hivi huyo Mohamed anazikwa lini? Maana wenye maji kama hayo huzikwa siku hiyo hiyo au kesho yake. na watoto wake majina ni akina nani?Umesahau jina la kwanza, Mohamed
Hivi huyo Mohamed anazikwa lini? Maana wenye maji kama hayo huzikwa siku hiyo hiyo au kesho yake. na watoto wake majina ni akina nani?Umesahau jina la kwanza, Mohamed
Hivi mbona mnataka kuleta uhuni kwenye majina ya watu sijui kwa nini hamtaki kuliweka jina lake la Mohamed..
Nyie wote ni wasukuma mikokoteni tu na siyo wa-Sukuma kama kabila. Kisukuma kina wingi wa kila neno ukitaka. Kisukuma kina lahaja za kikanda pia, Mwanza kuna lahaja zaidi ya 6, Shinyanga zaidi ya 4 na Tabora zaidi ya 4 pia. Sasa unabisha nini hapo Salum?
Nilichojifunza hapa ni kuwa Mwanzilishi wa CHADEMA hakuwa mkristo, wala hakuwa mchaga. Hivyo kwa mtazamo wangu ni dhahiri kuwa hiki chama sio cha wachaga wala hakifungamani na wakristo kama Magamba walivyopotosha ukweli. Nadhani hiki chama kimempoteza mwana uhamsho mwanzilishi aliyekuwa na uchungu na maisha ya wananchi..RIP Baba wa taifa wa Chadema- MAKANI
uamsho
Na vipi yule binti yake Dr Julie Makani??
Hili ni suala tatanishi na nifundisho kwa uamusho kwamba uislam na ukristo wa watanzania umejichanganya sana katika jamii ni tofauti na jamii zingine kama za kisomali, kioman nk ambazo huwezi kuta dini zote mbili ndani ya familia moja
tumia akili yako vizuri mkuu. kwani Makani ni mwarabu? we vipi?
hayo majina ya uamsho hukohuko Bububu na Mwanakwerekwe.
Unawezaje kutafsiri majina ya mtu ukawacha jina lake la mwanzo? kwi kwi kwi teh teh teh!
Bob Nyanga Makani,Mwenyekiti wa pili na Katibu Mkuu wa kwanza wa CHADEMA,amefariki dunia jana.Ninaomoyo mnyenyekevu kuwapa pole wote wanaohusika kwa namna moja au nyingine na msiba huu mkubwa.Mungu awape ustahamilivu na ujasiri mkubwa.Bwana alitoa,Bwana ametwaa...jina lake LIHIMIDIWE! Amina.
Hayati Bob Nyanga Makani alikuwa wa kipekee.Pamoja na kuwa Mwanasheria(baadaye Wakili wa Mahakama Kuu tangu tarehe 4/4/1986 na kupewa Nambari 131 ya Uwakili),alikuwa ni Naibu Gavana wa Kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania.Baadaye,kutokana na kutoridhishwa na utendaye Serikalini,Bob Nyanga Makani akishirikiana na wanamageuzi wengine chini ya Edwin Isaac Mtei,walianzisha CHADEMA mwaka 1992 naye kuwa Katibu Mkuu wa kwanza.
Neno 'Bob' humaanisha,pamoja na vitu vingine,kutikisa(hasa kichwa) kuanzia chini kwenda juu.Huonyesha usikivu wa kufuatilia na kukubaliana na jambo la msingi linaloelezwa.
'Nyanga' katika lugha ya Nyanja ya pale Zambia(ambayo hufanana na lugha nyingine za kibantu hapa kwetu) humaanisha pembe ya ndovu.Hii inaonyesha kuvuma na kuwa maarufu sana.Yeye pia alikuwa hivyo.
'Makani' kwa Kinyanja hichohicho,humaanisha upinzani wa kimaneno au kimatendo.Hapa sina haja ya kutoa maelezo marefu.Kila mtanzania anajua.Alikuwa mpinzani wa kweli.
Huyo ndiye Bob Nyanga Makani.Pumzika kwa amani Wakili Msomi na Mpambanaji 'Msikivu Mvumaji Mpinzani wa kweli'...
Unaonaje wewe ukitafsiri hilo jina MOHAMED maana yake nini? Tusijiingize katika mgogoro wa kidini bila sababu ya maana?
Bahati mbaya Bazazi haamini jina linabeba IMANI yake (dini). Kwangu kuna majina ya Kiarabu (yananasibishwa na Uislamu) na majina ya Kizungu (yananasibishwa na Ukristo). Huu ni umbilikimo wa fikra ambao ni mbaya sana.
Plz Be a greater thinker! THINK LOUD & OUT OF THE BOX.
Bazazi ni Bazazi!
Siyo "Deed Poll" ni "Deep Poll"Jina la Mohammed lilikoma siku alipoapa na kubadili jina kisheria kwa 'Deed Poll' .Hata kwenye Roll of Advocates, ambapo nawe upo,anaitwa Bob Nyanga Makani.Tazama nambari 131.Hilo ndilo jina lake.
Niko sahihi Mkuu...Siyo "Deed Poll" ni "Deep Poll"
Huyu dada nilisikia story yake nisingependa niiweke humu, aliolewa na mtoto wa Iddi Simba kuna kitu kuhusu Dini yake alikifanya baadae kilimletea shida , ulizia vizuri ndugu yangu.
Ndugu yangu JF sio sehemu ya porojo kitu kama hujui kitu kaa kimya! Hivi mtoto wa marehemu Bob Makani, Mohamed Makani akisikia hii kauli sidhani kama atajisikia vizuri kweli.
Mbona unaniuliza Jakaya tu hata Mrisho na Kikwete yote sijui. Naomba kujua mie!.