VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Bob Nyanga Makani,Mwenyekiti wa pili na Katibu Mkuu wa kwanza wa CHADEMA,amefariki dunia jana.Ninaomoyo mnyenyekevu kuwapa pole wote wanaohusika kwa namna moja au nyingine na msiba huu mkubwa.Mungu awape ustahamilivu na ujasiri mkubwa.Bwana alitoa,Bwana ametwaa...jina lake LIHIMIDIWE! Amina.
Hayati Bob Nyanga Makani alikuwa wa kipekee.Pamoja na kuwa Mwanasheria(baadaye Wakili wa Mahakama Kuu tangu tarehe 4/4/1986 na kupewa Nambari 131 ya Uwakili),alikuwa ni Naibu Gavana wa Kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania.Baadaye,kutokana na kutoridhishwa na utendaye Serikalini,Bob Nyanga Makani akishirikiana na wanamageuzi wengine chini ya Edwin Isaac Mtei,walianzisha CHADEMA mwaka 1992 naye kuwa Katibu Mkuu wa kwanza.
Neno 'Bob' humaanisha,pamoja na vitu vingine,kutikisa(hasa kichwa) kuanzia chini kwenda juu.Huonyesha usikivu wa kufuatilia na kukubaliana na jambo la msingi linaloelezwa.
'Nyanga' katika lugha ya Nyanja ya pale Zambia(ambayo hufanana na lugha nyingine za kibantu hapa kwetu) humaanisha pembe ya ndovu.Hii inaonyesha kuvuma na kuwa maarufu sana.Yeye pia alikuwa hivyo.
'Makani' kwa Kinyanja hichohicho,humaanisha upinzani wa kimaneno au kimatendo.Hapa sina haja ya kutoa maelezo marefu.Kila mtanzania anajua.Alikuwa mpinzani wa kweli.
Huyo ndiye Bob Nyanga Makani.Pumzika kwa amani Wakili Msomi na Mpambanaji 'Msikivu Mvumaji Mpinzani wa kweli'...
Hayati Bob Nyanga Makani alikuwa wa kipekee.Pamoja na kuwa Mwanasheria(baadaye Wakili wa Mahakama Kuu tangu tarehe 4/4/1986 na kupewa Nambari 131 ya Uwakili),alikuwa ni Naibu Gavana wa Kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania.Baadaye,kutokana na kutoridhishwa na utendaye Serikalini,Bob Nyanga Makani akishirikiana na wanamageuzi wengine chini ya Edwin Isaac Mtei,walianzisha CHADEMA mwaka 1992 naye kuwa Katibu Mkuu wa kwanza.
Neno 'Bob' humaanisha,pamoja na vitu vingine,kutikisa(hasa kichwa) kuanzia chini kwenda juu.Huonyesha usikivu wa kufuatilia na kukubaliana na jambo la msingi linaloelezwa.
'Nyanga' katika lugha ya Nyanja ya pale Zambia(ambayo hufanana na lugha nyingine za kibantu hapa kwetu) humaanisha pembe ya ndovu.Hii inaonyesha kuvuma na kuwa maarufu sana.Yeye pia alikuwa hivyo.
'Makani' kwa Kinyanja hichohicho,humaanisha upinzani wa kimaneno au kimatendo.Hapa sina haja ya kutoa maelezo marefu.Kila mtanzania anajua.Alikuwa mpinzani wa kweli.
Huyo ndiye Bob Nyanga Makani.Pumzika kwa amani Wakili Msomi na Mpambanaji 'Msikivu Mvumaji Mpinzani wa kweli'...