BMT yasema, makanjanja wameua michezo Tanzania

Daniel Mbega

JF-Expert Member
Mar 20, 2013
338
180
BARAZA la Michezo la Taifa (BMT) limesema kwamba, makanjanja (watu wasio na ujuzi wala elimu ya michezo) ndio waliochangia kuporomoka kwa michezo hiyo nchini, FikraPevu inaripoti.

Katika mahojiano maalum na FikraPevu, Katibu Mtendaji wa BMT, Mohamed Kiganja, amesema hata mchezo wa soka unaoelezwa kupendelewa kuliko mingine, nao haujazaa matunda yoyote kwa sababu wanaouongoza ni makanjanja ambao ama wamekwenda kwa ajili ya kupiga dili au wanataka kutengeneza majina ili waingie kwenye siasa.

“Ziko changamoto nyingi, lakini hili la makanjanja kujiingiza katika uongozi wa michezo ni tatizo kubwa kwa sababu ndilo linalochangia vyama vya michezo kudorora pamoja na timu kutofanya vizuri kwa kukosa mipango ya maendeleo,” amesema Kiganja ambaye ameteuliwa kushika wadhifa huo miezi mitatu iliyopita.

Soma zaidi hapa => BMT yasema, makanjanja wameua michezo Tanzania | Fikra Pevu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom