I am Groot
JF-Expert Member
- Jul 20, 2018
- 3,726
- 10,020
"Blacklist na whitelist" sio maneno mageni sana katika ulimwengu wa leo. Mara nyingi haya maneno yamezoeleka kutumika katika mambo ya kiusalama katika mitandao ya mawasiliano.
Ukiangalia kwa upande mwingine maneno haya hasa hapo zamani kidogo katika nchi za wenzetu 'ulaya na marekani' maneno haya yalimaanisha tofauti au utofauti kati ya kundi/jamii moja hadi nyingine nikimaanisha;
WHITELIST: Hili lilikuwa ni kundi lililochukuliwa kuwa na haki zote katika jamii. Halikadhalika;
BLACKLIST: Hili lilikuwa ni kundi au jamii fulani iliyotengwa ama isiyokuwa na umuhimu wala haki yoyote. Kundi hili lilitumiwa hasa kwa watu waliokuwa si wasiokuwa na asili ya watu weupe hasa (Waafrika na watumwa)
Sasa je, kuna ulazima wa maneno haya kuendelea kutumika kwa karne hii? Je, kuendelezwa kutumiwa kwa maneno haya si muendelezo wa ubaguzi wa rangi kwa mtindo wa kitofauti?
Nimemaliza
Ukiangalia kwa upande mwingine maneno haya hasa hapo zamani kidogo katika nchi za wenzetu 'ulaya na marekani' maneno haya yalimaanisha tofauti au utofauti kati ya kundi/jamii moja hadi nyingine nikimaanisha;
WHITELIST: Hili lilikuwa ni kundi lililochukuliwa kuwa na haki zote katika jamii. Halikadhalika;
BLACKLIST: Hili lilikuwa ni kundi au jamii fulani iliyotengwa ama isiyokuwa na umuhimu wala haki yoyote. Kundi hili lilitumiwa hasa kwa watu waliokuwa si wasiokuwa na asili ya watu weupe hasa (Waafrika na watumwa)
Sasa je, kuna ulazima wa maneno haya kuendelea kutumika kwa karne hii? Je, kuendelezwa kutumiwa kwa maneno haya si muendelezo wa ubaguzi wa rangi kwa mtindo wa kitofauti?
Nimemaliza