Chibidu
JF-Expert Member
- Dec 19, 2008
- 387
- 49
Wana JF habari za wikienda. kwa wale wataalam wa simu za mkononi naomba msaada wenu. mwenzenu nimekuwa nikitumia simu aina ya nokia E5 kwaajili ya matumizi ya internet hasa ninapokuwa mahali tofauti na nyumbani au ofisini. Sasa hiyo simu nimempa mdogo wangu kama zawadi. Sasa Katika kupitapita mitaa ya kariakoo nikakutana na simu inafanana kama ile niliyokuwa natumia, lakini yenyewe inaitwa blackberry Q3 ya kichina. Inaonesha facilities zote ninazotaka zimo, pamoja na internet. Tangu niinunue sasa nina zaidi ya wiki sijaweza ku connect internet. Ila yahoo mesenger inaunga kama kawaida. Dukani waliniambia kuwa nikiwapigia customer center wa mtandao ninaotumia watanifanyia installation na nitapata net kama kawaida. Nikafanya auto configuration mwenyewe ikanigomea. Nikawaendea watu wa airtel wanisaidie kufanya manual configuration, ndio kwanzaaa wakanikatisha tamaa, wakaniambia bro hizo chinise type huwa hatuna msaada nazo. Kwahiyo wakuu kama kuna mtu ana utaalam nazo naomba taulo (msaada) maana inanikosesha raha niwapo tofauti na nyumbani au ofisini. Maana nishainunua na bajeti yenyewe ya simu kwa siku za karibuni imeshabana. Majibu yangu nitayafuata baadaye hapa JF maana hapa nilipo ngereja kishachukua umeme wake, natumia simu ya mshikaji tu na mwenyewe kishaniambia muda alionipa umeisha