Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,171
- 23,866
Sera mbovu za uchumi sasa matokeo yake tunaanza kuyaona.
Biashara haiwezi kuendeshwa kwa mtutu wa bunduki au kwa kulazimisha kile kitu serikali inataka.
Tulilazimisha kodi zisizolipika, biashara zikafungwa kwa wingi.
Tumelazimisha biashara ya fedha ya kigeni kufanywa na mabenki tu, sasa kuna black market ya fedha hiyo.
Over regulate the economy na una pata a parallel economy.
Kstika parallel economy. Govt control almost hakuna na kodi huko huwezi kusanya.
Maduka yamefungwa na wafanyabiashara wamerudisha leseni, tujiulize sasa biashara zimekufa kabisa?
BIG NO!
Tujiulize machinga anapata wapi mali zake? Parallel economy.
Wachumi waliobobea watakuambia, Principle ya Demand and Supply ndio inatawala kote.
Iwekee vikwazo visivyovumilika, inakula kwako.
Waziri Mpango na Gavana BOT, Nd Luoga wajiuzulu, kazi ya kuendesha uchumi imewashinda.