Binti wa miaka 15 ateseka kwa kuvunjwa mguu na gari ya BOT SU36797

nyembeason

Member
May 4, 2009
44
21
Wadau, msaada tafadhali. Binti wa miaka 15 (mwanafunzi-secondary na shule haendi tena) alikanyagwa tarehe 24/06/2016 na gari ya serikali, BOT, na.SU 36797, katika maeneo ya Mkundi-Morogoro, barabara kuu ya lami ya Moro-Dom. Alipelekwa hospitali ya mkoa wa Morogoro. Matibabu yakafanyika na kuwekewa HOGO-POP. Dereva alishitakiwa na kupigwa faini ya TZS 30,000/ AU kifungo cha mwaka mmoja. Dereva alilipa faini.

Mtoto analelewa na mzazi mmoja-mama na maisha ni duni sana-tena sana. Nimekuwa nikiisaidia familia kwa kiasi nikijaliwa, nauli na matibabu na pia kwa kuipeleka kesi yake Chama cha Wanasheria Tanganyika kwa msaada wa kisheria. Amepewa Wakili na ameandika barua kwa kampuni ya BIMA. Hawataki kulipa. Hali ya mtoto ni MBAYA SANA kwa sasa. Mguu umevimba upya na unaonekana mifupa haikuunga kabisa. Wadau msaada kwa hili tafadhali
 
Sasa hapo kosa ni la bima au gari? Dereva alishawajibishwa na jamhuri (hapa tulilie sheria mbovu za nchi yetu) Tukirudi upande wa sheria bima ndio ina jukumu la kumlipa huyo majeruhi (kwamba atibiwe then wapeleke risiti kwa ajili ya refund)... sijui kama kuna utaratibu wa kulipwa kabla !
Bima ni utapeli tu maana wanatafuta mbinu za kukuminya badala ya kukusaidia
BTW: poleni sana
 
Wadau, msaada tafadhali. Binti wa miaka 15 (mwanafunzi-secondary na shule haendi tena) alikanyagwa tarehe 24/06/2016 na gari ya serikali, BOT, na.SU 36797, katika maeneo ya Mkundi-Morogoro, barabara kuu ya lami ya Moro-Dom. Alipelekwa hospitali ya mkoa wa Morogoro. Matibabu yakafanyika na kuwekewa HOGO-POP. Dereva alishitakiwa na kupigwa faini ya TZS 30,000/ AU kifungo cha mwaka mmoja. Dereva alilipa faini.

Mtoto analelewa na mzazi mmoja-mama na maisha ni duni sana-tena sana. Nimekuwa nikiisaidia familia kwa kiasi nikijaliwa, nauli na matibabu na pia kwa kuipeleka kesi yake Chama cha Wanasheria Tanganyika kwa msaada wa kisheria. Amepewa Wakili na ameandika barua kwa kampuni ya BIMA. Hawataki kulipa. Hali ya mtoto ni MBAYA SANA kwa sasa. Mguu umevimba upya na unaonekana mifupa haikuunga kabisa. Wadau msaada kwa hili tafadhali
Doh very sad kwa kweli hivi hadi miaka hii kuna fain ya elfu 30,000.
 
Sasa hapo kosa ni la bima au gari? Dereva alishawajibishwa na jamhuri (hapa tulilie sheria mbovu za nchi yetu) Tukirudi upande wa sheria bima ndio ina jukumu la kumlipa huyo majeruhi (kwamba atibiwe then wapeleke risiti kwa ajili ya refund)... sijui kama kuna utaratibu wa kulipwa kabla !
Bima ni utapeli tu maana wanatafuta mbinu za kukuminya badala ya kukusaidia
BTW: poleni sana
sijawahi kugundua taasisi nyivi kama shirika la
bima nchi hii
 
Sasa hapo kosa ni la bima au gari? Dereva alishawajibishwa na jamhuri (hapa tulilie sheria mbovu za nchi yetu) Tukirudi upande wa sheria bima ndio ina jukumu la kumlipa huyo majeruhi (kwamba atibiwe then wapeleke risiti kwa ajili ya refund)... sijui kama kuna utaratibu wa kulipwa kabla !
Bima ni utapeli tu maana wanatafuta mbinu za kukuminya badala ya kukusaidia
BTW: poleni sana
BOT shirika la umma....kwanini wasimpe matibabu mtoto wakadai bima....mtoo mguu waoza...!!!..very inhumane
 
Mwenyezi Mungu atamsaidieje? Msipende kumsingizia mwenyezi Mungu kwa uzembe, mtoto anahitaji msaada huyo, tumchangie apate matibabu na sio harusi.
 
Wadau, msaada tafadhali. Binti wa miaka 15 (mwanafunzi-secondary na shule haendi tena) alikanyagwa tarehe 24/06/2016 na gari ya serikali, BOT, na.SU 36797, katika maeneo ya Mkundi-Morogoro, barabara kuu ya lami ya Moro-Dom. Alipelekwa hospitali ya mkoa wa Morogoro. Matibabu yakafanyika na kuwekewa HOGO-POP. Dereva alishitakiwa na kupigwa faini ya TZS 30,000/ AU kifungo cha mwaka mmoja. Dereva alilipa faini.

Mtoto analelewa na mzazi mmoja-mama na maisha ni duni sana-tena sana. Nimekuwa nikiisaidia familia kwa kiasi nikijaliwa, nauli na matibabu na pia kwa kuipeleka kesi yake Chama cha Wanasheria Tanganyika kwa msaada wa kisheria. Amepewa Wakili na ameandika barua kwa kampuni ya BIMA. Hawataki kulipa. Hali ya mtoto ni MBAYA SANA kwa sasa. Mguu umevimba upya na unaonekana mifupa haikuunga kabisa. Wadau msaada kwa hili tafadhali
Kwa nn bima hawataki kulipa?tuanzie hapo kwanza.....
 
Bima gani mnayoongelea maana gari iliyomgonga ni ya serikali,gari nyingi za serikali hazina bima.
 
Hivi magari ya Serikali yameanza lini kulipa Bima? Ninachojua magari ya Donors yaan DFP ndio hukatiwa bima lkn haya STK, SU, MT, PT nk hayakatiwi bima. Au mim wa zaman, ngoja waje vijana wa sasa watupe elimu.
BOT kitengo cha Mahusiano kwa jamii waandaikiwe barua watatoa msaada kwa binti huyo. Nimejikuta namhurumia sana.
 
Mwenyezi Mungu atamsaidieje? Msipende kumsingizia mwenyezi Mungu kwa uzembe, mtoto anahitaji msaada huyo, tumchangie apate matibabu na sio harusi.
kama wewe hautambui uwepo wa Mungu basi usiforce watu wafanane
 
Du poleni sana. Nimewahi kukutana na kesi kama hiyo. Bima hawalipi kabla. Mlalamikaji atalipia gharama ndo anaprocess refund na Bima. Kwa kesi yangu ofisi ililipia gharama zote za mtoto. Maana ajali ilitokea kijijini na familia ya mtoto walikuwa ktkt hali duni. Nadhani waliosababisha ajali wanaweza angalia suala hili kwa umakini na kujaribu msaidia mtoto kwa gharama za matibabu nina uhakika uwezo huo wanao na kujaribu kuwasaidia kufuatilia na insurance kama tulivyofanya sisi. Ishu hapa sio dereva kulipa faini ni kiubinadamu zaidi
 
Magari ya serikali hayana bima. Magari hayo hayalipiwi road license. Magari hayo hayakamatwi na camera wanapozidisha spidi. Magari hayo pia yanakuwa na viyoyozi vya kuwapoza madereva mchana kutwa wakati mabosi wao wako ofisini. Pia magari hayo yanabeba maharusi siku za wikiendi. Na ni magari hayo yanayopaki pale vitu vidogo vinapoharibika na kuozea maofisini na kufanya ofisi nyingi za serikali kuwa kama gereji bubu katikati ya miji
 
wasiliana na viongozi wa serikali then suala lifike hata kwa jpm
 
Wadau, msaada tafadhali. Binti wa miaka 15 (mwanafunzi-secondary na shule haendi tena) alikanyagwa tarehe 24/06/2016 na gari ya serikali, BOT, na.SU 36797, katika maeneo ya Mkundi-Morogoro, barabara kuu ya lami ya Moro-Dom. Alipelekwa hospitali ya mkoa wa Morogoro. Matibabu yakafanyika na kuwekewa HOGO-POP. Dereva alishitakiwa na kupigwa faini ya TZS 30,000/ AU kifungo cha mwaka mmoja. Dereva alilipa faini.

Mtoto analelewa na mzazi mmoja-mama na maisha ni duni sana-tena sana. Nimekuwa nikiisaidia familia kwa kiasi nikijaliwa, nauli na matibabu na pia kwa kuipeleka kesi yake Chama cha Wanasheria Tanganyika kwa msaada wa kisheria. Amepewa Wakili na ameandika barua kwa kampuni ya BIMA. Hawataki kulipa. Hali ya mtoto ni MBAYA SANA kwa sasa. Mguu umevimba upya na unaonekana mifupa haikuunga kabisa. Wadau msaada kwa hili tafadhali
Kwa kuwa ameshapata wakili,naamini atasaidiwa kupata haki yake
 
Poleni sana. Very inhumane kwakweli. Hebu jaribuni hilo suala lipae kwenye media... hasa hasa ITV au Clouds Tv. Maana siku hizi ni mpaka issue iende viral on media ndipo watendaji wachukue hatua.

-Kaveli-
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom