Binti niliemtelekeza na bili bar, kumbe kawaeleza mabinti wote kazini, sasa ni vibuti tu

jean phillipe beyun

Senior Member
May 18, 2015
142
167
Kuna binti ambae tunafanya kazi pamoja na ambae nilimtoa outing siku moja, kinyume na matarajio akaniletea kundi la wasichana wenzie kunifilisi nami nika apply umafia wa hali juu kwa kuwakimbia na kuwatelekeza na bili kubwa waliyotumia wenyewe, mi nilikunywa bia 3 tu

Sasa kumbe tangu siku hiyo ameendesha kampeni kali ya kunichafua hapa kazini kwa mabinti wenzie kiasi kwamba hata nikiomba kampani ya kawaida tu kwenda lunch mabinti hunitazama chini hadi juu na mwisho kunisonya msonyo mkali sana na kuondoka zao huku wakitamka maneno kwa methali na mafunzo, wengine wakiniambia "" unalo babu"" sasa sijajua maana yake hadi sasa

Yote tisa, kumi nikaona nijaribu bahati yangu kwa binti mwingine ambae ni mtaratibu sana, yupo kivyake vyake na anaishi ki british sana hapa kazini, baada ya mazungumzo ya siku kadhaa, nikaona nimtafutie zawadi ndogo kusindikizia ujumbe wangu wa mahaba, weekend hii nikaenda dukani pale sinza duka moja linauza chupi tu za akina dada nikawaeleza nia yangu wakanifungia vizuri kwenye package maalum


Leo asubuhi tulipo sign in tu nikaangalia kushoto na kulia watu hawanitazami nikaenda haraka kwenye meza yake na kumpa kishkaji na kumwambia ni zawadi yake ni zawadi yake
Akaipokea nikarudi kwenye idara yangu maana tupo ghorofa tofauti ya 3 na 4

Nashangaa baada kama ya lisaaa moja nashtuka kumuona yule binti akinifuata huku amefura na kunirushia ile chupi usoni ikiwa imeshafunguliwa kwenye package yake na kuanza kunipaka kwamba namuonaje hadi nampelekea chupi,? Kwamba nisimfananishe yeye na flani (yule niliemkimbia bar)
Kumbe yule binti kaeleza kampuni nzima?

Nimepata aibu ya milele leo

Hivi wakuu nimekosea wapi?
Kumpelekea mwanamke zawadi kuna ubaya?
Mbona tulikua tunaenda vizuri tu tangu juzi? Au ni sumu amepewa na yule binti mwingine?
 
d4i6z.jpg
 
Haa haa haa yani sipati picha uso ulikushukaje. By the way wewe ni mwanaume lazima ukubaliane na hali halisi simama kiume zaidi , tena huyohuyo alokurushia hio lechupiz ndo mtamu ka mcharo sasa. NB dinda naye mpaka kieleweke kiume zaid ikiwezekana mtafute mkae sehem ilotulia mchane kila kitu akae akijua. Ila huyo kunguru mwingine nimemind kinoma sema siko kwenye office zenu ingekuwa ni mwendo wa kumuumbua tuu dadeki zake.
 
hahahahhaaaa...zawadi ya chupi?!..u are the (sorry for this) dumbest person i've read on today..duh!
 
Kwa nini usimpelekee nyumbani kwake badala ya ofisini, aibu nyingine huwa mnajitakia wenyewe, we husomi hata alama za nyakati
 
Kuna binti ambae tunafanya kazi pamoja na ambae nilimtoa outing siku moja, kinyume na matarajio akaniletea kundi la wasichana wenzie kunifilisi nami nika apply umafia wa hali juu kwa kuwakimbia na kuwatelekeza na bili kubwa waliyotumia wenyewe, mi nilikunywa bia 3 tu

Sasa kumbe tangu siku hiyo ameendesha kampeni kali ya kunichafua hapa kazini kwa mabinti wenzie kiasi kwamba hata nikiomba kampani ya kawaida tu kwenda lunch mabinti hunitazama chini hadi juu na mwisho kunisonya msonyo mkali sana na kuondoka zao huku wakitamka maneno kwa methali na mafunzo, wengine wakiniambia "" unalo babu"" sasa sijajua maana yake hadi sasa

Yote tisa, kumi nikaona nijaribu bahati yangu kwa binti mwingine ambae ni mtaratibu sana, yupo kivyake vyake na anaishi ki british sana hapa kazini, baada ya mazungumzo ya siku kadhaa, nikaona nimtafutie zawadi ndogo kusindikizia ujumbe wangu wa mahaba, weekend hii nikaenda dukani pale sinza duka moja linauza chupi tu za akina dada nikawaeleza nia yangu wakanifungia vizuri kwenye package maalum


Leo asubuhi tulipo sign in tu nikaangalia kushoto na kulia watu hawanitazami nikaenda haraka kwenye meza yake na kumpa kishkaji na kumwambia ni zawadi yake ni zawadi yake
Akaipokea nikarudi kwenye idara yangu maana tupo ghorofa tofauti ya 3 na 4

Nashangaa baada kama ya lisaaa moja nashtuka kumuona yule binti akinifuata huku amefura na kunirushia ile chupi usoni ikiwa imeshafunguliwa kwenye package yake na kuanza kunipaka kwamba namuonaje hadi nampelekea chupi,? Kwamba nisimfananishe yeye na flani (yule niliemkimbia bar)
Kumbe yule binti kaeleza kampuni nzima?

Nimepata aibu ya milele leo

Hivi wakuu nimekosea wapi?
Kumpelekea mwanamke zawadi kuna ubaya?
Mbona tulikua tunaenda vizuri tu tangu juzi? Au ni sumu amepewa na yule binti mwingine?

akunyimae kunde akupunguzia mashuzi.....wazungu wanasema BLESSING IN DISGUISE!!!!!
 
Chai ya motoooooooooooooooo na jua hili sasa

Anyway unaanzaje kumpelekea zawadi ya chupi mtu hujamzoea????
 
Hadithi njoo hadithi njoo, ukweli njoo, uongo njoo, utam kolea.

Ulipoishia siku ile ilitosha kabisa, updates ungeleta kuhusu yule yule binti tu.

Leo kuchanganya na hili la kufuli, umeshajulikana kuwa ni muongo tena wa kutupwa.

Haha haha
 
inaonekana maofisini kuna vituko sana, mke wangu hatakaa aajiriwe ofisini
 
sasa na wewe mtu huna mahusiano nae unaanzaje kumnunulia zawad ya pichu, zawadi kama hizo ni kwa wapenzi bana maana unakua kwanza unajua size yake. ndo ukome muwe mnajua kutofautisha zawadi ya kumnunulia mpenzi na rafiki.kafanya sahihi sana kukurudishia, halafu kama huna hela ya kutosha usipende kualika watu kwenye kula, tabia chafu kumtoroka mwenzio kumwachia bill.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom