X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
Alikuwa akimchukia sana mamake, kisa alikuwa ana chongo
Mama yake alikuwa anafanya kazi ya uwalimu na kufanya biashara ya kupika kwenye maharusi, ili kuweza kumtunza mtoto wake pekee. Mtoto ambaye alikuwa akimsomesha shule ya bweni kule Tabora. Mama huyu alikuwa mjane, mumewe alifariki kwenye ajali ya gari, miaka mingi nyuma....
Siku moja alifunga safari kwenda kumtembelea mtoto wake kule shuleni. Mtoto wake hakufurahia ujio wa mama yake, na chuki yake ilionekana dhahiri kuwa amechukia.
"Kwanini huyu mwanamke anapenda kuja kuniaibisha kila mara," alijisemea moyoni, dharau zake kwa mama yake na kutojali kwake kulionekana wazi wazi usoni kwake.
Siku ya pili yake mwanafunzi mwenzake darasani alimuuliza kumbe wewe mama yako anajicho moja? kijana yule akamjibu yule si mama yangu, ni jirani yetu kule nyumbani...
Kwa kweli hakumpenda mama yake... alitamani apotelee mbali asimuone tena...
Au afe hasiwepo tena duniani...
Mama yake hakumchukia na wala hakuonyesha kisirani kwa mtoto wake
Kijana yule halisoma kwa bidii sana ili aweze kupata scholarship, ili atakapo rudi masomoni awe mbali na mama yake
Kwa bidii zake alifanikiwa kwenda kusoma nje ya nchi kwa miaka mitatu
Kwa miaka yote hiyo hakuwahi kuwasiliana na mama yake, na watu wakimuuliza kuhusu wazazi wake uwajibu kuwa walishafariki siku nyingi
Baada ya kumaliza masomo nje ya nchi, alirejea nchini na kununua nyumba, akaoa na baada ya miaka michache akapata watoto wawili
Akawa ni mtu mwenye furaha na maisha yake na familia yake
Siku moja mama yake ambaye sasa ashakuwa mzee sana, akaja kumtembelea, baada ya kuitafuta nyumba yake kwa takribani siku nne...
Mama yake alikuwa ametamani kumuona mwanaye kabla MMungu ajamchukuwa
Na pia alitamani kuwaona wajukuu zake
Alipokuwa akigonga mlango, wakatoka wajukuu zake walipomuona kibibi kizee chenye jicho moja wakacheka na kumwambia baba yao kuna omba omba kaja anaonekana ana njaa sana huku wakicheka
Mwanaye alipotoka kumuona huyo omba omba, akagunduwa kuwa si omba omba bali ni mama yake mzazi
Alimwangalia kwa jicho kali na dharau na huku akimkaripia hivi wewe kizee ujafa tuu . Na umekuja kufanya nini hapa unatisha watoto zangu
Toka nisikuone hapa hatuna chakula wala pesa za kukupa .
Yule mama akajibu kwa upole... samahani baba nimekosea nyumba nilifikiri hapa anaishi mtoto wangu Fulani !!
Kijana akajibu huna mtoto nyumba hii huna haya weee mwanamke !!
Yule mama huku akilia ndani ya nafsi yake akajiondokea taratibu huku akijikongoja kwa uzee
Wiki chake kupita, kijana akaletewa barua kutoka kwa wakili wa serikali. Wakili akamtaka aende ofisini kwake. Alipofika na kujitambulisha, wakili akamfahamisha kuwa mama yake ambaye alikuwa analelewa nyumba ya wazee amefariki siku tatu nyuma. Akampatia na barua kutoka kwa mama yake. Wakili akashangaa kwani kijana hakuonyesha hata kusikitika !!
Habari ya kufiwa haikumuuzunisha hata chembe
Aliporudi nyumbani akajifungia ndani peke yake na kuisoma barua hile...
Kwa mwanangu mpendwa... siku zote nilikuwa nakufikiria na kukuombea dua ufanikiwe...
Nakutaka msamaha sana kwa kuja nyumbani kwako na kusababisha kutishika kwa watoto zako, kwa kuwa mimi nilikuwa chongo...!!
Na pia nakutaka msamaha kwa vijana wote waliokuwa wakikutania kwa kuwa na mama ambaye ni chongo...
Mwanangu mpendwa... Tangia siku ile nilipokuja kwako, nilipata maradhi na sikuweza tena kutoka nje...!!
Nawashukuru sana hawa vijana wanao tutunza hapa kwenye nyumba ya wazee...!! kwa kuweza kututunza vyema...
Mwanagu mpendwa... kuna jambo moja ambalo nililificha miaka yote hii na leo nimeona nikuandikie hii barua kukufahamisha kile kilicho kuwa ni siri yangu...!!
Japokuwa utapokuwa ukiisoma barua hii... nitakuwa nimeshatangulia kwa Mola wangu...
Ulipokuwa mdogo ulipata ajali mwanangu.... wewe na baba yako. Baba yako alipoteza maisha kwenye ajali hiyo, na wewe ukapoteza jicho lako moja...
Mimi nikiwa ni mama yako sikufurahia kukuona ukiwa na jicho moja...
Lakini sikuwa najinsi ya kufanya...
Lakini nilijitahidi kutafuta pesa na nikachukuwa mkopo serikalini nikakupeleka nje ya nchi kufanyiwa operesheni ya jicho...!! Nikakubali kutolewa jicho langu moja kukupa wewe mwanangu ili uione dunia kwa macho mawili huwe ni mwenye furaha duniani na kukuepusha kuchekwa na watoto wenzio....
Wenzangu walishangaa sana kusikia kuwa nimetoa jicho langu kwa ajili yako mwanangu... lakini najivunia tendo langu hilo kwani ni tendo ambalo limenipa furaha ktk maisha yangu....
I was so proud of my son who was seeing a whole new world for me, in my place, with that eye.
With my love to you huo ni urithi pekee nilio weza kukupatia
Ndimi mama yako .
Binti Chongo
Mama yake alikuwa anafanya kazi ya uwalimu na kufanya biashara ya kupika kwenye maharusi, ili kuweza kumtunza mtoto wake pekee. Mtoto ambaye alikuwa akimsomesha shule ya bweni kule Tabora. Mama huyu alikuwa mjane, mumewe alifariki kwenye ajali ya gari, miaka mingi nyuma....
Siku moja alifunga safari kwenda kumtembelea mtoto wake kule shuleni. Mtoto wake hakufurahia ujio wa mama yake, na chuki yake ilionekana dhahiri kuwa amechukia.
"Kwanini huyu mwanamke anapenda kuja kuniaibisha kila mara," alijisemea moyoni, dharau zake kwa mama yake na kutojali kwake kulionekana wazi wazi usoni kwake.
Siku ya pili yake mwanafunzi mwenzake darasani alimuuliza kumbe wewe mama yako anajicho moja? kijana yule akamjibu yule si mama yangu, ni jirani yetu kule nyumbani...
Kwa kweli hakumpenda mama yake... alitamani apotelee mbali asimuone tena...
Au afe hasiwepo tena duniani...
Mama yake hakumchukia na wala hakuonyesha kisirani kwa mtoto wake
Kijana yule halisoma kwa bidii sana ili aweze kupata scholarship, ili atakapo rudi masomoni awe mbali na mama yake
Kwa bidii zake alifanikiwa kwenda kusoma nje ya nchi kwa miaka mitatu
Kwa miaka yote hiyo hakuwahi kuwasiliana na mama yake, na watu wakimuuliza kuhusu wazazi wake uwajibu kuwa walishafariki siku nyingi
Baada ya kumaliza masomo nje ya nchi, alirejea nchini na kununua nyumba, akaoa na baada ya miaka michache akapata watoto wawili
Akawa ni mtu mwenye furaha na maisha yake na familia yake
Siku moja mama yake ambaye sasa ashakuwa mzee sana, akaja kumtembelea, baada ya kuitafuta nyumba yake kwa takribani siku nne...
Mama yake alikuwa ametamani kumuona mwanaye kabla MMungu ajamchukuwa
Na pia alitamani kuwaona wajukuu zake
Alipokuwa akigonga mlango, wakatoka wajukuu zake walipomuona kibibi kizee chenye jicho moja wakacheka na kumwambia baba yao kuna omba omba kaja anaonekana ana njaa sana huku wakicheka
Mwanaye alipotoka kumuona huyo omba omba, akagunduwa kuwa si omba omba bali ni mama yake mzazi
Alimwangalia kwa jicho kali na dharau na huku akimkaripia hivi wewe kizee ujafa tuu . Na umekuja kufanya nini hapa unatisha watoto zangu
Toka nisikuone hapa hatuna chakula wala pesa za kukupa .
Yule mama akajibu kwa upole... samahani baba nimekosea nyumba nilifikiri hapa anaishi mtoto wangu Fulani !!
Kijana akajibu huna mtoto nyumba hii huna haya weee mwanamke !!
Yule mama huku akilia ndani ya nafsi yake akajiondokea taratibu huku akijikongoja kwa uzee
Wiki chake kupita, kijana akaletewa barua kutoka kwa wakili wa serikali. Wakili akamtaka aende ofisini kwake. Alipofika na kujitambulisha, wakili akamfahamisha kuwa mama yake ambaye alikuwa analelewa nyumba ya wazee amefariki siku tatu nyuma. Akampatia na barua kutoka kwa mama yake. Wakili akashangaa kwani kijana hakuonyesha hata kusikitika !!
Habari ya kufiwa haikumuuzunisha hata chembe
Aliporudi nyumbani akajifungia ndani peke yake na kuisoma barua hile...
Kwa mwanangu mpendwa... siku zote nilikuwa nakufikiria na kukuombea dua ufanikiwe...
Nakutaka msamaha sana kwa kuja nyumbani kwako na kusababisha kutishika kwa watoto zako, kwa kuwa mimi nilikuwa chongo...!!
Na pia nakutaka msamaha kwa vijana wote waliokuwa wakikutania kwa kuwa na mama ambaye ni chongo...
Mwanangu mpendwa... Tangia siku ile nilipokuja kwako, nilipata maradhi na sikuweza tena kutoka nje...!!
Nawashukuru sana hawa vijana wanao tutunza hapa kwenye nyumba ya wazee...!! kwa kuweza kututunza vyema...
Mwanagu mpendwa... kuna jambo moja ambalo nililificha miaka yote hii na leo nimeona nikuandikie hii barua kukufahamisha kile kilicho kuwa ni siri yangu...!!
Japokuwa utapokuwa ukiisoma barua hii... nitakuwa nimeshatangulia kwa Mola wangu...
Ulipokuwa mdogo ulipata ajali mwanangu.... wewe na baba yako. Baba yako alipoteza maisha kwenye ajali hiyo, na wewe ukapoteza jicho lako moja...
Mimi nikiwa ni mama yako sikufurahia kukuona ukiwa na jicho moja...
Lakini sikuwa najinsi ya kufanya...
Lakini nilijitahidi kutafuta pesa na nikachukuwa mkopo serikalini nikakupeleka nje ya nchi kufanyiwa operesheni ya jicho...!! Nikakubali kutolewa jicho langu moja kukupa wewe mwanangu ili uione dunia kwa macho mawili huwe ni mwenye furaha duniani na kukuepusha kuchekwa na watoto wenzio....
Wenzangu walishangaa sana kusikia kuwa nimetoa jicho langu kwa ajili yako mwanangu... lakini najivunia tendo langu hilo kwani ni tendo ambalo limenipa furaha ktk maisha yangu....
I was so proud of my son who was seeing a whole new world for me, in my place, with that eye.
With my love to you huo ni urithi pekee nilio weza kukupatia
Ndimi mama yako .
Binti Chongo