BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,355
- 8,043
Mzee Salum Bakari amesikitishwa na kitendo cha binti yake kuandika barua ya kuacha shule na kuuza sare zake kisha kutoroka nyumbani.
Akizungumza na Mwananchi nyumbani kwake amesema kuwa siku ya tukio aliitwa shuleni na Mkuu wa shule ambayo anasoma binti ake kidato cha kwanza.
“Kwanza alianza kuchelewa kurudi shule, anarudi muda ambao wengine wamesharudi, tukifuatilia tunagundua kuwa shuleni hajaenda na nyumbani hayupo ina maana yuko katikati ameenda wapi? Ilifikia wakati nikawa na mawasiliano ya mwanafunzi wenzie nijue maendeleo yake,” amesimulia.
“Kwakweli sikupata taarifa ya kuwa mwanangu ameandika barua, lakini niliitwa shuleni na nikapewa barua ya mtoto aliyoandika ya kutaka kuacha shule. Mtoto aliandika kuwa haelelewi anachofundishwa kwakuwa anaona kama anawasindikiza wengine lakini,” amesema.
“Alipokubali kwenda shule kazi ilikuwa kupata sare za shule kwakuwa alikuwa ameuziuza na daftari pia. Nililazimika kutatufuta sare kwa watoto waliomaliza shule hiyo, nilipomwambia akafuate akasema sawa, na ilipofika saa 8 mchana alitoroka nyumbani mapaka sasa hajarudi,” amesema baba yake mzazi.
“Siku za nyuma nimewahi kumkamata akiwa anatembea na wanaume tofauti tofauti jambo lile sikulipenda kwakuwa niliona kuwa ni mtoto mdogo na hata nilipojaribu kufuatilia ili kujua alipo bado kwangu ni kitendawili kwakuwa nyumbani hayupo,” amesimulia.
Ofisa Elimu Kata Naliendele. Benjamin Ndossi amesema kuwa baadhi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza na vidato vya juu katika Shule ya Sekondari Naliendele wanaacha shule kwa kuandika barua.
“Yaani mzazi anakuja na mtoto shuleni wakiwa wameongozana tayari ameshaandika barua ya kukataa shule kisa haelewi lugha, kibaya zaidi mzazi akiulizwa na mwalimu anasema kuwa nitafanyaje kama mtoto ameamua mwenyewe kukataa shule,” amesema.
Diwani Kata ya Naliende, Masoud Dali alisema kuwa sisi kama viongozi jukumu letu kubwa ni kuhakikisha kuwa watoto wanarejea shuleni na kuendelea na masomo.
“Hii tabia ya kuwaacha na kuridhika na maamuzi ya watoto haifai na tunaikemea kwa nguvu zote inawezekanaje mzazi unakubaliana na mtoto kuwa aache shule wakati serikali imeweka mikakati ya kuhakiksiha kuwa tunatengeneza mazingira rafiki kwa wanafunzi hatuwezi kukubali watoto wachukue maamuzi yenye madhara kwao kwa siku zijazo,” amesema Dali.
MWANANCHI
Akizungumza na Mwananchi nyumbani kwake amesema kuwa siku ya tukio aliitwa shuleni na Mkuu wa shule ambayo anasoma binti ake kidato cha kwanza.
“Kwanza alianza kuchelewa kurudi shule, anarudi muda ambao wengine wamesharudi, tukifuatilia tunagundua kuwa shuleni hajaenda na nyumbani hayupo ina maana yuko katikati ameenda wapi? Ilifikia wakati nikawa na mawasiliano ya mwanafunzi wenzie nijue maendeleo yake,” amesimulia.
“Kwakweli sikupata taarifa ya kuwa mwanangu ameandika barua, lakini niliitwa shuleni na nikapewa barua ya mtoto aliyoandika ya kutaka kuacha shule. Mtoto aliandika kuwa haelelewi anachofundishwa kwakuwa anaona kama anawasindikiza wengine lakini,” amesema.
“Alipokubali kwenda shule kazi ilikuwa kupata sare za shule kwakuwa alikuwa ameuziuza na daftari pia. Nililazimika kutatufuta sare kwa watoto waliomaliza shule hiyo, nilipomwambia akafuate akasema sawa, na ilipofika saa 8 mchana alitoroka nyumbani mapaka sasa hajarudi,” amesema baba yake mzazi.
“Siku za nyuma nimewahi kumkamata akiwa anatembea na wanaume tofauti tofauti jambo lile sikulipenda kwakuwa niliona kuwa ni mtoto mdogo na hata nilipojaribu kufuatilia ili kujua alipo bado kwangu ni kitendawili kwakuwa nyumbani hayupo,” amesimulia.
Ofisa Elimu Kata Naliendele. Benjamin Ndossi amesema kuwa baadhi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza na vidato vya juu katika Shule ya Sekondari Naliendele wanaacha shule kwa kuandika barua.
“Yaani mzazi anakuja na mtoto shuleni wakiwa wameongozana tayari ameshaandika barua ya kukataa shule kisa haelewi lugha, kibaya zaidi mzazi akiulizwa na mwalimu anasema kuwa nitafanyaje kama mtoto ameamua mwenyewe kukataa shule,” amesema.
Diwani Kata ya Naliende, Masoud Dali alisema kuwa sisi kama viongozi jukumu letu kubwa ni kuhakikisha kuwa watoto wanarejea shuleni na kuendelea na masomo.
“Hii tabia ya kuwaacha na kuridhika na maamuzi ya watoto haifai na tunaikemea kwa nguvu zote inawezekanaje mzazi unakubaliana na mtoto kuwa aache shule wakati serikali imeweka mikakati ya kuhakiksiha kuwa tunatengeneza mazingira rafiki kwa wanafunzi hatuwezi kukubali watoto wachukue maamuzi yenye madhara kwao kwa siku zijazo,” amesema Dali.
MWANANCHI