Bingo ya 15,000$ ukitoa siri ya nani ana document za Balali

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Nikiwa nimekaa naangalia mpira na kama kawaida mara umeme umekatika napata sms toka kwa Kalunyungu .Kaninieleza kwamba sasa Serikali ya CCM imeamua kupanda dau nalo ni 15,000$ kama utatoa taarifa ya nani ana document alizo acha Balali .

Nina aambiwa JF wana kasi ya ajabu kwa sasa kumpata mwenye nazo .Amesha kuwa located kazi sasa ni kumfanya alegee atoe na JF wazimwage jinsi zilivyo bila ya kungoja .Je na wewe unasikia haya ninayo yapata muda huu ??

Stay tune maana muda wowote waweza kuona baadhi maandishi ya Marehemu Balali hapa ubaoni .Serikali haitaki hilo na UWT hawalali wanataka document hizo .
 
Lunyungu,

Kumbe na wewe huna data? serikali watatoa hizo pesa wakati wanajua walikomficha Ballali?

Endelea kuwa Mdanganyika!
 
napata sms toka kwa Kalunyungu .Kaninieleza kwamba sasa Serikali ya CCM imeamua kupanda dau nalo ni 15,000$ kama utatoa taarifa ya nani ana document alizo acha Balali .

Mkuu Lunyungu,

Heshima mbele kaka, maneno mazito haya si unajua kuwa kwa muoga huenda kicheko, lakini kwa shujaa huenda kilio, maana asiyejua maana huwa haaambiwi maana, kwa sababu mtaka cha uvunguni either ageuze kitanda au ainame, nimekusikia mkuu, na nimekubali!

Mkuu Wangu Mtanzania,

Sio rahisi kuzuia mwanga wa jua asubuhi kwa kutumia kiganja cha mkono, maana utakushinda tu!
 
Mkuu Mtanzania kwenye hili naona uko nyuma .Ama hujaelewa nasemaje .Wao wanatafuta data ambazo Balali ameacha nyuma hawamtafuti Balali .Data ziko katika mikono ya watu baadhi yao ni Watanzania, wana CCM , mawakili Tanzania na kulingana na dondoo ambazo tumeziona na kwa jinsi ilivyo kuwa ukweli wa EPA mengi Balali aliyasema so wanazitafuta mimi sasa ndiye nakupa data kaa utulie uone what next .
 
Samahani mkuu naomba ufafanuzi, hao UWT wanahusikaje? Na wao wametajwa kwenye ufisadi? Au ni UWT nyingine nisiyoifahamu mimi - Umoja wa wanawake Tz, ile jumuiya ya ccm?
 
Lunyungu,
Nasubiria mamo Ubaoni hapa. Hapo ndipo serekali ya JK watapagawa na kuchanganyikiwa, kama ilivyo kwa ripoti ya EPA
 
Haya wakuu!! sisi yetu macho... na kubofya tu... www,jamiiforums.com twasubiri, tusiokuwa nazo hatuna haja ya kuwakatisha tamaa tusubiri...
 
Samahani mkuu naomba ufafanuzi, hao UWT wanahusikaje? Na wao wametajwa kwenye ufisadi? Au ni UWT nyingine nisiyoifahamu mimi - Umoja wa wanawake Tz, ile jumuiya ya ccm?

Wewe ni Senior and Expert Member na hujui UWT ni nini:) Ni Usalama wa Taifa.
 
Mkuu Mtanzania kwenye hili naona uko nyuma .Ama hujaelewa nasemaje .Wao wanatafuta data ambazo Balali ameacha nyuma hawamtafuti Balali .Data ziko katika mikono ya watu baadhi yao ni Watanzania, wana CCM , mawakili Tanzania na kulingana na dondoo ambazo tumeziona na kwa jinsi ilivyo kuwa ukweli wa EPA mengi Balali aliyasema so wanazitafuta mimi sasa ndiye nakupa data kaa utulie uone what next .

Lunyungu,

Hakuna data, hakuna video, hakuna audio, hakuna mikanda. Endelea kusubiri ila niambie lini utaamini umefungwa bao ili ikifika wakati huo unipe mji?

Wewe rudia threads za Ballali na utaona wazi uwongo ni ule ule. Watu wamevujisha EPA, budget ya serikali ndio ziwe kanda za Ballali tena ambazo eti kuna watu kibao wamekabidhiwa?

Amka mkuu, kwenye siasa hakuna siri maana kila mtu ana interest zake, sio mliona jinsi
Mbowe uzalendo ulivyomshinda pamoja na kuambiwa ni siri, akaamua kutoa habari za kifo cha Ballali? Hakuweza kuvumilia maana aliona hapo kuna uwezekano wa kuwarushia mawe CCM.

Fumbo mfumbie mjinga, mwerevu hung'amua. Wengine tulishaona ni changa la macho toka siku ile ile wanatangaza kifo.

Tulivyowapiga mawe watetezi wa Ballali hapa mpaka wengine wakapoteza composure, kungekuwa na data wangeshazitoa ili kuwaumbua akina Mtanzania, Mwafrika wa Kike na wengine lakini si umeona wakizidiwa wanaleta matusi. Ukiona mtu anatukana, ni dalili tosha hana data.
 
Lunyungu,

Hakuna data, hakuna video, hakuna audio, hakuna mikanda. Endelea kusubiri ila niambie lini utaamini umefungwa bao ili ikifika wakati huo unipe mji?

Wewe rudia threads za Ballali na utaona wazi uwongo ni ule ule. Watu wamevujisha EPA, budget ya serikali ndio ziwe kanda za Ballali tena ambazo eti kuna watu kibao wamekabidhiwa?

Amka mkuu, kwenye siasa hakuna siri maana kila mtu ana interest zake, sio mliona jinsi
Mbowe uzalendo ulivyomshinda pamoja na kuambiwa ni siri, akaamua kutoa habari za kifo cha Ballali? Hakuweza kuvumilia maana aliona hapo kuna uwezekano wa kuwarushia mawe CCM.

Fumbo mfumbie mjinga, mwerevu hung'amua. Wengine tulishaona ni changa la macho toka siku ile ile wanatangaza kifo.

Tulivyowapiga mawe watetezi wa Ballali hapa mpaka wengine wakapoteza composure, kungekuwa na data wangeshazitoa ili kuwaumbua akina Mtanzania, Mwafrika wa Kike na wengine lakini si umeona wakizidiwa wanaleta matusi. Ukiona mtu anatukana, ni dalili tosha hana data.


Mkuu Mtanzania .Ubishi wa Balali kafa ama hajafa mie sitaki kuingia huko .Ndiyo maana utaona kwamba sikuwahi kuandika lolote katika ule mjadala ila kuna ninacho kiamini ukisema hapa JF watakuvaa tu ndiyo maana mjadala ule niliacha uendelee.Leo naongelea maandiko ya Balali awe hai ama amekufa yanapatikana kwa baadhi ya watu .Nasema we are working on getting them na yatamwagwa hapa .Hili ndilo muhimu kwangu na kw amuda huu.Upande wa BoT na serikali wamesha sema na wao hawana la kuongeza.Tunataka kuona Balali yeye alikuwa na yapi wakati wa matukio haya yanatokea ?
 
Mkuu Mtanzania .Ubishi wa Balali kafa ama hajafa mie sitaki kuingia huko .Ndiyo maana utaona kwamba sikuwahi kuandika lolote katika ule mjadala ila kuna ninacho kiamini ukisema hapa JF watakuvaa tu ndiyo maana mjadala ule niliacha uendelee.Leo naongelea maandiko ya Balali awe hai ama amekufa yanapatikana kwa baadhi ya watu .Nasema we are working on getting them na yatamwagwa hapa .Hili ndilo muhimu kwangu na kw amuda huu.Upande wa BoT na serikali wamesha sema na wao hawana la kuongeza.Tunataka kuona Balali yeye alikuwa na yapi wakati wa matukio haya yanatokea ?

Lunyungu,

Hata mimi naongelea documents hizo hizo, toa tarehe, tukusubiri mpaka lini kabla hujatoa mji?

Hizo documents unazozisema hazipo labda kama unataka tusubiri mpaka 2015.

Leakes zote za Ballali zinafanywa kwa makusudi mazima yenye lengo la kuwadanganya Watanzania, wajanja walishang'amua mapema.
 
Mtanzania unajua kama majina ya watu weney documents yanajulkana na JF we are at work tutaujua ukweli .Kama ni mambo ya kupikwa mimi nasema hayatadumu .Kwa sasa nina stick na what I am telling you now .Hadi hapo nitakapo ona kwamba kuna longo longo lakini kwa sasa nasema JF iko kazini si Lunyungu pekee bali hata wewe unaweza kuibua kabla sijapata na kuweka hapa .Hakuna uongo ulio jificha miaka kadhaa .
 
Mtanzania unajua kama majina ya watu weney documents yanajulkana na JF we are at work tutaujua ukweli .Kama ni mambo ya kupikwa mimi nasema hayatadumu .Kwa sasa nina stick na what I am telling you now .Hadi hapo nitakapo ona kwamba kuna longo longo lakini kwa sasa nasema JF iko kazini si Lunyungu pekee bali hata wewe unaweza kuibua kabla sijapata na kuweka hapa .Hakuna uongo ulio jificha miaka kadhaa .

Lunyungu,

Sawa tutasubiri lakini tupe tarehe. Wengine tulijaribu kufuatilia na kugundua ni changa la macho tu kama lile la uchawi kule Dodoma.

Endelea ndugu yangu na mafanikio mema.
 
Nikiwa nimekaa naangalia mpira na kama kawaida mara umeme umekatika napata sms toka kwa Kalunyungu .Kaninieleza kwamba sasa Serikali ya CCM imeamua kupanda dau nalo ni 15,000$ kama utatoa taarifa ya nani ana document alizo acha Balali .

Nina aambiwa JF wana kasi ya ajabu kwa sasa kumpata mwenye nazo .Amesha kuwa located kazi sasa ni kumfanya alegee atoe na JF wazimwage jinsi zilivyo bila ya kungoja .Je na wewe unasikia haya ninayo yapata muda huu ??

Stay tune maana muda wowote waweza kuona baadhi maandishi ya Marehemu Balali hapa ubaoni .Serikali haitaki hilo na UWT hawalali wanataka document hizo .

Typical Lunyungu!!!
 
Nasema we are working on getting them na yatamwagwa hapa .Hili ndilo muhimu kwangu na kw amuda huu.Upande wa BoT na serikali wamesha sema na wao hawana la kuongeza.Tunataka kuona Balali yeye alikuwa na yapi wakati wa matukio haya yanatokea ?

Mkuu Lunyungu, hapa tupo ukurasa mmoja respect!
 
US 15,000 ndogo sana kwa CCM watoe dau zaidi!..kitu kama asilimia 10 ya fedha zote...I mean kitu kama 1.5 millioni..
Mkimtaka Saadam muhimu dau liwe la uhakika laa sivyo JF itazipokea na kuzitoa buree kwa faida ya wananchi wote!
 
Back
Top Bottom