Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu kama ni kulia tutalia wote hakuna hospitali ya wanaCCM pekee, au nauli ya daladala ya wana CCM ni tofauti na ya ACT-Wazalendo.Zote hizo ni hasira za kushindwa na mtalia sana
Hakika miaka kumi iliyopita tulikuwa utumwani MISRI. Asante Bwana Yesu kwa ukombozi huu.
Alialikwa wapi wakati alijipendekeza mwenyewe......
Subiri nikishaapishwa kama Magufuli....Magufuli akiamua sasa hivi anajipendekeza fasta anakwepia pipa mpaka DC....ila mambo hayo wanayo waswahili tu....Kajipendekeze na wewe kwa Obama kama ni rahisi.
Subiri nikishaapishwa kama Magufuli....Magufuli akiamua sasa hivi anajipendekeza fasta anakwepia pipa mpaka DC....ila mambo hayo wanayo waswahili tu....
Mwambie leo Kikwete amwalike Obama kama hata kusikilizwa atasikilizwa.Thubutu ujipeleke tu kumuona Obama bila mualiko rasmi. White House utaiona paa tu kama anavyoiona Ikulu Lowassa, kama anahamu hata ya kupita njia ile.
Mswahili alikwenda US kwa mambo mengine kabisa baadae akaomba kuonana na Obama akakubaliwa...hakukuwa na mwaliko kama unavyofikiri....Thubutu ujipeleke tu kumuona Obama bila mualiko rasmi. White House utaiona paa tu kama anavyoiona Ikulu Lowassa, kama anahamu hata ya kupita njia ile.
Naomba unitafasirie mkuu, sijakuelewa
Hata mi nimefurahi anavyoondoka.
If I speak I will speak a lot let me spear my words until further
times. Within a month if not three months time I will be able to talk on this topic otherwise at the moment am puzzled.
Kweli mkuu nina wasiwasi naye inawezekana ndio wale "kalio thinkers"Nani amelia kumpata Magufuli utakuwa unachanganya mambo.
Wanajamii kichwa cha habari cha jieleza, nimeshitushwa na kichwa cha gazeti hili na maneno ya chini yake maana kwa kiasi kikubwa yanamuhusu Rais mstaafu, Je! Yana ukweli wowote, vipi jawa jamaa hawatapigwa rungu tena kwa maneno yao haya??
Vp hii miaka mitatu ya jiwe?Kipigo nilichokipata tangu Kikwete aingie madarakani na 'declare' siku ya leo kama sikukuu kwangu, nasherehekea kwa sababu zifuatazo,
- Naachana na rais ambaye hakuwa serious kulingana na umuhimu wa ofisi yake,
- Rais aliyetumia zaidi ya nusu ya uongozi wake akiwa nje akitumia kodi yangu badala ya kuwatumikia wananchi wake,
- Rais asiyethamini taaluma za watu wakiwemo waalimu, wauguzi yeye ni siasa tu,
- Rais asiyejali mihimili mingine,
- Rais aliyetuhumiwa kwa kila dili EPA yumo, Richmond yumo, Merameta yumo, Escrow yumo, what type of a president,
- Hakuipenda nchi nchi yake kwa dhati, tangu aseme pesa zetu siyo za umma niliumia sana,
- Maliasili zinahamishwa yeye hakujali,
- Rais aliyekuza udini na ukanda "rais hawezi toka kaskazini" hakuonekana kukemea,
- Rais aliyetuambia anayo majina ya wauza unga hadi leo anaondoka nayo,
- Rais anayesamehe wezi wakubwa wa EPA wakati wadogo wakiozea jela,
- Rais aliyependa vijembe kwa wananchi wanaotofautiana naye,
- Rais aliyetumia ofisi kwa maslahi yake na familia yake.
Nikuyakumbuka haya na mengine mengi hakika leo nasherehekea kuondoka kwake na wala siyo kuapishwa kwa Magufuli.