Bukyanagandi
JF-Expert Member
- Jun 24, 2009
- 11,061
- 16,743
Hata mimi hicho kilinishangaza kidogo! Kwani Rais Magufuli hawezi kubatilisha utehuzi huo? Mashirika ya UMMA ya umuhimu wa pekee kama TTCL alipaswi kufanyiwa mchezo, mimi kwa mfano sipati picha kwa nini baadhi ya Viongozi Serikalini walikuwa wanaipigia debe Kampuni ya simu ya VietNam wanawapatia projects ambazo zinapaswa kufanywa na TTCL kwani waliwambia TTCL haina uwezo wa kutekeleza projects hizo - wanapiga vita shirika la UMMA sijui kwa maslahi ya akina nani? Mh.Magufuli chunguza sana ujio nchini wa Kampuni hii ya VietNam na ijulikane bayana mkataba wake na Serikali ulihusu nini hasa,sio wanatumia mbinu za kutaka kuidhoofisha TTCL wakishirikiana na viongozi wenye ubinafsi - kuna kitu hakija kaa sawa hapa.Sio hiyo tu, baada ya kubakiza siku 2 ofisini kaendelea kuteua maswahiba wake, ni juzi tu kateua m/kiti wa bodi ya wakurugenzi TTCL haya si matumizi mazuri ya ofisi halafu sio busara.