Binadamu wa kawaida au ni kiumbe

habari ya hapa

JF-Expert Member
Dec 20, 2012
12,793
8,739
Nina rafiki yangu amekutana na makubwa baada ya kukutana na mwanadada mrembo maendeo ya Posta mpya wiki tatu zimepita, baada ya kukutana alikuja kwangu na huyo mchumba wake kunitambulisha kuwa nimepata wifi yako na ninampenda sana nahitaji kufunga nae ndoa baada ya mwaka mmoja km mungu akitupa uzima.

Hiv karibuni rafiki yangu alinipigia akanambia kuhusu hayo anayoyaona kwa huyo bibie, anasema kwanza hapendi pombe mchumba wangu nimejaribu kumwelewesha kuwa nipe muda pombe nitaacha amekuwa mgumu kunielewa, tumekuwa tukipishana sana kuhusu suala hili.
Anasema, ananiweka kwa wakati mgumu mchumba wangu kwani kila nilolifanya ninapokuwa kwa shughuli zangu ninaporudi nyumbani yote mchumba wangu hunaambia kuwa leo umekutana na Fulani, umefanya hiv na vile ili hali ni kweli hayo anayoambiwa nakuwa nimefanya.


Leo asubuhi amekuja nyumbani kwangu mapema km saa moja, nikamuuliza kulikoni mapema yote hii, akasema jana wakati niilirudi nyumbani mchumba wangu alinifungulia mlango lkn wakati naingia sikumwona niliwasha taa lkn ckuona mtu hapo mlangoni na nilipoingia chumbani nilimkuta kalala na ili hali mlango ulikuwa umefungwa swali nililojiuliza huyu bibie amefunguaje huo mlango, bac ili bidi nitulie kidogo.


Nilichukua chakula mezani kwani tayari alikuwa kishakiandaa nikala nikaingia chumbani alikuwa kawasha TV hivyo kulikuwa na mwanga na yeye yupo kitandani kalala lkn si usingizi, pale pale alipo lala akanyanyua mkono akawasha taa, wakati bado nashangaa kile nimekiona akaniambia leo umekunya pombe, na pia ulipotoka kazini umeenda kuzini na msichana (akamtaja kwa jina) na umemsindikiza na gari hadi nyumbani kwao, (ili hali ni kwlei nimefanya yote aliyokuwa akiniambia), swali ninalojiuliza amejuaje? kwa kweli mwili wote umekufa ganzi siamini yale niliyoona na niliyosikia toka kwake hiv ninavyokwambia usiku sikulala nimeshindwa na sasa hiv nahama pale nyumbani namuachikia kila kitu, alimaza kwa kusema, isiwe tabu vitu vinatafutwa na uhai hautafutwi.

NB: Huyu kaka ni mtu ambaye ni rafiki yangu sana, sasa kwa hili nilishindwa hata nimshaurije ndo maana nimelileta kwenu nanyi mtoe mawazo yenu ili niyafikishe kwani sasa hiv ni kweli kahama kwake yupo hotel wakati anasubiri apate nyumba nyingine na kila kitu kaacha hivyo anaanza maisha upya.

 
Safi sana,anajua ana mchumba kwa nini alienda kuzini??hiyo ni mwanzo tuu na akienda huko kwingine atamkuta tena...
 
Hilo ni jini, aende kwenye maombi upesi kabla halijamnyongelea mbali! Jamani watoto wa kiume punguzeni zoa zoa!
 
Nina rafiki yangu amekutana na makubwa baada ya kukutana na mwanadada mrembo maendeo ya Posta mpya wiki tatu zimepita, baada ya kukutana alikuja kwangu na huyo mchumba wake kunitambulisha kuwa nimepata wifi yako na ninampenda sana nahitaji kufunga nae ndoa baada ya mwaka mmoja km mungu akitupa uzima.

Hapo kwenye bold...................huyu mvulana ni halali yake jini

btw uliliomba hilo jini ruhusa ya kuuleta huu uzi hapa au umekurupuka tu
 
Msaada wangu kwa huyo rafiki yako aende kwenye maombi na si kuhama nyumba kwani hilo ni jini na linaweza mfuata popote.
 
Ngoja likurudie na wewe na kimbelembele chako! Leo akirudi usiku atasimuliwa kuwa amekwambia wewe na wewe ukaiweka JamiiForums. Kalale kwa mganga vikindu vinginevyo imekula kwako. (JUST A JOKE):heh::heh:
 
Hapo kwenye bold...................huyu mvulana ni halali yake jini

btw uliliomba hilo jini ruhusa ya kuuleta huu uzi hapa au umekurupuka tu


hapana sijaomba ruhusa ila nafuta jinc ya kumsaidia rafiki yangu
 
Ngoja likurudie na wewe na kimbelembele chako! Leo akirudi usiku atasimuliwa kuwa amekwambia wewe na wewe ukaiweka JamiiForums. Kalale kwa mganga vikindu vinginevyo imekula kwako. (JUST A JOKE):heh::heh:


umenichekesha kweli me ni maombi akija kwangu atakutana na moto
 
ndo akome kukurupukia wadada asio wajua kisa urembo wao.huyo mdada atakuwa jini tu.nainawezekana hao wadada alioenda kudili nao ni yeye mwenyewe ili ampime uaminifu wake.chamsingi aache pombe.uzinzi na kila aina ya dhambi amludie mungu wake na kusali kweli sio kwa maigizo.maana majini hayakimbiw kizembezembe ajitoe kweli kwa mungu.ni hayo tu cjui wengine....
 
huyo rafiki atafatwa hata huko hotelini. bora ahamie nyumba ya ibada kama anaweza.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom