Bill Gates: We Must Depopulate Africa to Save Europe

CHANJO IPO NJIANI NCHINI TANZANIA... MUJINDAE.........



4ba3e855-da94-49ad-b87b-bb8299a0e1a3.jpg
 
168551960_2145457372257437_7708179639673365409_n.jpg


168880956_2145452572257917_9187788203733997412_n.jpg


VIRUSI VYA CORONA: WATU SABA WAFARIKI BAADA YA KUTUMIA CHANJO YA ASTRAZENECA NCHINI UINGEREZA.
Watu saba wamefariki nchini Uingereza kutokana na damu kuganda mwilini baada ya kupewa chanjo ya Oxford-AstraZeneca, mamlaka ya kudhibiti dawa imethibitishia BBC.
Kwa ujumla wato 30 kati ya milioni 18 waliopewa chanjo hiyo kufikia Machi 24 wamekabiliwa na hali ya damu kuganda.
Bado haijulikani ikiwa ni bahati mbaya tu au athari ya kweli ya chanjo.
Shirika la udhibiti wa Dawa na Bidhaa za Afya linanasema faida ya chanjo zinaendelea kuzidi madhara yake.
Hata hivyo, hali ya kuganda kwa damu kwenye ubongo, kitaalamu "cerebral venous sinus thrombosis" au CVSTs zimesababisha nchi nyingine - zikiwemo Ujerumani, Ufaransa na Canada - kudhibiti utumizi wa chanjo hiyo.
Shirika la Afya duniani na Wakala wa Dawa wa Ulaya wanasema faida za chanjo hiyo huzidi hatari zozote.
Data zilizotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Dawa (MHRA) siku ya Ijumaa, zilionesha kuwa watu 22 walipata hali ambayo kwa lugha ya kimatibabu inafahamika kama cerebral venous sinus thrombosis (CVST) ambayo ni aina fulani ya mgando wa damu kwenye ubongo.
Hii ilifuatiwa na na viwango vya chini vya seli, zinazosaidia damu kuganda, mwilini. MHRA pia ilibaini watwengine wanane walikabiliwana tatizo la damu kuganda mwilini.
Sasa MHRA imethibitishia BBC kupita barua pepe, kwamba "inasikitika watu saba wamefariki ".
Dkt June Raine, Afisa mkuu mtendaji wa MHRA, amesema: "Manufaa… ya kudhibiti maambukizi ya Covid-19 na changamoto zake yanaendelea kuwa juu kuliko hataru yoyote kwa hiyo watu wakubali kupewa chanjo wakiombwa kufanya hivyo."
Uchunguzi wa kubaini ikiwa chanjo ya AstraZeneca inasababisha hali isiyokuwa ya kawaida ya damu kuganda mwilini, inaendelea.
Mapema wiki hii Shirika la Dawa la Muungano wa Ulaya lilisema "halijathibitisha, lakini kuna uwezekano".
Kuna mambo mawili yanatia hofu. Kwanza hali isiyokuwa ya kawaid ya damu kuganda, inayojumuisha viwango vya chini vya seli zinazosaidia damu kuganda na kingamwili adimu katika damu ambazo zimehusiishwa na tatizo la damu kuganda.
Suala lingine linalojitokeza kuhusu usalama wa chanjo ni tofauti kati ya chanjo ya Oxford-AstraZeneca na Pfizer-BioNTech.
Kumeshuhudiwa visa viwili vya damu kuganda kwenye ubongo (CVST) baada ya watu kutumia chanjo ya Pfizer nchini Uingereza, kati ya watu zaidi ya milioni 10 waliochanjwa watu, lakini hawakuwa na viwango vya chini vya seli ya inayosaidia damu kuganda.
2px presentational grey line
Hatari inaweza kuwa kubwa kiasi gani?
Inabaki uwezekano kabisa kuwa hatari haipo kwani chanjo hazijathibitishwa kusababisha kuganda kwa damu kwenye ubongo.
Taasisi ya Paul Ehrlich ya Ujerumani imeripoti visa 31 na vifo tisa kati ya watu milioni 2.7 waliopewa chanjo huko.
Hatahivyo, data za hivi karibuni za Uingereza ziliripoti visa vitano tu, kati ya watu zaidi ya milioni 11 waliopewa chanjo.
Shirika la Dawa la Ulaya, ambalo limetathmini data kutoka kote ulimwenguni, linakadiria kuwa kuna hatari moja kati ya 100,000 ya CVST kwa watu walio chini ya umri wa miaka 60 ambao wamepewa chanjo ya AstraZeneca.
Mkuu wa ufuatiliaji wa usalama wa shirika hilo, Dk Peter Arlett, alisema hiyo ni "zaidi ya tunavyotarajia kuona".
Hatahivyo, haijulikani ni kweli kiasi gani kuhusu kiwango cha hali hii kujitokeza kwenye ubongo hapo kabla. Makadirio yanatofautiana kutoka kwa karibu kesi mbili kwa watu milioni kila mwaka hadi karibu 16 katika kila watu milioni kwa nyakati za janga la corona yenyewe inaweza kuwa inasababisha pia.
Chanjo ya AstraZeneca ni salama?
Hakuna usalama kwa asilimia mia moja katika dawa na hata tiba ambazo ni hatari hutumiwa katika mazingira yanayofaa.
Dawa za tiba ya mionzi zina athari mbaya, lakini zina thamani kubwa; na hata dawa za kutuliza maumivu kama paracetamol na ibuprofen zina athari mbaya, ni nadra sana.
Uamuzi huegemea kwa kutazama faida zinazozidi hatari.
Hii ni changamoto haswa katika janga la corona. Kawaida dawa inategemea "kanuni ya tahadhari" kuthibitisha usalama wa kutosha kabla ya kutoa dawa mpya kwa idadi kubwa ya watu. Lakini katika janga hilo, ucheleweshaji wowote wa chanjo ya watu pia utagharimu maisha.
Kulingana na data ya Ujerumani peke yake, ikiwa chanjo ya watu milioni moja basi unatarajia watu 12 watakuwa na tatizo la damu kuganda na wengine wanne watakufa.
Lakini ikiwa watu milioni wenye umri wa miaka 60 watapata virusibasi karibu 20,000 watakufa na Covid-19. Ikiwa watoto milioni 40 wa miaka wanapata virusi hivyo basi karibu 1,000 hufa. Ingekuwa watu mia chache katika miaka yao ya 30.
Faida za chanjo huongezeka kwa kutegemea umri na nchi kama Ujerumani na Canada zimeruhusu chanjo ya AstraZeneca kutumika katika vikundi vya wazee. Uamuzi huu pia utasababishwa na chanjo mbadala ambazo zinapatikana na ni nani bado anahitaji kupatiwa chanjo.
Ulimwengu unachunguza data kwa nguvu, lakini majibu yatachukua muda.. chanzo. https://www.bbc.com/swahili/habari-56624943
 
hili suala la chanjo ni tata. niliona clip mahali mdada wa kiisraeli analia akielezea jinsi gani watu waliogoma chanjo wanavyonyanyasika nchini. inaonekana huko mbeleni itakuwa ni lazima na sio hiari kuchanjwa.
 
hili suala la chanjo ni tata. niliona clip mahali mdada wa kiisraeli analia akielezea jinsi gani watu waliogoma chanjo wanavyonyanyasika nchini. inaonekana huko mbeleni itakuwa ni lazima na sio hiari kuchanjwa.
Ma-Free-Mason wana lengo lao lakuwapunguza idadi ya watu duniani. Wanatumia pesa kwa nguvu ili wanazilazimisha Serikali Dhaifu na Masikini Kuchanja nguvu ili watimize yale waliyo yakusudia kuwa wauwa watu ili wapate watu duniani kupunguwa. Kwa kiasi fulani wamefanikiwa sana haswa Barani Afrika Baadhi ya Viongozi waliopo Madarakani wana njaa ya pesa wakisha onyeshwa pesa na wazungu basi chochote watakacho sema Wazungu hawatapinga.Wako tayari wawamalize Wananchi wao wanyonge ili wapate kumfurahisha mzungu. Baadhi ya Viongozi waKiafrika wana roho mbaya juu ya Wananchi wao.

50ffff94-bed7-4b08-8bbc-71dc26059889.jpg
 
Bill Gates never said β€˜3 billion people need to die’
By ALI SWENSON
January 26, 2021
CLAIM: Microsoft co-founder Bill Gates wants to eliminate at least 3 billion people in the world, starting in Africa, in a plot involving vaccines.

AP’S ASSESSMENT: False. Gates never said this. The billionaire philanthropist has spoken about the benefits of slowing the rate of population growth, but he has not advocated killing people.

THE FACTS: A 2019 video falsely claiming Gates wants to depopulate the globe is circulating online anew this month as COVID-19 vaccines become more widely available in the United States and elsewhere.


ADVERTISEMENT

Instagram and Twitter posts containing the video made the further unsubstantiated claim that Gates wanted to use mandatory vaccines as part of his plan to eliminate billions of people.

The video shows naturopath Robert O. Young speaking on a panel for the International Tribunal for Natural Justice, an independent, U.K.-based group that holds β€œhearings” and β€œtrials” and whose members have promoted baseless conspiracy theories about 5G technology and the coronavirus.

Young, who has previously been convicted for practicing medicine without a license and was ordered to pay $105 million to a woman who said he advised her against traditional cancer treatment, claimed without evidence that Gates planned to kill billions of people, starting in Africa.

β€œIn the words of Bill Gates, at least 3 billion people need to die,” Young said. β€œSo we’ll just start off in Africa, we’ll start doing our research there, and we’ll eliminate most of the Africans because they’re deplorable. They’re worthless. They’re not part of this world economy.”

A review of public statements by Gates found nothing matching these claims. Young’s statement appeared to misrepresent comments Gates made during a TED Talk in 2010, when he said vaccines and improved health care could help reduce the rate of global population growth and, as a result, lower carbon emissions.

β€œThe world today has 6.8 billion people,” Gates said during the talk. β€œThat’s headed up to about 9 billion. Now, if we do a really great job on new vaccines, health care, reproductive health services, we lower that by perhaps 10 or 15%.”

ADVERTISEMENT

Gates was talking about reducing the rate of population growth, not the population, by 10 or 15%.

In past interviews, Gates has argued that improving vaccines and health care can paradoxically slow the rate of population growth in poor countries, because it lowers the child mortality rate. With more children making it to adulthood, Gates has said, parents may choose to have a smaller family size.

β€œAmazingly, as children survive, parents feel like they’ll have enough kids to support them in their old age, so they choose to have less children,” Gates said in a 2012 interview.

Gates has been a frequent target of vaccine and coronavirus conspiracy theories in recent months, several of which The Associated Press has debunked.


The Bill and Melinda Gates Foundation and the International Tribunal for Natural Justice did not respond to requests for comment.

___

This is part of The Associated Press’ ongoing effort to fact-check misinformation that is shared widely online, including work with Facebook to identify and reduce the circulation of false stories on the platform.

Here’s more information on Facebook’s fact-checking program:
Nimelia..... Nalia.....😭😭😭😭😭😭
 
Msweet ni uongo. Mitandaoni kuna uongo mwingi sana kuhusu mambo mbali mbali likiweno hili la Bill Gates.

Makampuni na biashara zinahitaji watumiaji wengi wa bidhaa ili kupata faida zaidi
Sasa Bill Gate eti aseme watu 3b wafe yeye hataki faida kwa hao 3b?
Ni logic tu
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Huyo muanzisha uzi yuko busy kusambaza uongo wake ambao hauna kichwa wala miguu.
Makampuni na biashara zinahitaji watumiaji wengi wa bidhaa ili kupata faida zaidi
Sasa Bill Gate eti aseme watu 3b wafe yeye hataki faida kwa hao 3b?
Ni logic tu
 
169433875_886426291922287_267011437125622966_n.jpg
169601548_886426331922283_8928490446559029605_n.jpg


MH: RAIS SAMIA SULUHU HASSAN CORONA VIRUS COVID 19 NI FREEMASON 666 SHETANI LUCIFER.
NAKUSHAURI ACHANA NA CORONA VIRUS COVID 19, HAKUNA KINGA, TIBA WALA MATIBABU YA KISAYANSI, ZAIDI YA KUOMBA MUNGU ALIE HAI KTK JINA LA YESU KRISTO WA NAZALETI. (fuata nyayo za Hayati Rais John Joseph Magufuri, utashinda achana na Hiyo Tim.)

UKIIPOKEA CORONA VIRUS COVID 19 TU, KITI CHA URAIS ULICHO KALIA KITAKUSHINDA.
Daniel 5:25 Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; MENE, MENE, TEKELI, NA PERESI.
(Mh: Rais Samia Suluhu Hassan, nisipo kwambia Ukweli, nitadaiwa, unapotea.)

NIMEFANYA UTAFITI WA KISAYANSI KUHUSU CHANJO YA CORONA VIRUS, COVID 19 NIMEONI NI UWONGO MTUPU, NI MPANGO WA SHETANI IBIRISI LUCIFER KUKAMILISHA MIPANGO YAKE.
UTAFITI WA CHANJO YA CORONA VIRUS COVID 19.

(1)Hakuna Sayansi Duniani ambayo inaruhusu chanjo kwa Mtu/Watu wazima, hakuna hii kitu, Wala hakuna Sayansi ya namna hii Duniani.

(2) Kisayansi chanjo inahusu watoto, ukifosi Chanjo au ukilazimisha basi mtu asizidi umri wa miaka 18 - full stop, hii miaka 18 ni Chanjo ya kulazimisha.

(3) Sayansi gani inaruhusu chanjo kwa Watu wazima? Miaka 30 + kwenda mbele, mtu ana miaka 60 + anapewa chanjo !!!!!! Sijawahi ona Sayansi ya namahii huyu ni Shetani tu hakuna Sayansi hapa, wizi tu.

(4)Kama Tanzania Kuna Madaktari bingwa na bobezi waniambie hii Sayansi ya chanjo kwa Watu wazima walio Soma wapi, Nchi gani na Chuo gani?

UTAFITI NCHI ZILIZO POKEA CHANJO.
Wingereza na Chanjo yao ya Astrazeneca wamechanja watu wakafa kabisa na Waziri husika akasema tutaishi na Corona virus Kama mafua mengine hakuna Lock Down.
Afrika kusini ilipokea chanjo ikasitisha baada ya kuona haisaidii chochote zaidi ya kutia hasara pesa za walipakodi.
Kenya walipokea chanjo na wanazidi kuchanjwa na ndio wanazidi kufa na Lock Down ndio inazidi kila mkoa.
Marekani, Brazili na Wingereza huko ndio wanachanjwa kila siku na lock down juu na ndio wanaongoza kwa idadi ya vifo.

UTAFITI UNAONYESHA, MADAKTARI 95% WANATAKA LOCK DOWN, CHANJO NA BARAKOA.
Swala la Corona virus Covid 19 ni swala la Kiroho, Sio swala la kimwili Kama mnavyo lichukulia.
Mh: Rais Samia suluhu Hassan, huu ni ushauri tu sio lazima.
Mwisho,
Nendeni mkamuulize Khamisi Kigwangara ile ajari alio nusurika kufa ilisababishwa na nini? Alikua anataka kufanya nini ndio yakamtokea hayo?
Najua mengi Sana na Siri nyingi Sana, Mungu Alie hai haniruhusu kufunguka, ila kaeni mkijua kabla hamjafanya Wala halijatokea lolote Mimi najulishwa kabla.
Mh:Rais Samia suluhu Hassan, Mengine sio Makofi ya heri ni makofi ya Shari na hatari.
Kama utapokea Corona Virus Covid 19, Makamo wako wa Rais, atakua Rais sio wewe Tena.
Mwalimu na Mtumishi lsack Malila Ebenezer live.
 
_117786054_gettyimages-1232025237.jpg

Chanjo ya AstraZeneca inasababisha hatari ya damu kuganda kwenye ubongo ?​


Mabonge ya damu yasiyo ya kawaida kwenye ubongo yamegunduliwa kwa watu wachache baada ya kudungwa chanjo ya Oxford-AstraZeneca.
Hali hii ya kuganda kwa damu kwenye ubongo, kitaalamu "cerebral venous sinus thrombosis" au CVSTs zimesababisha nchi nyingine - zikiwemo Ujerumani, Ufaransa na Canada - kuzuia ni nani anaweza kupewa chanjo. Shirika la Afya duniani na Wakala wa Dawa wa Ulaya wanasema faida za chanjo hiyo huzidi hatari zozote.
Wanasayansi na wasimamizi wa usalama wa dawa ulimwenguni wanajaribu kujua ikiwa chanjo inasababisha athari hizi, ni hatari gani kubwa inaweza kuwa na inaweza kuwa na maana gani katika programu za chanjo.

Chanjo husababisha damu kuganda?​

Kwa sasa, hatufahamu.
Wakala wa Dawa Ulaya (EMA), ambao wamekuwa wakipitia data za usalama, wanasema "hawajathibitisha, lakini inawezekana".
Shirika linapaswa kufahamu ikiwa kuganda kwa damu kulikokripotiwa ni athari ya baada ya chanjo au bahati mbaya ambayo ingeweza kutokea kawaida. Hii ni ngumu sana wakati wa kushughulika na masuala ambayo ni nadra kutokea . Ikiwa, kwa upande mwingine, mtu mmoja kati ya kila watu 10,000 ataripoti kutokea kwa hali ya kuganda damu basi jibu litakuwa dhahiri.
Nimezungumza na wanasayansi wanaoheshimika ambao wengine wana wasiwasi, wengine wanazidi kushawishika.
Hali isiyo ya kawaida ya kuganda damu huwa kama ishara ya kitu kinachoendelea. Mara nyingi huonekana wakati huo huo kukiwa na viwango vya chini vya chembe chembe za damu, ambazo ni moja wapo ya dalili kubwa na kingamwili zinazohusiana na shida nyingine za kuganda zinazoonekana kwenye damu.
Wengine wanasema hakuna ushahidi wa kutosha na kesi zilizoripotiwa zinaweza kuwa si sababu ya Covid, bali yenyewe inahusishwa na kuganda kusiko kwa kawaida.

Hatari inaweza kuwa kubwa kiasi gani?​

Inabaki uwezekano kabisa kuwa hatari haipo kwani chanjo hazijathibitishwa kusababisha kuganda kwa damu kwenye ubongo.
Taasisi ya Paul Ehrlich ya Ujerumani imeripoti visa 31 na vifo tisa kati ya watu milioni 2.7 waliopewa chanjo huko.
Hatahivyo, data za hivi karibuni za Uingereza ziliripoti visa vitano tu, kati ya watu zaidi ya milioni 11 waliopewa chanjo.
Shirika la Dawa la Ulaya, ambalo limetathmini data kutoka kote ulimwenguni, linakadiria kuwa kuna hatari moja kati ya 100,000 ya CVST kwa watu walio chini ya umri wa miaka 60 ambao wamepewa chanjo ya AstraZeneca.
Mkuu wa ufuatiliaji wa usalama wa shirika hilo, Dk Peter Arlett, alisema hiyo ni "zaidi ya tunavyotarajia kuona".
Hatahivyo, haijulikani ni kweli kiasi gani kuhusu kiwango cha hali hii kujitokeza kwenye ubongo hapo kabla. Makadirio yanatofautiana kutoka kwa karibu kesi mbili kwa watu milioni kila mwaka hadi karibu 16 katika kila watu milioni kwa nyakati za janga la corona yenyewe inaweza kuwa inasababisha pia.
Chanjo ya AstraZeneca ni salama?
Hakuna usalama kwa asilimia mia moja katika dawa na hata tiba ambazo ni hatari hutumiwa katika mazingira yanayofaa.
Dawa za tiba ya mionzi zina athari mbaya, lakini zina thamani kubwa; na hata dawa za kutuliza maumivu kama paracetamol na ibuprofen zina athari mbaya, ni nadra sana.
Uamuzi huegemea kwa kutazama faida zinazozidi hatari.
Hii ni changamoto haswa katika janga la corona. Kawaida dawa inategemea "kanuni ya tahadhari" kuthibitisha usalama wa kutosha kabla ya kutoa dawa mpya kwa idadi kubwa ya watu. Lakini katika janga hilo, ucheleweshaji wowote wa chanjo ya watu pia utagharimu maisha.
Kulingana na data ya Ujerumani peke yake, ikiwa chanjo ya watu milioni moja basi unatarajia watu 12 watakuwa na tatizo la damu kuganda na wengine wanne watakufa.
Lakini ikiwa watu milioni wenye umri wa miaka 60 watapata virusibasi karibu 20,000 watakufa na Covid-19. Ikiwa watoto milioni 40 wa miaka wanapata virusi hivyo basi karibu 1,000 hufa. Ingekuwa watu mia chache katika miaka yao ya 30.
Faida za chanjo huongezeka kwa kutegemea umri na nchi kama Ujerumani na Canada zimeruhusu chanjo ya AstraZeneca kutumika katika vikundi vya wazee. Uamuzi huu pia utasababishwa na chanjo mbadala ambazo zinapatikana na ni nani bado anahitaji kupatiwa chanjo.
Ulimwengu unachunguza data kwa nguvu, lakini majibu yatachukua muda.
 
169498045_491263592065987_7832324000296197418_n.jpg


Sipingani na huyu mama ila sisi wa Afrika wazungu bado wanatutawala kifikra
πŸ‘¨β€πŸ’»
ndiyo maana utawala wa Magufuli ulikuwa mgumu sana na ilikuwa siyo rahisi kumuelewa na kwa kizazi cha sasa ni vigumu kumuelewa
πŸ‘¨β€πŸ’»
sisi wa Afrika tabia yetu ni wabinafsi waliowengi hatuna chetu tuna changu kitu ambacho wazungu hawana
πŸ‘¨β€πŸ’»
wazungu wanathamini chao nchi nyingi za ulaya zimejengwa kwa raslimali za Afrika
πŸ‘¨β€πŸ’»
Marais wengi wa Afrika wamekuwa wakienda ulaya na vibakuli kuomba misaada wakati mzungu alitakiwa kuja Afrika na kibakuli kutuomba misaada
πŸ‘¨β€πŸ’»
mzungu mtoto wake anasomeshwa bure kuanzia la chekechea mpaka form four mtoto anakwenda shule na mkate uliowekwa kila kikombwezo na juice pembeni hata mtoto wa mlala hoi
πŸ‘¨β€πŸ’»
ulaya hawana aridhi ya kulima mazao kama Afrika tulivyojaaliwa lakini vijana wetu hawaachi kumsifia mzungu kwamba ndiye mkombozi wake wakati muafrika ndiye mkombozi wa mzungu hii yote ni uroho wa marais wa Afrika
πŸ‘¨β€πŸ’»
marais wetu wanavuta hela zao na kutuaminisha wa Afrika kwamba nchi zetu ni za ulimwengu wa 3 hatuwezi kumbe wamekuwa wakijilimbikizia mali
πŸ‘¨β€πŸ’»
wakati tuna uwezo vijana wetu kuwaajili kwa raslimali zetu wenyewe tungeweza kusomesha watoto wetu wakabeba mkate na vikolombwezo kibao , tuna mifugo , tuna ardhi tuna vyakula vya asili lakini mzungu kaanza kuingiza mavyakula yake wameuwa mashamba yetu kwa mbolea zao
πŸ‘¨β€πŸ’»
vijana wa Afrika hasa Tanzania amkeni hamjachelewa Magufuli katuamsha kaacha alama nyuma , kataeni chanjo zao mtu anakwambia eti polio na vyandarua wanatuletea wao, siyo kweli hizo ni biashara zao
πŸ‘¨β€πŸ’»
mfano mama samia akikubali chanjo yeye hapo atapiga hela wazungu watapiga hela tukishindwa kulipia hela kitalu c kimeondoka
πŸ‘¨β€πŸ’»
sikatai utawala wa Magufuli hela ilikuwa ya shida lakini alikuwa anatengeneza kesho yetu , nafikiri Mungu angetuachia Magufuli miaka 10 watanzania tungekuwa na uhakika wa maisha na kizazi kijacho
πŸ‘¨β€πŸ’»
na kingine kwa Magufuli watangulizi wake ndiyo walioharibu kwenda na vibakuli ulaya kuomba omba na kusain mikataba feki
πŸ‘¨β€πŸ’»
Rais samia , Rais samia , Rais samia , nchi nyingi za ulaya wamechemsha lockdown Tanzania hata kama kuna corona hakuna ya hivyo sana mbona ? usijaribu lockdown, utauwa watu watu watakuchukia mama , kuwa na moyo wa kizalendo mama
RIP Dady Magufuli
 

Askofu Gwajima aitahadharisha Serikali kuhusu chanjo za corona​


gwajima-pc.jpg

Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima akizungumza bungeni alipokuwa akichangia mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, jijini Dodoma leo. Picha na Edwin Mjwahuzi


Summary

  • Mbunge wa Kawe (CCM), Askofu Josephat Gwajima ameshauri Serikali kuwa makini na madhara yanayoweza kujitokeza kwa wananchi iwapo Taifa litaruhusu chanjo ya ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya corona kutumika nchini
By Sharon Sauwa
More by this Author

Dodoma. Mbunge wa Kawe (CCM), Askofu Josephat Gwajima ameshauri Serikali kuwa makini na madhara yanayoweza kujitokeza kwa wananchi iwapo Taifa litaruhusu chanjo ya ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya corona kutumika nchini.

Gwajima ameyasema hayo leo Jumanne Mei 11, 2021 wakati akichangiwa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto mwaka 2021/22.

Amesema hayuko kinyume na chanjo bali yuko makini na aina ya chanjo za ugonjwa huo.

Huku akitaja aina tatu za chanjo ya ugonjwa huo, amebainisha kuwa ni tofauti na chanjo nyingine zilizokuja duniani ambazo zilikuwa zikichukua kati ya miaka nane hadi 10 kabla ya kuanza kutumiwa.

β€œNi chanjo za mwendo kasi unapojaribu kuuliza kwa nini inakuwa haraka wanasema sababu ni kukuwa kwa teknolojia, wamemobilize resources na pandemic,” amesema.

Amesema aina hiyo ya chanjo haijajulikana kuwa atazaliwa mtu wa namna gani baada ya miaka 10, kwamba kwa kawaida chanjo zote kabla ya kutumika ni lazima ziwe zimeruhusiwa na taasisi za nchini Marekani za CDC na FDA.
Hata hivyo, amesema chanjo ya corona hazikuruhusiwa na taasisi hizo bali zimeruhusiwa na mamlaka ya dharura ambayo inasema madhara yanayotokana na chanjo hiyo ni juu ya mtumiaji mwenyewe.

β€œSerikali na wizara ya afya wawe makini wanapochagua chanjo hizi waangalie madhara ya sasa, siku zijazo na Taifa. Tatizo tulilonalo ni kudhani kila kinachotoka Ulaya kinatufaa sisi,” amesema.

Ameitaka wizara ya Afya kabla kuamua kuitumia wawe na wataalam watakaoangalia kwa makini vitu vilivyomo kwenye chanjo hiyo na matatizo watakayoyapata watu watakaozaliwa baadaye.

Amesema ni ujinga mkubwa kuruhusu majaribio ya chanjo hiyo kwa Watanzania wote kwa sababu ya haraka.
chanzo.https://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/askofu-gwajima-aitahadharisha-serikali-kuhusu-chanjo-za-corona-3396356
 
Back
Top Bottom