Hospitali ya Mkoa wa Singida ipo hoi hakuna hata panadol za kutuliza maumivu, dawa za kawaida kabisa katika hospitali, vituo vya afya, na Zahanati. Kuna Mwanafunzi wa Chuo cha Uhasibu amefika hospitalini amebanwa na kifua akaambiwa akanunue dawa ili aje kuchomwa Sindano. Turudi nyuma kidogo jana watu walikuwa wanamsifia Mbunge wa Jimbo hilo kuwa anatumia pesa nyingi kusaidia. Vipi juu ya suala hili, mbona hospitali ipo hoi muda mrefu. Hivi Mbunge mwenyewe ana taarifa kuwa watu huwa wanaugua? atafikishiwa vipi taarifa, kila mara yupo nje ya nchi kushughulikia biashara zake na kurudi kuja kujisifu kuwa anachangia mihela yote kila kitu utadhani serikali haifanyi wajibu wake kwa watu wa Singida. Anyway serikaliw wajibikeni haraka kwa Tatizo la Singida Mjini Hospitali ya Mkoa sasa ni Critical Issue