Bilioni 50 zinazodaiwa kurudishwa BOT kumbe changa la macho

Sawa waliwageuzia mashitaka kuwa deni's hata kuwataja majina wanashindwa? na waliowapeleka mahakamani si watalipa hizo hela kama mahakama ikijiridhisha walijiEPA? mambo mengine bwana, manatuharibia POSE CCM!
 
Abdulhalim, haisaidii kuponda kila kinachosemwa.

Sawa, hatukutegema tofauti na kinachoendelea, lakini ndio tukae kimya? Sote tunajua impact ya majadiliano ya humu JF. Wahusika huwa wana pita pita humu, kama sio tunajadiliana nao humu bila kujua.

Hivyo, kufufua ishu kama hii ni muhimu katika kusukuma ufuatiliaji

Sio mbaya kua na matumaini na mategemeo. Tatizo ni kutegemea kuvuna madafu kwa kupanda chelewa.
 
Ule ulikuwa usanii tuuu, pesa yote ile irudishwe, pale mkulu lazima anahusika ndo maana akawadanganya eti pesa imerudishwa, hana lolote.
Haswa ndo maana waziri mkuu alisema hawa watu hawakamatiki. wakikamatwa serikali itayumba reference alikuwa ni mkulu-rais.
 
Nchi yetu italiwa sijui hadi lini.
Hadi hapo kutakapokuwa hakuna cha kuliwa tena:(

Ungejua jinsi wanavyoteseka wala usingesema!!! Hawana uwezo kwa vile kule ndo kwenye ufisadi zaidi. Wale wazalendo na wanajeshi wenye akili wote wamecha jeshi na nani unaona siku hizi anajiunga zaidi ya wale wanaokosa ajira sehemu nyingine. Waliopo anaona wapo kwa favour tu ndo maana wamekaa hawaongei. wanasubiri wakatiwe maji wakapige utafikiri jeshi la 1907 linaloamini kila kitu ni nguvu na vitisho.
Wasomi wazuri wapo wengi tu ndani ya geshi ila ndo hivyo tena ile sera ya Nyerere ya Siasa geshini ili politicize geshi. Wote wanafikiria Ukuu ama wa Mkoa au Wilaya. Chukulia mfano wa Kombe aliyekuwa kamanda wa Usalama barabarani na aliwahi kuwa mkuu wa Polisi Arusha amedai yeye ni kada mzuri wa CCm tangu zamani sasa kweli huyu wakati akiwa madarakani aliacha ukada wake?

Ni kweli tuna Wanasiasa wanao vaa nguo za jeshi, hatuna jeshi. Kama jeshi litatwaa madaraka kwa nguvu watwaaji watakuwa ni Masajenti na makoplo hawa wengine hawawezi dhubutu.
Hao ndio kabisa wala usitegemee. Mtu ambaye imemchukua miaka 25 kuwa koplo na anakaribia kustaafu apate 1.5m kama kiinua mgongo unadhani atafikiria ku-risk? Hata kama itamchukua miaka mingine kumi ya kufuatilia malipo yake.

Huko Jeshini wanaogopana kupita kiasi maana usalama wa taifa wamewaingilia kwenye kila kona. Ndio maana ma-Sajent wameamua kuwa majambazi wa kutumia silaha na hawana mpango na mapinduzi kama wale waliomtishia Nyerere.

tatizo ni kuwa ni lini yatatokea au mpaka tutakapochinjana?
Hiyo hapo kwenye red ndio suluhu iliyobaki maana amani (in our case heshima) haiji bila ncha ya upanga.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom