Bilioni 50 zinazodaiwa kurudishwa BOT kumbe changa la macho

Jk Alijua Mapinduzi Ya Kijeshi Yanaweza Tokea Na Ndiyo Maana Amemuweka Nchimbi Na Mwinyi Mahala Pale Maana Ni Maswahiba Lakini Sidhani Kama Taaluma Zao Zinaendana Na Wadhifa Waliopewa
 
Naomba kuuliza hizi bilioni 50 zangu na wananchi wenzangu ziko wapi?

Inabidi tuulize mapema manake kuna kitu inaitwa "kilimo kwanza" ambayo inaweza pewa tafsiri isiyo rasmi = khanga na kofia za uchaguzi
 
Naomba kuuliza hizi bilioni 50 zangu na wananchi wenzangu ziko wapi?

Inabidi tuulize mapema manake kuna kitu inaitwa "kilimo kwanza" ambayo inaweza pewa tafsiri isiyo rasmi = khanga na kofia za uchaguzi

Na sare za kijani kama hizi katika kuelekea October 2010






Maulid ya Mtume (S.A.W) Mikocheni kwa Warioba jiji Dar katika uwanja wa Lauret Int. School. ambapo Mama Salma Kikwete alikuwa mgeni rasmi na kuhudhuriwa na Mama Sitti Mwinyi na viongozi na wanawake wa kiislam toka maeneo mbalimbali

kinamama katika maulid hiyo



sare za kijani zilitawala maulidini hapo

utulivu na usikivu vilitawala​
 
Mkulu wa pale magogoni ndie aliyekuwa front kutusanii. Issue yeyote inayomhusisha RA mkulu hafurukuti bana.
 
Ngoja niendelee kumsikiliza Marijani Rajabu maana hawa wana siasa wanaharibu utaratibu wangu wa siku
 
Mie sikuamini kama hizi pesa zimerejeshwa since then nadhani huu ni mwendelezo tu wa yaliyojiri sio zaidi. Wewe utawezaje kuiba mabilioni ya shilingi halafu uyalipe within few months haingii akilini hata kidogo ni danganya toto hamna lolote. Hawa jamaa kwanza wapelekwe jela na sio kudaiwa kama wakopaji hilo litakuwa kosa kubwa Tanzania inalifanya
 
at time it hard and deeply giving pain to read about this issue.
 
Ule ulikuwa usanii tuuu, pesa yote ile irudishwe, pale mkulu lazima anahusika ndo maana akawadanganya eti pesa imerudishwa, hana lolote.
 
at time it hard and deeply giving pain to read about this issue.

the deepest pain will come kama wakipindisha sheria. Maana watakaokuja baada ya hapo watarefer to the EPA case (case laws)kama evidence na matokeo yake watashinda kesi zao na kuondoka na mabilioni yetu na nchi ikiangamia.
 
Kingine ninachojiuliza ni hiki: kwanini vyombo vya habari Tanzania vinaendeshwa kwa mtindo wa "Breaking News" au "News just in" halafu baada ya hapo hakuna ufuatiliaji?

Au ndio hizo milioni 5 wanazopewa kwenye baraza la wahariri zinawanyamazisha? Yaani kweli hata chombo kimoja kisifuatilie?
 
Kwa sasa kila Mtanzania mwenye nafasi ya kuiba na aibe! Ukikamatwa ingia mkataba wa kurudisha polepole!
 
Hivyo ndio watu wetu na serikali yetu ndio ilivyo hivyo basi hakuna shaka kuwa inapaswa kufanya hivyo maana wangepata wapi pesa hizo ndio maana watu wakauliza kuwa kuwa na ushahidi maalumu kabisa kuliko suala ya mkataba maana halina maana yoyote ile
 
Tumezoea kudanganywa.Wkt ikitangazwa na JK kwamba fmabilioni hayo yamerejeshwa tulitakiwa tuhoji ni akina nani hasa wamerejesha na fedha hizo zimetumika kiasi gani na kwa vipi.Tulikubari kirahisi tu kama ilivyo kawaida.Nchi yetu italiwa sijui hadi lini.
 
Tumezoea kudanganywa.Wkt ikitangazwa na JK kwamba fmabilioni hayo yamerejeshwa tulitakiwa tuhoji ni akina nani hasa wamerejesha na fedha hizo zimetumika kiasi gani na kwa vipi.Tulikubari kirahisi tu kama ilivyo kawaida.Nchi yetu italiwa sijui hadi lini.

Ilihojiwa. Nakumbuka. Jibu likatolewa kuwa tusitake sana kujua ni akina nani mradi pesa zimerudishwa.

Sisi ndio wadau wa hii nchi jamani. Tunatakiwa tupewe mshindo nyuma (feedback) na hawa watu tunaowalipa mshahara!!
 
Hivi ninyi mlitegemea kitu gani tafauti? nashindwa kuwashangaa ati.


Abdulhalim, haisaidii kuponda kila kinachosemwa.

Sawa, hatukutegema tofauti na kinachoendelea, lakini ndio tukae kimya? Sote tunajua impact ya majadiliano ya humu JF. Wahusika huwa wana pita pita humu, kama sio tunajadiliana nao humu bila kujua.

Hivyo, kufufua ishu kama hii ni muhimu katika kusukuma ufuatiliaji
 
Back
Top Bottom