Bilioni 40 /- za mafisadi zanufaisha wakulima

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Bilioni 40 /- za mafisadi zanufaisha wakulima
Mwandishi Wetu
Daily News; Friday,December 19, 2008 @21:15

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wassira amesema wakulima nchini wameanza kunufaika na fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) kwa kuongeza thamani ya vocha kwa ajili ruzuku za mbolea na mbegu.

Alisema thamani ya vocha hizo zimeongezeka na kufikia Sh bilioni 70.7 ambalo ni ongezeko la Sh bilioni 40 za EPA na tayari mawakala wamewasilisha vocha za malipo za Sh bilioni nne. Rais Jakaya Kikwete aliamuru kuwa fedha zilizorejeshwa na mafisadi wanaotuhumiwa kuchota Sh bilioni 133 katika akaunti hiyo ya Benki Kuu ya Tanzania zitakwenda kusaidia sekta ya kilimo.

Tayari Sh bilioni 70 zimesharejeshwa na watuhumiwa hao ambao kati yao, 21 wameshapandishwa mahakamani wakituhumiwa kwa wizi huo. Akizungumza Dar es Salaam jana kuhusu ufikishwaji wa pembejeo za ruzuku kwa wakulima kwa kutumia vocha, Wassira alisema fedha hizo zinanufaisha wakulima 700,000 huku Benki ya Dunia ikiahidi kusaidia fedha kwa wakulima 300,000 kuanzia msimu huu wa kilimo hivyo kunufaisha jumla ya wakulima milioni moja.

Alisema matumizi ya vocha yatamnufaisha mkulima moja kwa moja bila kupitia kwa wakala mwenye vigezo vya kuwa mkulima mdogo mwenye uwezo wa kufidia tofauti za bei na atakayefuata maelekezo ya Ofisa Ugani. Alisema aina za mbolea zinazopata ruzuku ni mbolea za kupandia na za kukuzia na kuwatoa hofu wakulima nchini kuwa mbolea ya Minjingu inafaa kama kirutubisho cha fosfati kwani imefanyiwa utafiti wa kutosha na kuonekana inafaa.

“Tumefanya utafiti katika Wilaya ya Kilombero Morogoro na Igomela na Mbarali Mbeya ambako wakulima wa mpunga wa Kijiji cha Mkula wameweza kuongeza uzalishaji kutoka wastani wa gunia sita kwa ekari hadi gunia thelathini kwa ekari kwa kutumia mbolea hiyo ya Minjingu,” alisema.

Kuhusu upungufu wa chakula, Waziri alisema watu 240,000 wanakabiliwa na upungufu huo na serikali inatakiwa kupeleka tani 7,000 za chakula kwa ajili ya kusaidia wilaya kadhaa zinazokabiliwa na upungufu wa chakula. Alitaja baadhi ya wilaya zinazokabiliwa na upungufu wa chakula kuwa ni Longido, Same, Monduli, Mwanga, Rombo, Bunda, Musoma Vijijini, Rorya, Kwimba na Ukerewe, lakini alisema wilaya hizo ni kwa sehemu ndogo na hali ya chakula nchini ni ya kuridhisha.
 
Hapa kuna usanii na ufisadi wa hali ya juu. Watanzania hatujapewa hata list ya wahusika wote wa ufisadi waliorudisha pesa na pia kuambiwa kila mmoja amerudisha kiasi gani. Sasa leo hii tunaambiwa kwamba shilingi 40 billioni zimeshatolewa kwa wakulima!!!! Na hatuna ushahidi wowote kuhakikisha pesa hizo kweli zimetolewa kwa wakulima au zimewekwa kwenye bank account ya chama cha mafisadi.

Naona hapa Watanzania tumeliwa hakuna pesa yotote iliyorudishwa na mafisadi wa BoT. Kama ni kweli zimerudishwa na sababu zipi hasa zinazoifanya serikali ipate kigugumizi cha hali ya juu kutoa list ya waliorudisha pesa hizo na ziliwekwa wapi ili Watanzania tuhakikishe ukweli wa kauli zilizotolewa na JK, Mkullo na wengineo!!?
 
Duh...ama kweli Watanzania tutia huruma...Rais kwa masikio yangu nilisikia akisema Fedha zinakwenda kwenye fungu litalotumika kuanziasha Benki ya Wakulima...."Benki" kwa sababu hili ni "long term solution" sio kwenda kwenye ruzuku ya mbolea kwa wakulima wanaotegemea mvua...Au mimi nina matatizo ya masikio jamani...Raisi hakusema "Benki ya Wakulima"?
 
Hivi kwa nini wasisubiri chrismas ipite ndio waje na huu uongo wao,kweli bado tuna safari ndefu,halafu mtu mmoja anatuamulia jinsi yakutumia hizi pesa.sasa wamekula kidhibiti wakati hata kesi bado.
Kweli ****** ya sufuria hayaogopi moto.
 
Naombeni9 mtu mwenye ufahamu anisaidie kuhusu hii Voucher ya Mkulima. How does it work?
 
Kuna njemba inajiita umushoshoro inaelekea ni kada wa chama imenitumia PM hii hapa chini.

Bubu,
Inafikia wakati tufanye mambo yetu kisayansi.

Bezo zako zimekaa kama zinatokea kijiweni kwa wanywa kahawa ambao wanaongzwa na huba na chuki katika kuchangia mada zinazoibuikia kijiwe husika.

Badala ya kutaka serikali itaje waliorudisha na zimewekwa akaunti gani kwa nini usiende mahakamani ukapate nguvu ya kisheria kuilazimisha serikali badala ya kuumiza kichwa chako na kunung'unika kwa jambo rahisi sana.

Asante kwa muda wako
 
Duh! njemba inataka tupambane na mafisadi kisayansi!!!...haya tunasubiri utupe darasa la jinsi ya kupambana na mafisadi kisayansi.

Serikali inadai mafisadi wa BOT wamerudisha karibu 70 billoni, serikali inajua fika kwamba credibility yake imeshuka mno, hivyo kwa maoni yangu ili kujenga tena credibility hiyo hawana budi kutoa list ya mafisadi wote waliorudisha pesa na kiasi walichorudisha na zimewekwa katika bank gani na watoe bank account #. Kinyume na hivyo ni usanii tena wa hali ya juu.

Kama utakumbuka serikali hii hii ndiyo ilianza kumshinikiza Dr Slaa alipotua tuhuma za ufisadi BoT na kumuita muongo na anataka kuleta machafuko nchini na hatimaye umwagaji wa damu. Viongozi wa juu wa serikali hii akiwemo Waziri Mkuu Pinda, Mwanasheria Mkuu Mwanyika na Mkuu wa polisi walitamka hadharani kwamba mafisadi wa EPA ni matajiri wa kupindukia wakikamatwa nchi itawaka moto.

Sasa wewe unatwambia tufanye mambo kisayansi!!! Haya tunasubiri darasa lako la kufanya mambo kisayansi.

Weekend njema.
 
hakuna fedha iliyorudi. Fedha itakuwa imerudi pale tu itakapowekwa bayana ni nani nakurudisha nini, na alirusha wapi?
Vile vile kwa sababu kuna wizi na usanii ndani yake lazima mkaguzi binafsi wa kimataifa mwenye sifa na uzoefu asiyehongeka kukagua mahesabu hayo na kuweka ripoti adharani. La sivyo wajinga ndio waliwao.
 
Kuna njemba inajiita umushoshoro inaelekea ni kada wa chama imenitumia PM hii hapa chini.

Bubu,
Inafikia wakati tufanye mambo yetu kisayansi.

Bezo zako zimekaa kama zinatokea kijiweni kwa wanywa kahawa ambao wanaongzwa na huba na chuki katika kuchangia mada zinazoibuikia kijiwe husika.

Badala ya kutaka serikali itaje waliorudisha na zimewekwa akaunti gani kwa nini usiende mahakamani ukapate nguvu ya kisheria kuilazimisha serikali badala ya kuumiza kichwa chako na kunung'unika kwa jambo rahisi sana.

Asante kwa muda wako


He has a point...lakini kila mmoja wetu anapambana pale anapoweza.
 
Mabilioni ya EPA sasa yamchanganya Wasira, Mkullo adai hajui chochote kuhusu pesa hizo

2008-12-20 14:33:54
Na Mashaka Mgeta

Wakati baadhi ya watu wakiendelea kuhoji kuhusu fedha zilizorejeshwa na baadhi ya watu walioziiba kutoka kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Waziri wa Chakula, Kilimo na Ushirika, Stephen Wasira amejichanganya wakati wa kuzitolea ufafanuzi.

Akilihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano mjini Dodoma Agosti 21, mwaka huu, Rais Jakaya Kikwete alisema ameagiza fedha hizo zirejeshwe na kuelekezwa Wizara ya Chakula, Kilimo na Ushirika katika mfuko wa pembejeo kupitia Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB).

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Wasira alisema sehemu ya fedha hizo, zimeanza kutumika katika mpango wa ruzuku ya mbolea inayotolewa kwa kutumia vocha kwa wakulima wa baadhi ya mikoa hapa nchini.

Wasira, alisema fedha zilizotokana na marejesho ya EPA, zilichangia kwa kiasi kikubwa kufanikisha utekelezaji wa mpango huo.

Hata hivyo, Wasira hakutaja kiasi cha fedha zilizoelekezwa kwa mpango huo kutoka katika fungu la marejesho ya EPA, kwa madai kuwa mfumo wa utoaji wake kwa wizara hiyo, ulifuata utaratibu wa kawaida wa Hazina.

Nipashe ilipowasiliana na Mkulo kwa njia ya simu jana kwa lengo la kutoa ufafanuzi kuhusu mchakato mzima wa wizara yake kupeleka fedha hizo katika mfuko wa pembejeo, alionekana kukasirika na kusema hajui lolote kuhusu hatua ya wizara yake kuelekeza fedha za EPA kwa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika.

``Mimi sina habari na hizo fedha, labda yeye mwenyewe (Wasira) akwambie ni kiasi gani, sina comment (maoni) kwa hilo. Kama anasema alizipata hizo fedha, yeye mwenyewe awatajie kiasi gani, mimi sijui kabisa,`` alisema Mkulo.

Aliongeza: ``Mpigie simu Wasira ama Katibu Mkuu wake, waambie Waziri wa Fedha kasema yeye halijui hilo suala...huyo bwana (Wasira) akutajie mwenyewe ni kiasi gani.``

Kauli hizo, zilidhihirisha kuwepo utata kuhusu uwepo na matumizi ya fedha hizo, hofu iliyowahi kutolewa pia na baadhi ya wananchi, wakiwemo wanaharakati na viongozi wa vyama vya upinzani.


Wamekuwa wakisema kuwa mchakato wa urejeshaji wa fedha hizo haukuwa na uwazi kwa kuwa serikali haijawahi kueleza ni akaunti gani fedha za EPA ziliingizwa.

Wasira aliwaambia wandishi wa habari kuwa fedha zilizoibwa kutoka EPA na kurejeshwa serikalini zimeanza kutumika katika mpango wa utoaji ruzuku ya mbolea kwa mtindo wa vocha, ambapo jumla ya wakulima 700,000 watanufaika.

``Kwa kweli pamoja na fedha zilizotengwa kwa kipindi cha mwaka wa bajeti, fedha zilizotoka EPA zilituongezea nguvu kubwa sana katika kufanikisha mpango huu,`` alisema Wasira.

Hata hivyo, Ofisa mmoja wa TIB aliwahi kukaririwa na baadhi ya vyombo vya habari hivi karibuni, akisema kuwa benki hiyo bado haijapokea fedha zilizochotwa kutoka EPA.

Aidha, Wasira alisema mfumo wa kutumia vocha ulibuniwa na serikali, kama njia ya kuepusha ukiritimba na ufujaji wa fedha zilizotolewa kupitia fidia ya mbolea.

Kwa mujibu wa Wasira, wakulima waliopo katika mpango huo, wanapata mifuko minne ya mbolea aina ya minjingu na kilo 10 za mbegu bora za mahindi na mpunga.

Alisema gharama ya jumla ya pembejeo hizo, inakadiriwa kuwa zaidi ya Sh 100,000.

Wasira, alisema mpango wa ruzuku ya vocha, utaendeshwa katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Rukwa, Ruvuma, Morogoro, Kigoma, Kilimanjaro, Arusha, Manyara na wilaya za Tarime mkoani Mara na Sikonge mkoani Tabora.

Alisema, awali ilibainika kuwa fidia iliyolipwa na serikali kwa kampuni za usambazaji mbolea ya ruzuku, haikuwanufaisha wakulima, badala yake iliishia mikononi mwa wafanyabiashara hao.

Kutokana na hali hiyo, Wasira, alisema serikali ililazimika kujifunza mbinu ya kutumia vocha, iliyosaidia kuinua kilimo cha mazao ya chakula katika nchi jirani ya Malawi.

Alisema mpango huo wa vocha utawawezesha wakulima katika maeneo ya vijijini, kununua mbolea kutoka kwa wafanyabiashara wadogo, watakainunua kwa waagizaji wa jumla.

Aliwaonya wahusika katika mpango kujiepusha na vitendo vinavyoweza kukwamisha utekelezaji wake.

SOURCE: Nipashe
 
Back
Top Bottom