MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Mhe Rais wangu, ninakusalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Kazi iendelee!
Najua Mhe Rais pengine utasema huu ni ushauri wa mitandaoni na huwezi kufanyia kazi maoni ya mitandaoni,lakini haya ndio majukwaa huru kwa 100% yanaweza kukupa ushauri mzuri kuliko wale wanaokutazazma ana kwa ana wengine waoga hawakuambii ukweli. Sasa huu ndio ukweli! Nakuomba mhe Rais pokea maoni yangu kwa mikono yote ni muhimu sana. Hii ni njia yangu sahihi maana siwezi kuja IKULU kukushauri.
Nirudi kwenye hoja,Mama tunajua ulishauriwa wakati unafanya mabadiliko ya baraza la mawaziri kuhusu uteuzi wa Ndg Dkt Mwigulu Nchemba lakini Watanzania walio wengi walikushauri kua huyu usimamizi wa Wizara hii kwake ni mgumu kutokana na kutokua makini na pia anaendekeza sana siasa, huyu ni typical politician hawezi kua msimamizi wa wizara ya fedha. Mwigulu ni tofauti na Dkt Mpango, Mpango hakuwa mwanasiasa ni mtendaji,aliteuliwa kutoka kwenye kazi za kiutendaji.
Haiwezekani kati ya miezi ambayo yeye yupo ofisini pesa zinaliwa kiasi kile asijue mpaka waziri mkuu akabaini.Waziri anafanya nini? Kuna wanaomtetea kua eti hakua waziri, yaani pesa zinapigwa mpaka mwezi huu wa May Mwigulu akiwabofisini wizarani halafu kuna watu wanatetea eti hakuwa waziri. Huu ni udhaifu mkubwa sana wa waziri na ni lazima tuwe na uchungu na taifa hili badala ya kutazama usoni.
Hivyo basi, Mhe Rais tunakuomba shughulika na hili mapema kabla halijakuletea shida, wapo watanzania wachache wenye umakini na kazi zao, siyo lazima watoke kwa wabunge waliopo, unaweza kuteua mbunge toka nafasi 2 za Rais zilizosalia. Hii wizara ni roho ya taifa, ikikwama na taifa litakwama.
Mwisho, Mhe Rais nakutakia majukumu mema sisi tupo pamoja nawe na tutaendelea kukuunga mkono na kukutia moyo kiongozi wetu.
Najua Mhe Rais pengine utasema huu ni ushauri wa mitandaoni na huwezi kufanyia kazi maoni ya mitandaoni,lakini haya ndio majukwaa huru kwa 100% yanaweza kukupa ushauri mzuri kuliko wale wanaokutazazma ana kwa ana wengine waoga hawakuambii ukweli. Sasa huu ndio ukweli! Nakuomba mhe Rais pokea maoni yangu kwa mikono yote ni muhimu sana. Hii ni njia yangu sahihi maana siwezi kuja IKULU kukushauri.
Nirudi kwenye hoja,Mama tunajua ulishauriwa wakati unafanya mabadiliko ya baraza la mawaziri kuhusu uteuzi wa Ndg Dkt Mwigulu Nchemba lakini Watanzania walio wengi walikushauri kua huyu usimamizi wa Wizara hii kwake ni mgumu kutokana na kutokua makini na pia anaendekeza sana siasa, huyu ni typical politician hawezi kua msimamizi wa wizara ya fedha. Mwigulu ni tofauti na Dkt Mpango, Mpango hakuwa mwanasiasa ni mtendaji,aliteuliwa kutoka kwenye kazi za kiutendaji.
Haiwezekani kati ya miezi ambayo yeye yupo ofisini pesa zinaliwa kiasi kile asijue mpaka waziri mkuu akabaini.Waziri anafanya nini? Kuna wanaomtetea kua eti hakua waziri, yaani pesa zinapigwa mpaka mwezi huu wa May Mwigulu akiwabofisini wizarani halafu kuna watu wanatetea eti hakuwa waziri. Huu ni udhaifu mkubwa sana wa waziri na ni lazima tuwe na uchungu na taifa hili badala ya kutazama usoni.
Hivyo basi, Mhe Rais tunakuomba shughulika na hili mapema kabla halijakuletea shida, wapo watanzania wachache wenye umakini na kazi zao, siyo lazima watoke kwa wabunge waliopo, unaweza kuteua mbunge toka nafasi 2 za Rais zilizosalia. Hii wizara ni roho ya taifa, ikikwama na taifa litakwama.
Mwisho, Mhe Rais nakutakia majukumu mema sisi tupo pamoja nawe na tutaendelea kukuunga mkono na kukutia moyo kiongozi wetu.