Bila ya kushughulikia njama za Makinda wabunge wa CDM hawafiki kokote.

Byendangwero

JF-Expert Member
Oct 24, 2010
871
56
Tangu kuanza kwa bunge linaloendelea makinda amejitokeza wazi kwamba amepania kweli kweli kukwamisha wabunge wa CDM katika kutekeleza wajibu wao wa kuisimamia na kuikosoa serikali inapobidi. Katika njama zake hizo, Makinda anaonekana kusaidiwa na wabunge wa CCM na hata baadhi ya wabunge wa vyama vya upinzani ambao spika huyo huwapa upendeleo maalum wa kuzungumza na kutenda jinsi wapendavyo bila ya kuzingatia kanuni na maadili ya bunge. Kitu kinacho sababisha spika huyo kuonyesha jeuri hiyo, ni imani kwamba CDM haiwezi kumfanya chochote bungeni kwakuwa wabunge wa CCM kutokana na wingi wao watamrinda. Katika hali hiyo napendekeza spika huyo ashughulikiwe kwa nguvu ya umma; katika maandamano yanayotarajiwa kuendeshwa na CDM nchi nzima, njama hizo za Makinda ziwekwe wazi kwa umma, ili kote nchini walaani hizo hujuma zake.
 
kweli kabisa,na pia sehemu kubwa ya watanzania wameamka na wapo macho mno,tatzo lingine linakuja,kipindi hiki Cha bunge umeme haupo hvyo inakua ngumu kwa wanaharakati kuckiliza na kuona bunge,hii jambo la umeme nahc zipo ki-ccm zaidi! Ila mwisho wao upo wajiandae kuachia ngazi!
 
Inferiority complex ndio inakusumbueni, Binafsi namsifu kwa kuwa strong hadi sasa licha ya nia ya cdm kutaka kumpelekesha kwa miongozo ya ajabu ajabu ambayo yote ameipangua ipasavyo na sasa anaonekana anawaonea, pale si mahala pakwenda kuonyesha ufahari kuwa wewe ni mjuvi zaidi bali kanuni na muongozo wa spika ndio sheria.
 
inferiority anayo yeye,kivip adai ushahidi then abadilike apelekewe aliogopa kuumbuka mbele ya macho ya jamii! Acha utumwa wa nafs kjana jaji na chambua mambo kwa kina! Wek up,toka kweny ucngz wa pono!
 
ukiangalia bunge yaani ni dhahiri kwamba soon or later linakuwa halina control. Jana naona spika haeshimiki watu wanamjibu tu mbunge akiongea bila spika kuruhusu, yaani vurugu tu. Kama uliona wakati Regia akiongea kuna watu wana switch on mike wana kejeli na spika hafanyi lolote. Huu ni upuuuzi kweli kweli.
 
Ni kweli na ninaamini hakika PENYE NIA PANA NJIA.
Kama ilivyo NIA YA CDM kupambana hadi kieleweke njia itapatikana lazima, na itakuwa aibu kwao.

Njia mojawapo niliyo ipenda ni pale yajapo mambo ya kisanii mnapo toka na kuwaacha humo wasanii nawapa5.B
Si utani inawauma mpaka kumoyo; Hasa wale ambao dhamira zao hazija ingia kutu.

Ombi kwa CDM;
MSIBADILI MALENGO YENU BALI RUKSA KUBADILI NJIA YA KUFIKIA MALENGO.
 
Leo nilikuwa natoka Kaisho kwenda makao makuu ya wilaya ya karagwe (kayanga); Kaisho ni kata iko mpakani na uganda na ni remote kweli. Katika hiyo hiace mjadala wa spika na namna anavyoliendesha bunge ulitawala. Amini usiamini wananchi wengi hawaridhiki na spika anavyofanya. Wamefikia mahali pa kusema kuwa ccm na viongozi wake ngazi zote wanaonekana hawako karibu na watu kwa maana hawajui watu wanasema nini juu yao. Yaani ile kazi ya chama nje ya chama haifanyiki tena, wamezama kwenye kazi ya chama ndani ya chama, na huko wanajishibisha wenyewe. Kauli hiyo imetolewa na mwanamke mmoja ambaye umri wake ni kama miaka kati ya 40 - 45 hivi.
Wanavyochakachua kanuni wanafikiri wananchi wanaridhika kumbe wanajidanganya.
CDM anzisheni tena ile operesheni ya kutembea nchi nzima; wakati wao wako kwenye hizo kamati zao nyinyi sambaa nchi nzima,na matokeo yataonekana soon.
 
Napendekeza posho na marupurupu yapunguzwe ili kupunguza matumizi ya serikali kama USA . Pengine itasaidia watu wawe objective zaidi kwenye important issues to the nation than cheap political inclinations.
 
Ukweli ni kuwa bunge hili linaweza kuitwa bunge la miongozo! Yaani spika anadharaulika sana, hakuna heshima tena bungeni. Jana kama uliona uchaguzi wa makamshina ilikuwa vurugu na ni imani yangu hata uchakachuaji uliwezekana.Hii itabaki kuwa changamoto kwa siku za usoni kuchagua maspika makini na si bora spika.
Ona issue ya Lema alivyoihandle kibabaishaji mara nakupa siku tano kisha anakumbushwa na watu walikuwa wanasubiri kujua uongo wa Lema au PM lakini sijui nini kimemshitusha anasema apeleke ushahidi ofisini kwake ili akiona unafaa kuutoa kwa maslahi ya CCM autoe lakini kama upo kinyume basi amlinde PM asije akadhalilika. Mwisho namkubali sana Makinda kwa jinsi alivyo shupavu wa kutii amri za wakuu wake!
 
Rejea namna alivyopatikana spika huyu tangu mwanzo anashauriwa au anabembelezwa kugombea uspika utaona kuwa kulikuwa na ajenda maalum.huyu mama namsifu jinsi anavyotetea maslahi ya chama chake laiti Kama viongozi wote wangekuwa na msimamo huo lakini katika ngazi ya maslahi ya taifa tungekuwa tupi level moja na nchi za Malaysia , Singapore etc
 
Natabiri kama PAOLO: kuna wakati atajiuzulu huyu mama. Ni mtu wa hamaki na kutojiamini.
 
Nilishasema huyu mama ana kiherehere chake bungeni inawezekana tayari Fisadi 1 ameshamchukuwa na kumpa mshiko wake kuliangamiza Taifa letu. Maana hana hata aibu huyu mama, ana roho mbaya kama sura yake hata masudi ni mzuri sijui kwanini huyu mama asinge enda kugombania watu wenye sura mbaya:coffee:
 
Unategemea nini baada ya kukiri kuwa RA ndiye aliyefunga safari kutoka Igunga hadi Njombe akamshauri agombee kiti hicho!
 
Spika huyu amepandikizwa kulinda maslah ya mafisadi wakuu kama RA,AC,EL watafunaji mkate wa taifa,huyo spika kama atazidi kuwajibika kiremote control wamekutana na 'vichwa' cdm wataumbuka
 
Makinda anasaidia kuongeza hasira za wapigakura kwa chama chake which is good for the opposition.
 
Back
Top Bottom