Bila viboko, nidhamu ya wanafunzi hakuna

karv

JF-Expert Member
Dec 26, 2019
1,799
3,221
Habari zenu wapendwa

Nidhamu ya mwanafunzi imeshuka kutokana na kufutwa kwa adhabu ya viboko shuleni.

Miaka ya nyuma mwanafunzi alikuwa na nidhamu ya hali ya juu. Mwanafunzi alikuwa anaheshimu mwalimu kama alivyo heshimu wazee wake. Alipokemewa na mwalimu akisikiliza kwa sauti.

Mwalimu alipomuhukumu mwanafunzi shuleni, mwanafunzi huyo alikiri na kukubali kosa lakini kwa sasa hali haipo ivyo.

Kwa sasa mwanafunzi alihukumiwa na mwalimu ataondoka kwa kilio hadi nyumbani na kutoa malalamiko kuwa amepigwa. Na mzazi au mlezi bila ya kuuliza ataenda mbio hadi kwa mwalimu na kuanza kubwata na kutoa lugha chafu na kutaka kupigana na mwalimu na wengine huenda mbali hadi kuwafanyia mambo ya kishirikina.

Uchache wa walimu shuleni na watoto kuzurura hovyo mtaani pia huchangia kupungua kwa nidhamu. Vile vile walimu kufanya biashara shuleni kuliko kufundisha darasani pia huchangia nidhamu kushuka.

Tunaomba serikali kupitia wizara husika itazame suala la utoro kwa wanafunzi na walimu kwa ujumla.

Ukiangalia kwa undani utaona wanafunzi wengi hasa wa sekondari hizi za kata huzurula sana mitaani ukiuliza watakujibu shuleni hakuna walimu.

Vile vile kuna suala la wanafunzi wa kike wa sekondari wanapanga uraiani. Hawa ni wepesi sana kupata mimba ukizingatia wengi hujihusisha na mapenzi na watu wanaoishi nao karibu pindi tu hali zao za kifedha zinapokuwa chini.

Na kwa kumalizia napongeza uwepo wa shule za sekondari za kata lakini shule hizo bila walimu ni kama nyumba bila mlango wala madirisha

Ahsante naomba kuwasilisha
 
Habari zenu wapendwa

Nidhamu ya mwanafunzi imeshuka kutokana na kufutwa kwa adhabu ya viboko shuleni.

Miaka ya nyuma mwanafunzi alikuwa na nidhamu ya hali ya juu. Mwanafunzi alikuwa anaheshimu mwalimu kama alivyo heshimu wazee wake. Alipokemewa na mwalimu akisikiliza kwa sauti.

Mwalimu alipomuhukumu mwanafunzi shuleni, mwanafunzi huyo alikiri na kukubali kosa lakini kwa sasa hali haipo ivyo.

Kwa sasa mwanafunzi alihukumiwa na mwalimu ataondoka kwa kilio hadi nyumbani na kutoa malalamiko kuwa amepigwa. Na mzazi au mlezi bila ya kuuliza ataenda mbio hadi kwa mwalimu na kuanza kubwata na kutoa lugha chafu na kutaka kupigana na mwalimu na wengine huenda mbali hadi kuwafanyia mambo ya kishirikina.

Uchache wa walimu shuleni na watoto kuzurura hovyo mtaani pia huchangia kupungua kwa nidhamu. Vile vile walimu kufanya biashara shuleni kuliko kufundisha darasani pia huchangia nidhamu kushuka.

Tunaomba serikali kupitia wizara husika itazame suala la utoro kwa wanafunzi na walimu kwa ujumla.

Ukiangalia kwa undani utaona wanafunzi wengi hasa wa sekondari hizi za kata huzurula sana mitaani ukiuliza watakujibu shuleni hakuna walimu.

Vile vile kuna suala la wanafunzi wa kike wa sekondari wanapanga uraiani. Hawa ni wepesi sana kupata mimba ukizingatia wengi hujihusisha na mapenzi na watu wanaoishi nao karibu pindi tu hali zao za kifedha zinapokuwa chini.

Na kwa kumalizia napongeza uwepo wa shule za sekondari za kata lakini shule hizo bila walimu ni kama nyumba bila mlango wala madirisha

Ahsante naomba kuwasilisha
Wapi huko viboko vimefutwa? Huku kwetu viboko kama Kawa ila kwa kuzingatia umri,jinsia na afya ya mtoto. Mzazi/mlezi anayekuja shuleni kwa Shari mchukulieni hatua za kisheria kwa kuleta vurugu ndani ya taasisi na kusanabishwa huduma mbalimbali ikiwemo kufundishwa kwa watoto kukosekana halafu ataona mziki wake.
Walimu hasa wa kike kufanya biashara na wateja wake ni wanafunzi kweli kunashusha nidhamu kwa watoto na utendaji mbaya kwake mwalimu kwa upande wa walimu wa kiume hasa wa sekondari kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi Nako kunachangia kushuka kwa nidhamu kwa watoto.
 
Nani kakwambia viboko hamna, lazima wapigike kama Kawa. Mwanafunzi haendi bila mwalimu kuwa mkali.
 
Ndio maana leo viongozi wanatukanwa na watoto wao wanalalamika hawakumbuki wao ndio sehemu ya hilo
 
Nani kakwambia viboko hamna, lazima wapigike kama Kawa. Mwanafunzi haendi bila mwalimu kuwa mkali.
Viboko havisaidii. Hii ni kutokana na utafiti na siyo bla bla bla za mitaani. Ukitaka kujua tofauti ya kufundisha kwa viboko na kufundisha kwa maelezo angalia tofauti eg ya viongozi wa nchi za kiafrika na viongozi wa nchi zilizoendelea.
 
Viboko havisaidii. Hii ni kutokana na utafiti na siyo bla bla bla za mitaani. Ukitaka kujua tofauti ya kufundisha kwa viboko na kufundisha kwa maelezo angalia tofauti eg ya viongozi wa nchi za kiafrika na viongozi wa nchi zilizoendelea.
Sio Kila muda upige, hapana. Ila kwa namna yake vinasaidia
 
Habari zenu wapendwa

Nidhamu ya mwanafunzi imeshuka kutokana na kufutwa kwa adhabu ya viboko shuleni.

Miaka ya nyuma mwanafunzi alikuwa na nidhamu ya hali ya juu. Mwanafunzi alikuwa anaheshimu mwalimu kama alivyo heshimu wazee wake. Alipokemewa na mwalimu akisikiliza kwa sauti.

Mwalimu alipomuhukumu mwanafunzi shuleni, mwanafunzi huyo alikiri na kukubali kosa lakini kwa sasa hali haipo ivyo.

Kwa sasa mwanafunzi alihukumiwa na mwalimu ataondoka kwa kilio hadi nyumbani na kutoa malalamiko kuwa amepigwa. Na mzazi au mlezi bila ya kuuliza ataenda mbio hadi kwa mwalimu na kuanza kubwata na kutoa lugha chafu na kutaka kupigana na mwalimu na wengine huenda mbali hadi kuwafanyia mambo ya kishirikina.

Uchache wa walimu shuleni na watoto kuzurura hovyo mtaani pia huchangia kupungua kwa nidhamu. Vile vile walimu kufanya biashara shuleni kuliko kufundisha darasani pia huchangia nidhamu kushuka.

Tunaomba serikali kupitia wizara husika itazame suala la utoro kwa wanafunzi na walimu kwa ujumla.

Ukiangalia kwa undani utaona wanafunzi wengi hasa wa sekondari hizi za kata huzurula sana mitaani ukiuliza watakujibu shuleni hakuna walimu.

Vile vile kuna suala la wanafunzi wa kike wa sekondari wanapanga uraiani. Hawa ni wepesi sana kupata mimba ukizingatia wengi hujihusisha na mapenzi na watu wanaoishi nao karibu pindi tu hali zao za kifedha zinapokuwa chini.

Na kwa kumalizia napongeza uwepo wa shule za sekondari za kata lakini shule hizo bila walimu ni kama nyumba bila mlango wala madirisha

Ahsante naomba kuwasilisha
Huku nilipo walimu wanarogwa sana
 
Back
Top Bottom