Bila Upelelezi kukamilika hakuna kukamata, ukiachiwa na Mahakama hakuna kukamatwa tena

Mwananchi Huru

JF-Expert Member
Nov 20, 2021
1,448
1,003
photo_2022-01-18_01-30-19.jpg
Tunaposema kila Mtanzania amuunge mkono Rais wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hassan tunamaanisha mambo kama haya, Niwe mkweli tu tangu Uhuru Mama huyu ni watofauti sana hebu ona alichofanya kwenye magazeti na hii,
===
Bunge limepitisha Mabadiliko muhimu ya Sheria kupitia muswada wa mabadiliko ya Sheria mbalimbali Na. 7 wa mwaka 2021 ambapo kifungu cha 131 cha Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai kimefanyiwa mabadiliko.

Kifungu hiki kipya cha 131A kinamkataza Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP), Polisi, au yeyote mwenye mamlaka ya kushitaki, kutokupeleka kesi mahakamani pasipo upelelezi kukamilika. Hii ilipelekea mtu kukaa na kesi kwa miaka mingi huku kila siku akiambiwa na waendesha mashitaka kuwa upelelezi haujakamilika.

Pia kwenye mabadiliko haya, ikiwa utashitakiwa na mahakama kukuachia huru, basi polisi hana mamlaka ya kukukamata tena na kukufungulia kesi upya. Kitendo hiki kilikuwa kinawafanya watu watoke mbio sana mahakamani mara baada tu ya kuachiwa huru.

Kwa msingi huu Mwendesha mashtaka wa serikali, Polisi, na wengine wote wenye mamlaka ya kushitaki, ikiwa hajakamilisha upelelezi hana haki ya kufungua kesi mahakamani hadi pale atakapokamilisha upepelezi na pia hawezi kukukamata ikiwa umepatikana huna hatia na mahakama.

Unaweza ukaniuliza ikiwa wamekatazwa kupeleka kesi mahakamani kabla upelelezi haujakamilika, ina maana sasa watuhumiwa watasota sana selo mpaka polisi wakamilishe upepelezi wa makosa yao?

Jibu ni hapana, mabadiliko hayo hayo kifungu cha 131A (2) kinasema kuwa ikiwa upelelezi haujakamilika na hivyo kutomwezesha mtu kupelekwa mahakamani basi anatakiwa aachiwe kwa kupewa dhamana wakati polisi ama mamlaka nyingine ikiendelea kukamilisha upelelezi wa makosa yake. Hautakiwi kuwekwa selo au kukaa polisi ikiwa upepelezi wa kosa lako haujakamilika.

Hata hivyo, katazo hili la kutopeleka kesi mahakamani bila upelelezi kukamilika linahusu makosa yote isipokuwa makosa ya kubaka (rape), wizi wa kutumia silaha (armed robnery), kumiliki silaha kinyume cha sheria, kumiliki nyara za serikali kinyume cha sheria, makosa ya kujeruhi sana (grievious harm), kosa la kuhatarisha usalama wa taifa, usafirishaji dawa za kulevya, na jinai nyingine ambazo hadhi yake husikilizwa tu na mahakama kuu. Kama kesi yako imefunguliwa mahakama kuu basi kosa hilo haliguswi na mabadiliko haya, utaratibu wa kawaida wa mashauri ya jinai utafuatwa.

Kifungu cha 131A(3) cha mabadiliko haya kinatoa msisitizo kwenye kifungu cha 170(6) cha Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai kwamba kama makosa ambayo adhabu zake kama mtu angekuwa anahukumiwa na mahakama angehukumiwa kulipa faini ya Tshs 200,000/= basi mtu huyo anatakiwa akiri kosa kwa maandishi, kisha alipe faini hiyo kwenye akaunti za serikali, na aachiwe huru.
 
Mtu akifanya unaloona zuri apongezwe na akikosea akosolewe, tatizo letu wabongo hatupo hivyo yani sisi tuna option mbili tu tukuchukie mazima(tukufanye shetani) au kukupenda mazima(tukufanye malaika).
 
Safii iyo ni nzuri. Polisi wafanye upelelezi mtu ukiwa unaendelea na majukumu yako. Ukikamilika ndio ufike rumande kama kosa halina mdhamana.

Lakini bado sioni kama kutakua na utekelezaji maana makosa yaliyo wekwa hapo ndio huwa yanawekesha watu rumande / celo,wakisubiri upepelezi.

Bado kupunguza VAT
 
Safii iyo ni nzuri. Polisi wafanye upelelezi mtu ukiwa unaendelea na majukumu yako. Ukikamilika ndio ufike rumande kama kosa halina mdhamana.

Lakini bado sioni kama kutakua na utekelezaji maana makosa yaliyo wekwa hapo ndio huwa yanawekesha watu rumande / celo,wakisubiri upepelezi.

Bado kupunguza VAT
Bado sn lakini itaisaidia kidogo
 
Wanaompinga Mama ni vichaa na watu wabaya tu,

Wasiopenda kuona WATANZANIA wakiwa wamoja wakati wote,

Wasiopenda watu waishi kwa raha mstalehe kwenye nchi yao,

Tunayo nafasi ya kujenga Taifa bora sana tukiwa na Mama Samia,
Kiukweli Samia ni kiongozi bora sanaa kuwai kutokea jamani!
 
Kwahyo kama kosa lako adhabu yake ni 200,000 faini unakiri kwa maandishi unalipa faini then unaachiwa huru....

BUT Adhabu zenye faini huwa zina kifungo pia (Yaani either miaka fulani au faini ya 200,000),, Je sheria inazungumziaje kuhusu kifungo cha muda gani unaweza kukiri kwa maandishi...!?

Wajuzi niwekeni sawa hapa kama mmenielewa...
 
Back
Top Bottom