Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,087
- 6,568
Ukienda South Africa hii leo ukakutana na ndugu wa Steven Biko na ukafanya nao mazungumzo lazima watakuambia kweli kuwa kuna kovu kubwa ndani ya mioyo yao.
Maana ndugu yao aliuawa bila hatia na utawala dhalimu wa makaburu. Tena aliuawa kifo kibaya. Huu ni mfano tu ambao unaonesha namna gani ukiukwaji wa haki za binadamu unaweza kuzalisha chuki ya kudumu.
Kwa hapa Tanzania kuna chuki kubwa sana ndani ya mioyo ya watanzania hasa baada ya Tundu Lissu kumiminiwa risasi zaidi ya 33 kama vile yeye sio binadamu.
Maana ni tukio ambalo kila mtu haamini kuwa anaweza kufanyiwa binadamu aliyekuwa anahoji masuala ya msingi juu ya taifa lake.
My take: Taifa linalotenda haki humuinua Mungu.
Maana ndugu yao aliuawa bila hatia na utawala dhalimu wa makaburu. Tena aliuawa kifo kibaya. Huu ni mfano tu ambao unaonesha namna gani ukiukwaji wa haki za binadamu unaweza kuzalisha chuki ya kudumu.
Kwa hapa Tanzania kuna chuki kubwa sana ndani ya mioyo ya watanzania hasa baada ya Tundu Lissu kumiminiwa risasi zaidi ya 33 kama vile yeye sio binadamu.
Maana ni tukio ambalo kila mtu haamini kuwa anaweza kufanyiwa binadamu aliyekuwa anahoji masuala ya msingi juu ya taifa lake.
My take: Taifa linalotenda haki humuinua Mungu.