jingalao
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 35,052
- 28,242
Bila shaka yoyote na kwa kujikumbusha matukio kadhaa ni wazi kuwa ajenda ya madiwani kutaka kuongezewa posho ilikuwa ni ajenda iliyopenyezwa na madiwani wa Chadema.
Ajenda hii ilikuwa ni ajenda mbaya ya kuwaabisha madiwani ambao wanatakiwa kuwa karibu na wananchi na kuibua shida za wananchi au kutoa mapendekezo kwa serikali kuu jinsi ya kuboresha maisha ya wananchi wa hali ya chini na sio kutaka kunenepesha matumbo yao.
Tunakumbuka mkuu wa mkoa wa Arusha na mkurugenzi wa jiji la Arusha alivyotukanwa na madiwani wa chadema wakiongozwa na Lema kisa kukata kiwango cha posho cha madiwani.
Tunakumbuka pia madiwani wa Meru walivyosusia vikao katika halmashauri hiyo kisa kupunguzwa kwa posho.
Pia wapo madiwani wa manispaa ya Moshi ambao waligomea mafunzo ya uwezeshaji yaliyoandaliwa na Tamisemi kisa posho.
Mifano hii inaashiria kuumizwa sana kwa madiwani wa chadema kutokana na punguzo la posho.Imagine diwani wa Arusha alikuwa analiliia kulipwa posho ya nauli sh 100000 ilihali nauli ya tax haizidi elfu tatu.
Hakuna shaka ushawishi wa madiwani hawa katika mkutano wa ALAT ukipelekea kumtega Magufuli awaingezee posho.
Kwa kuwa Magufuli ni mzalendo na amedhamiria kutuokoa kutoka makucha ya wanasiasa waroho alikataa wazi wazi na bila kumung'unya neno,hasira ya kukataliwa kwa ajenda ilipelekea upotoshaji wa kauli ya Rais na mjadala ukahamishiwa kwenye nyongeza ya mishahara.
Ni vyema tujadili na kujua nini kitafuata baada ya Magufuli kukataa ombi hili la madiwani wa chadema lililowasilishwa kwa mdomo wa AlAT.
JE WATASUSIA VIKAO?
Ajenda hii ilikuwa ni ajenda mbaya ya kuwaabisha madiwani ambao wanatakiwa kuwa karibu na wananchi na kuibua shida za wananchi au kutoa mapendekezo kwa serikali kuu jinsi ya kuboresha maisha ya wananchi wa hali ya chini na sio kutaka kunenepesha matumbo yao.
Tunakumbuka mkuu wa mkoa wa Arusha na mkurugenzi wa jiji la Arusha alivyotukanwa na madiwani wa chadema wakiongozwa na Lema kisa kukata kiwango cha posho cha madiwani.
Tunakumbuka pia madiwani wa Meru walivyosusia vikao katika halmashauri hiyo kisa kupunguzwa kwa posho.
Pia wapo madiwani wa manispaa ya Moshi ambao waligomea mafunzo ya uwezeshaji yaliyoandaliwa na Tamisemi kisa posho.
Mifano hii inaashiria kuumizwa sana kwa madiwani wa chadema kutokana na punguzo la posho.Imagine diwani wa Arusha alikuwa analiliia kulipwa posho ya nauli sh 100000 ilihali nauli ya tax haizidi elfu tatu.
Hakuna shaka ushawishi wa madiwani hawa katika mkutano wa ALAT ukipelekea kumtega Magufuli awaingezee posho.
Kwa kuwa Magufuli ni mzalendo na amedhamiria kutuokoa kutoka makucha ya wanasiasa waroho alikataa wazi wazi na bila kumung'unya neno,hasira ya kukataliwa kwa ajenda ilipelekea upotoshaji wa kauli ya Rais na mjadala ukahamishiwa kwenye nyongeza ya mishahara.
Ni vyema tujadili na kujua nini kitafuata baada ya Magufuli kukataa ombi hili la madiwani wa chadema lililowasilishwa kwa mdomo wa AlAT.
JE WATASUSIA VIKAO?