Kama kichwa cha habari kinavyojieleza ni kwamba kupata cheti cha kuzaliwa au kifo kutoka ofisi ya kutoa vyeti hivyo (RITA) Mkoani Arusha ni shughuli kubwa sana.
Ukifika mara ya kwanza unakuta foleni ndefu ya ajabu. Ukifanikiwa kuwakuta watendaji unapewa namba ya kulipia (Kontro namba)
ukisha lipia ndio utaambiwa njoo baada ya wiki tatu. Ukirudi baada ya wiki tatu unakuta mazingira ya mlundikano wa watu ni vilevile,
inakuchukua siku nzma nyingine kufanikiwa kuwakuta wahusika.
Ukiwakuta wahusika wanakuambia cheti husika hakionekani ndio imetoka hivyo, hapo ni wewe ujiongeze kama unaharaka uwaone kwa njia inayoitwa kujiongeza.
Imekuwa ni jambo la kawaida kabisa pale ofisi za RITA Arusha kuambiwa njoo baada ya wiki moja, nk kumbe kinachotakiwa ni RUSHWA
Cha ajabu ofisi hizi za RITA zipo jengo moja na ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arusha lakini mambo ya ajabu na kutesa wananchi yanafanyika
Ni lini wananchi watapata huduma ya bila kutakiwa kutoa RUSHWA kwa watu walioajiriwa na kulipwa kwa KODI zetu?
Ukifika mara ya kwanza unakuta foleni ndefu ya ajabu. Ukifanikiwa kuwakuta watendaji unapewa namba ya kulipia (Kontro namba)
ukisha lipia ndio utaambiwa njoo baada ya wiki tatu. Ukirudi baada ya wiki tatu unakuta mazingira ya mlundikano wa watu ni vilevile,
inakuchukua siku nzma nyingine kufanikiwa kuwakuta wahusika.
Ukiwakuta wahusika wanakuambia cheti husika hakionekani ndio imetoka hivyo, hapo ni wewe ujiongeze kama unaharaka uwaone kwa njia inayoitwa kujiongeza.
Imekuwa ni jambo la kawaida kabisa pale ofisi za RITA Arusha kuambiwa njoo baada ya wiki moja, nk kumbe kinachotakiwa ni RUSHWA
Cha ajabu ofisi hizi za RITA zipo jengo moja na ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arusha lakini mambo ya ajabu na kutesa wananchi yanafanyika
Ni lini wananchi watapata huduma ya bila kutakiwa kutoa RUSHWA kwa watu walioajiriwa na kulipwa kwa KODI zetu?