Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Suala la ununuzi wa magari ya ATCL tumeliandika sana hapa tangu mwanzo na kuweka ushahidi wote wa nani alikuwa na gari gani na alilipata vipi na tuliweka mikataba ya ununuzi wa magari yale. Angalau sasa kidogo wamefuatilia jambo hili. Hata hivyo kashfa kubwa zaidi ATCL ilikuwa ni ya ununuzi wa Airbus 320 ununuzi ambao umeliletea taifa hasara kubwa zaidi kuliko huo wa magari. Sasa kama TAKUKURU na vyombo vingine havitaleta mashtaka kwenye hili tutaona ni geresha tu.
Ununuzi wa Airbus ndio uliogubikwa na ukiukwaji mkubwa sana wa kanuni zote za manunuzi ya umma, na kama tulivyoonesha umelisababishia taifa gharama kubwa na ulisaidia sana kulizamisha shirika hilo hata kuondoa uwezekano wote wa kuweza kufufuka na kuwa shirika la kisasa.
Kwa hiyo, bila kuleta mashtaka dhidi ya wahusika wote - wakitaka vielelezo vyote vipo humu humu - itakuwa ni kuwadanganya watu. NI kuchezea hisia za Watanzania kwani makosa waliyoshtakiwa nayo hayalingani kabisa na mambo ambayo waliyasababisha ATCL.
Thats all..
Ununuzi wa Airbus ndio uliogubikwa na ukiukwaji mkubwa sana wa kanuni zote za manunuzi ya umma, na kama tulivyoonesha umelisababishia taifa gharama kubwa na ulisaidia sana kulizamisha shirika hilo hata kuondoa uwezekano wote wa kuweza kufufuka na kuwa shirika la kisasa.
Kwa hiyo, bila kuleta mashtaka dhidi ya wahusika wote - wakitaka vielelezo vyote vipo humu humu - itakuwa ni kuwadanganya watu. NI kuchezea hisia za Watanzania kwani makosa waliyoshtakiwa nayo hayalingani kabisa na mambo ambayo waliyasababisha ATCL.
Thats all..