Bila kuwa na katiba mpya itakayoondoa wabunge vilaza tutegemee migomo zaidi au pengine maandamano kama ya Kenya.

Matongee

JF-Expert Member
Jun 17, 2023
1,046
2,679
Hii sio wiki nzuri kwa nchi zetu za Afrika Mashariki hasa Tanzania na Kenya. Wakati Kenya wanaandamana kihuni kupinga kupitishwa kwa sheria mpya ya fedha huku Tanzania kuna mgomo wa wafanyabiashara. Hawa wafanyabiashara wana hoja kadhaa za msingi ingawa pia wanazo hoja zingine za kipumbavu. Baada ya kutazama kwa kina huu mgomo nimeona tatizo kuu ni BUNGE LA TANZANIA kupitisha sheria za hovyo mno. Kinachoendelea kwa sasa ni kulipishana kodi juu ya kodi. Sina haja ya kuelezea watu wanalipa kodi kiasi gani kwasababu kuna nyuzi nyingi humu zimeelezea. Kimsingi HAZILIPIKI.

Hatutaweza kuwabadili wabunge ghafla bila kubadili kifungu cha katiba kinachoruhusu hata mwendawazimu kuingia bungeni kisa anajua kusoma na kuandika. Ukitazama bunge utaona ni wabunge wachache sana wanaoweza kuchambua muswada uliopelekwa bungeni. Wengi wao wakisimama ni kuomba serikali iwajengee daraja au zahanati jimboni. Hivi kwenye ulimwengu wa kidigitali hata barabara iliyopo maporini si inaonekana tu? Utakuta ni muda wa kujadili muswada wa sheria ya elimu mbunge anasimama kuomba serikali ijenge barabara ya kijijini kwake.

Ninashauri sana serikali pia ishtuke kuwa hata hawa polisi tulio nao ni polisi wa kizazi kipya ambao hawajui mambo ya "Zidumu fikra za mwenyekiti".. hawa wa sasa nao wanataka maisha mazuri na sio kuishi kwa dhiki makambini. Ipo siku nao watasapoti wananchi. Mwaka 2008 kuna jamaa alipost yuko na watoto wake wenye umri kama miaka 4 hadi 8 wakiwa wamevaa gwanda za CHADEMA. Wale watoto kwa sasa ni watu wazima kwahiyo kama walikuzwa na baba mpinzani tayari hapo ni shida.
 
Hii sio wiki nzuri kwa nchi zetu za Afrika Mashariki hasa Tanzania na Kenya. Wakati Kenya wanaandamana kihuni kupinga kupitishwa kwa sheria mpya ya fedha huku Tanzania kuna mgomo wa wafanyabiashara. Hawa wafanyabiashara wana hoja kadhaa za msingi ingawa pia wanazo hoja zingine za kipumbavu. Baada ya kutazama kwa kina huu mgomo nimeona tatizo kuu ni BUNGE LA TANZANIA kupitisha sheria za hovyo mno. Kinachoendelea kwa sasa ni kulipishana kodi juu ya kodi. Sina haja ya kuelezea watu wanalipa kodi kiasi gani kwasababu kuna nyuzi nyingi humu zimeelezea. Kimsingi HAZILIPIKI.

Hatutaweza kuwabadili wabunge ghafla bila kubadili kifungu cha katiba kinachoruhusu hata mwendawazimu kuingia bungeni kisa anajua kusoma na kuandika. Ukitazama bunge utaona ni wabunge wachache sana wanaoweza kuchambua muswada uliopelekwa bungeni. Wengi wao wakisimama ni kuomba serikali iwajengee daraja au zahanati jimboni. Hivi kwenye ulimwengu wa kidigitali hata barabara iliyopo maporini si inaonekana tu? Utakuta ni muda wa kujadili muswada wa sheria ya elimu mbunge anasimama kuomba serikali ijenge barabara ya kijijini kwake.

Ninashauri sana serikali pia ishtuke kuwa hata hawa polisi tulio nao ni polisi wa kizazi kipya ambao hawajui mambo ya "Zidumu fikra za mwenyekiti".. hawa wa sasa nao wanataka maisha mazuri na sio kuishi kwa dhiki makambini. Ipo siku nao watasapoti wananchi. Mwaka 2008 kuna jamaa alipost yuko na watoto wake wenye umri kama miaka 4 hadi 8 wakiwa wamevaa gwanda za CHADEMA. Wale watoto kwa sasa ni watu wazima kwahiyo kama walikuzwa na baba mpinzani tayari hapo ni shida.
Tatizo siyo usomi tatizo ni tabia ya unyumbu, unyumbu ni tabia ya waliopewa dhamana kuahirisha kufikiri kwa nafsi kwasababu ya kujipendekeza ama uoga kwa viongozi wao na kutumikia kundi fulani kwa masilahi binafsi
 
Tambua sio kila changamoto ya nchi itahitaji Katiba ibadirishwe, unapoongelea kubadirishwa kwa katiba unaongelea mapungufu makubwa ya kisheria na kanuni za nchi.

Kwenye hili ulilisema wala haihitaji hayo yote ni swala la upuuzi ambalo mtu yeyote analiona halijakaa sawa.
Yapo mambo ambayo tunaona kweli hapa katiba inahitajika ili kuyaweka bayana.
 
Katiba Mpya Ina Msaada gani kuongeza kipato?
Kwanini ccm hamtaki katiba mpya hii ya zamani imetoa msaada gn wa kuongeza kipato zaid ya kunufaisha majizi ccm kuiba mali za umma tu na kujilimbikizia mali
Na kujihakikishia utawala kwa wizi wa kura
We ulisikia wpi watangaza matokeo ya uchaguzi wameteuliwa na mwenyekiti wa ccm taifa huo si usenge huo.
Miaka zaidi ya 60 ya uhuru kwa katiba hii mbovu mmeshindwa hata kuwapa watz maji tu.
Zaidi mmefilisi mashirika ya umma, viwanda mmevimaliza
Kila mwaka CAG mteule wa mwenyekiti wa ccm anasema wizi wizi kila kona hatua hazichukuliwi kisa katiba ya kisengerema hii.
Viongozi wakuu wamejiwekea kinga ya kutoshitakiwa hata nikikuuliza hapo sababu ni nn wao kujipa kinga hiyo kama kweli ni wema na waadilifu huna jibu kummmmma ww.
 
Back
Top Bottom