macho_mdiliko
JF-Expert Member
- Mar 10, 2008
- 21,779
- 39,572
Sasa mbona sipati link ya moja kwa moja ya jinsi huyu jamaa alivyo husika kwenye tukio au kuwa primary source kwenye incidence yenyewe. Kwa mujibu wa maelezo ya huyu jamaa ni kwamba wakati akiwa polisi kuripoti tukio lake aliwasikia polisi wakitarifiana kupitia radiocalls kuhusu tukio la kibanda. Na hii ni kawaida kwa polisi kuripoti matukio ya sehemu mbalimbali kupitia radiocalls katika vatuo vyao au makao makuu. Na kwa jinsi navyo fahamu radiocalls za polisi huwa hazina siri kwani taarifa zake husikika katika kwa polisi mwingine yeyote mwenye radiocall. Sasa je huyu Joseph Ludovick anawezaje kuwa chanzo cha taarifa cha moja kwa moja cha tukio eti kwa kuwasikia tu polisi wakiwasiliana kutokea kwa tukio la kibanda kupiti radiocalls?
Ndugu, ni hivi: Kwenye ule video ya Rwakatare, kuna sehemu Rwakatare anamwambia maneno haya huyo anayezungumza nae: ''Hajui ni nani adui, ni nani.... unanielewa.... yaani unamwacha kwenye nanihii.... anakuja hapa anakutana na Ludovick'' Sasa hii inaonyesha kuwa Rwakatare alikuwa anazungumza na mtu anayeitwa Ludovick.
Wakati huohuo, Kibanda alipoumizwa, kuna bwana anaitwa Ludovick alipost story kwenye blog moja eti ameporwa na akaenda kuripoti polisi. Alipokuwa polisi akasikia ma-polisi wanawasiana kwenye radio call kuwa Kibanda ameshambuliwa. Hii ilikuwa ni usiku na habari za Kibanda zilikuwa hazijasambaa.... HALAFU hata maelezo yake ya kuporwa yanaacha mashaka makubwa. Jaribu kuyasoma wewe utaniambia kama majambazi hutumia style ya namna hiyo kupora mtu.....