Baada ya kusomwa kwa bajet ya serikali kwa mwaka 2021/22, kumekuwa na mijadala lukuki kuhusu vyanzo vya fedha kupitia ulipaji wa kodi. Serikali imekuwa ikiwaogopa wananchi kuwaelimisha Watanzania umuhimu wa kulipa kodi, badala yake inabuni mbinu za kufidia kodi matokeo yake makosa.
Uoga wa serikali kuwatoza kodi watanzania directly ni kujikomba na kuweka mtaji wa kisiasa kwa kuogopa kuchukiwa na Wananchi.Hii tabia ya watanzania kutokujua umuhimu wa kulipa kodi na kutolipa kodi moja kwa moja tunachelewa kimaendeleo.
Serikali ina uhakika wa kodi kwa watumishi wa umma tu ambao hawana ujanja, ila haipati kodi kutoka kwa Wananchi na wafanya biashara. Mfano ukienda Kariakoo wafanyabiashara wenye maduka makubwa hawalipi kodi badala yake wanatoa bidhaa nje huku wakitumia vijana kuwauzia.
Watanzania kutokulipa kodi ni tatizo linalotengenezwa na serikali yenyewe, hizo njia nyingine ni usumbufu tu, mwishowe Watanzania wanashindwa kujua umuhimu wa kulipa kodi.
Uoga wa serikali kuwatoza kodi watanzania directly ni kujikomba na kuweka mtaji wa kisiasa kwa kuogopa kuchukiwa na Wananchi.Hii tabia ya watanzania kutokujua umuhimu wa kulipa kodi na kutolipa kodi moja kwa moja tunachelewa kimaendeleo.
Serikali ina uhakika wa kodi kwa watumishi wa umma tu ambao hawana ujanja, ila haipati kodi kutoka kwa Wananchi na wafanya biashara. Mfano ukienda Kariakoo wafanyabiashara wenye maduka makubwa hawalipi kodi badala yake wanatoa bidhaa nje huku wakitumia vijana kuwauzia.
Watanzania kutokulipa kodi ni tatizo linalotengenezwa na serikali yenyewe, hizo njia nyingine ni usumbufu tu, mwishowe Watanzania wanashindwa kujua umuhimu wa kulipa kodi.