Bila kujiongeza maisha haya huwezi kumove on katika maisha kama kijana

Mboka man

JF-Expert Member
Aug 22, 2020
477
1,637
Moja Kati ya vitu nilivyovigundua katika maisha haya ni kwamba

1.ukisubili upate kazi ndiyo uweze kuanza maisha utachelewa sana .

2.ukisubili upewe mtaji na wazazi au ndugu zako wa karibu ufanye biashara utachelewa sana

3.ukisubili marafiki zako wa karibu wakusaidie kupata kazi au kukupa fursa utachelewa sana .

4.ukisubili wazazi au ndugu waliofanikiwa ndio waamue hatma ya maisha yako utachelewa sana

Katika haya maisha nilichogundua bila kujiongeza kijana mwenzangu hakuna mtu atayetokea kuja kukusaidia kutatua changamoto zako zinazokukabili bila wewe kujiongeza ninaposema kujiongeza hapa nina angalia maeneo Makuu matatu eneo la kwanza kujitegemea
eneo la pili plan ipi utatumia kuendesha maisha yako ya kila siku
eneo la tatu kutengeneza familia yako ya

Nikianza na eneo la kwanza kujitegemea kijana unapoanza kufikiria kujitegemea ndipo akiri inapoanza kukuaa ufahamu wapi pakuanzia

Eneo la pili ni plan ipi utatumia kuendesha maisha yako ya kila siku hapa nina maana kama kijana unatakiwa utafute plan ya kuendesha maisha yako kama unaona issue za kazi hazija kaa poa basi karibu biashara au kazi nyingine

Eneo la tatu ni mahusiano familia yako ya badae hapa ninazungumza especially vijana wa kiume kama upo nyumbani ni ngumu kupata mwanamke ambae atakuwa tayali kufanya maisha na wewe kama upo nyumbani bado

Kama una lolote la kuongezea ruksaa
 
Mbona points zako zinakinzana na za juu mkuu au sijaelewa... Utajitegenea vipi huku huna kazi? Au utafanya vipi biashara bila mtaji?

Umesema usitegemee ndugu wala marafiki ni vema ukatujulisha ni vipi utapata mtaji au hyo kazi

Sent from my TA-1004 using JamiiForums mobile app

Well swali zuli sana hiloo naomba nikueleze kitu

1.ikoo hivi kama huna ajira ni jinsi Gani unaweza kujitegemea na utafanya biashara kwa mtaji upi

Sasa hapo inabidi uwe na akiri ya kujiongeza ni mbinu Gani unaweza kuitumia kutafuta hela ndogo ndogo at least kila siku una save elfu 500 ndani ya miezi Sita una ndani ya mwaka una laki moja na elfu 75 hapo una hela ya chumba elfu 2 na hela ya kuanzisha biashara ya mtaji wa elfu 50
 
Moja Kati ya vitu nilivyovigundua katika maisha haya ni kwamba

1.ukisubili upate kazi ndiyo uweze kuanza maisha utachelewa sana .

2.ukisubili upewe mtaji na wazazi au ndugu zako wa karibu ufanye biashara utachelewa sana

3.ukisubili marafiki zako wa karibu wakusaidie kupata kazi au kukupa fursa utachelewa sana .

4.ukisubili wazazi au ndugu waliofanikiwa ndio waamue hatma ya maisha yako utachelewa sana

Katika haya maisha nilichogundua bila kujiongeza kijana mwenzangu hakuna mtu atayetokea kuja kukusaidia kutatua changamoto zako zinazokukabili bila wewe kujiongeza ninaposema kujiongeza hapa nina angalia maeneo Makuu matatu eneo la kwanza kujitegemea
eneo la pili plan ipi utatumia kuendesha maisha yako ya kila siku
eneo la tatu kutengeneza familia yako ya

Nikianza na eneo la kwanza kujitegemea kijana unapoanza kufikiria kujitegemea ndipo akiri inapoanza kukuaa ufahamu wapi pakuanzia

Eneo la pili ni plan ipi utatumia kuendesha maisha yako ya kila siku hapa nina maana kama kijana unatakiwa utafute plan ya kuendesha maisha yako kama unaona issue za kazi hazija kaa poa basi karibu biashara au kazi nyingine

Eneo la tatu ni mahusiano familia yako ya badae hapa ninazungumza especially vijana wa kiume kama upo nyumbani ni ngumu kupata mwanamke ambae atakuwa tayali kufanya maisha na wewe kama upo nyumbani bado

Kama una lolote la kuongezea ruksaa
Umeongea vema sana mkuu aliye na masikio amesikia big up komred
 
Mbona points zako zinakinzana na za juu mkuu au sijaelewa... Utajitegenea vipi huku huna kazi? Au utafanya vipi biashara bila mtaji?

Umesema usitegemee ndugu wala marafiki ni vema ukatujulisha ni vipi utapata mtaji au hyo kazi

Sent from my TA-1004 using JamiiForums mobile app
The future is not something we enter into, it's something we create. There is no tablet which will give you prosperity and there is no medicine will take you to a better future, the future is something that you create by yourself.
 
Sijawahi kuwa na hata milioni ya mkupuo kwenye akaunti, lakini nilipoamua tu nianze kujenga nyumba... mwaka wa tatu huu nyumba naelekea kuhamia.

Ningesema niendelee kusubiri nipate pesa, ningeendelea kuota tu usingizini.

Cha ajabu ni kwamba najenga na maisha mengine yanaendelea vile vile, ni nguvu ya maamuzi tu.
 
Sijawahi kuwa na hata milioni ya mkupuo kwenye akaunti, lakini nilipoamua tu nianze kujenga nyumba... mwaka wa tatu huu nyumba naelekea kuhamia.

Ningesema niendelee kusubiri nipate pesa, ningeendelea kuota tu usingizini.

Cha ajabu ni kwamba najenga na maisha mengine yanaendelea vile vile, ni nguvu ya maamuzi tu.
You nile'it mkuu....
 
Safi sana kijana. Umeongea ukweli mtupu. Nakuunga mkono kwa asilimia mia moja. Vijana wengi wanapitia hali ngumu ya maisha Sababu ya kukosa mtaji muhimu sana wa maarifa ya maisha. Vijana wana akili za darasa bila maarifa ya maisha.

Ukitaka kumfelisha kijana kwa haya maisha ya sasa then mnyime elimu ya maarifa ya namna ya kuendesha maisha nje ya mfumo wa ajira rasmi. Serikali imewasusa vijana hadi wamekosa ramani mjini sababu matarajio yao ni kuajiriwa.

Hata hapa utawaona wadio na maarifa watakujia juu na kukuhoji kuwa unaanzaje kwenda kupanga au kuanza maisha bila kuwa hata na kazi ya kukulipa 50,000. Utawaona we soma tu comments.

Nawajua sana hao vijana. Wachache watakuelewa. Sikatai wengi wameanza maisha baada ya kupata viajira vya kujishikiza. Ila as siku zinakwenda hali inazidi kuwa tete na vijana wenye elimu bila ajira inaongezeka. Hili ni tatizo ata an alarming level.

So mkuu congrats sana kwa uzi huu niupa like kubwa sana. Na popote ulipo MUNGU akufungulie uzidi kuwa mchango kwa vijana wenzetu na taifa kwa ujumla.
 
Mbona points zako zinakinzana na za juu mkuu au sijaelewa... Utajitegenea vipi huku huna kazi? Au utafanya vipi biashara bila mtaji?

Umesema usitegemee ndugu wala marafiki ni vema ukatujulisha ni vipi utapata mtaji au hyo kazi

Sent from my TA-1004 using JamiiForums mobile app
Umeprove point ile ile anayoongea. Huo unaongea ni utegemezi uliopitiliza. Maisha ni kama kutupwa katikati ya msitu mnene ukiwa na kisu tu na umevaa pensi ya jeans huku miguuni upo pekupeku..... Na msitu unawamyama wakali wa kila aina na wenye sumu.....

Utakaa uanze kulia au utaanza piga hatua taratibu ukitafuta kutoka msituni kwenda barabarani kupata salama yako.


Kuanza kujitegemea sio hadi uwe na ajira kwanza. Sometimes ajira inakukuta miaka miwili au mitatu baada ya kuanza jitegemea.
 
Mimi nafikiri unatakiwa uamue wewe mru mwenyewe kama unataka utafute kazi au kama ufanye biashara yote yanawezekana ila watu wengi wanapenda sana kushikwa mkono.....

Kitu nilichojifunza broo ukisubili Kushikwa mkono maisha haya utachelewa sana nakumbuka miaka 5 iliopita niliamini ndugu zangu ambao wapo vitengo serikali na sekta binafsi niliamini watashika mkono lakini matokeo yake

Kila mtu alikuwa bize na mambo yake pale ndipo nilipojifunza katika haya maisha usimtegemee binadamu
 
Sijawahi kuwa na hata milioni ya mkupuo kwenye akaunti, lakini nilipoamua tu nianze kujenga nyumba... mwaka wa tatu huu nyumba naelekea kuhamia.

Ningesema niendelee kusubiri nipate pesa, ningeendelea kuota tu usingizini.

Cha ajabu ni kwamba najenga na maisha mengine yanaendelea vile vile, ni nguvu ya maamuzi tu.
Mkuu nielekeze uliwezaje na unaishi mkoa gani. Kama ni Dar es Salaam nakupa hongera sana
 

Similar Discussions

55 Reactions
Reply
Back
Top Bottom