Bila kujali vyama, tumpongeze na tuwapongeze wote kwa ujumla, haikuwa kitu rahisi

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Oct 31, 2014
5,347
11,447
Kwa furaha kubwa naandika nikitoa shukrani kwa Serikali ya Jam ya Muungano na pia Mkuu wa Mkoa wa Dar kwa kuamua rasmi siku ya kumaliza Corona.

Hatua hii ni kubwa na najua Mabeberu itawaumiza sana kuona nchi maskini imeweka siku maalumi ya kumaliza Corona na maisha kurudi upya.wao bado wanahangaika nayo.

Leo nlipokuwa napita barabarani nawaona wauza barakoa najiuliza nikitabasamu baada ya Jumapili watauza nini sasa? Wengine nimewashauri hizi barakoa walizobaki nazo wauze hata tsh 100 ili wamalize mapema.

Naona kabisa sanitizer hazitakuwa deal tena, maana za nini na Corona tunaenda kui lockdown Jumapili? Nashauri lifanyike tamasha kubwa la Kumaliza Corona Dar es Salaam.

Dunia ijue sisi tumeweza. Kiukweli tumeishi miezi miwili na nusu ya mateso shida na adha kubwa, kumbe viongozi wetu walikuwa wakifanya mchakato na sasa mchakato umefanikiwa. Jumapili hakutakuwa na Corona tena DSM, itabaki historia.

Naipongeza serikali na nampongeza mkuu wa mkoa kwa kufanikisha hilo.hili, jambo si rahisi hata kidogo, ni juhudi kubwa na maarifa yametumika.


Narudia haikuwa kitu RAIS.
 
Rais Wala Makonda hawajasema Kama Corona imekwisha Ila Corona imepungua, Wagonjwa wamepungua kwa kiasi kikubwa, wengi wao Nyungu na dawa za asili zimesaidia kwa kiasi kikubwa, Hofu juu ya Corona imepungua kwa wananchi.

Ukiacha madaktari na wauguzi waliopambana Ila Mungu ametupambania Kama Taifa. Hatuna budi kumshukuru mwenyezi Mungu kwa yote.

JPM tunampongeza kwa Uthubutu wa kumwachia Mungu ni Jambo la kushangaza lakini limefanikiwa ,Masheikh, Wachungaji,Wana maombi na wote walio liombea Taifa wanastaili pongezi pia.Hata wale waliokua waki ikosoa serikali wanastaili pongezi wali ifanya serikali irekebishe baadhi ya kasoro mfano mazishi ya usiku, watu kuzikwa ambako ndugu hawakupenda, mapungufu ya vifaa Tiba n.k

Leo kuna sehemu nimeona Shehena ya vifaa tiba vikishushwa kutoka ng'ambo.Hii inaonyesha serikali inajali na inasikiliza wananchi wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom