Bila kadi hupandi mabasi ya mwendokasi kuanzia August 1

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
USAFIRI MWENDOKASI: Uongozi wa UDART leo umetangaza kuwa kuanzia Agosti Mosi 2016, hakuna mtu mzima atakayepanda mabasi hayo bila kutumia Kadi, mfumo wa tiketi utatumiwa na wanafunzi pekee.

=======

Kampuni ya Usafirishaji ya mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam (UDART) inatarajia kusitisha matumizi ya tiketi za karatasi ifikapo Julai 30 mwaka huu.

Uamuzi huo unalenga kudhibiti foleni za kununua tiketi za karatasi kutokana na idadi kubwa ya abiria; kati ya 150,000 na 200,000 wanaotumia usafiri wa mabasi hayo kwa siku. “Kwa siku abiria wapatao laki moja na nusu hadi laki mbili wanatumia usafiri wa mabasi yaendayo haraka kila siku, sasa kumekuwa na foleni vituoni na pia tunakusanya magunia na magunia ya karatasi na kuna maeneo mengine uchafu unakuwa mwingi,” Mkurugenzi Mtendaji wa UDA-RT, David Mgwasa aliwaambia waandishi wa habari jana.

Hata hivyo, kusitishwa huko kwa tiketi za karatasi, kunalenga watu wazima pekee wanaolipa Sh 650. Wanafunzi wanaolipa Sh 200, wataendelea kutumia tiketi za karatasi ambazo zitakuwa zikipatikana kwenye vituo vya mabasi.

Mgwasa alisema licha ya hatua hiyo kulenga kupunguza foleni kwenye vituo, pia itaondoa uchafu unaotokana na tiketi za karatasi.

Wakati huo huo, alisema kutokana na mpango huo wa kusitisha tiketi, kuanzia leo kampuni imepunguza gharama ya ununuzi kutoka Sh 5,000 kwa tiketi za hadi Sh 2,000, Sh 500 itakuwa gharama ya kadi na Sh 1,500 ni nauli. “Kuanzia kesho (leo) kadi zitauzwa kwa gharama ya Sh 2,000 kwenye vituo vyote vya mabasi ya mwendokasi,” alisema.

Mgwasa alisema tangu kuanza kuuzwa kwa kadi hizo kwa gharama ya Sh 5,000 tayari kadi 55,000 zimeshanunuliwa na kubakia kadi 150,000 ambazo ziko kwenye promosheni ya kuuza kadi kwa Sh 5000.

Alisema baada ya kadi hizo kuisha, abiria atalazimika kununua kadi hiyo kwa thamani ya Sh 5,000 bila kuwekewa fedha za nauli kama ilivyokuwa awali.

Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Maxcom Afrika (MaxMalipo), Deogratius Lazari alisema wamejipanga kuhakikisha tiketi za kadi zinapatikana kwenye vituo vya mabasi. Aliwataka wateja kuhakikisha wanaweka salio katika vituo hivyo. “ Kampuni za simu ziko katika hatua ya mwisho za kukamilisha mifumo yao ili abiria aweze kuongeza salio kupitia mitandao ya simu ila kwa sasa abiria wanatakiwa kutumia vituo vyetu vya mabasi
 
Hata huko tulikogeza matumizi ya kadi kwenye usafiri kuna cash pia. Maana si kila raia anatumia usafiri wa umma daily; wapo wageni wanoingia Dar kwa siku chache na kuondoka na pengine hajui atarudi tena lini, wapo ambao wana usafiri wao binfasi lakini hupata dharura akatumia hayo mabasi may be once in a year kwa mifano hiyo ni upuuzi kulazimisha kila abiria awe na kadi.

Pia matumizi ya credit card yanahitaji mtu mwenye kipato kinachoeleweka endelevu lakini wengi wa abiria wanaotumia usafiri wa umma hapa Dar wana vipato vya kuungaunga. UDART tangu waanze wanaonyesha ni watu ambao ni wavivu kufanya utafiti kabla ya kufikia maamuzi.

Kubwa zaidi, huu usafiri bado unawatoa ushamba wengi wakazi wa Dar na wageni wa Dar sasa kuwaongezea hiyo kitu ni kuwavuruga zaidi. Hapo nahisi kuna mtu (mzabuni) wa hizo kadi analazimisha kazi
 
USAFIRI MWENDOKASI: Uongozi wa UDART leo umetangaza kuwa kuanzia Agosti Mosi 2016, hakuna mtu mzima atakayepanda mabasi hayo bila kutumia Kadi, mfumo wa tiketi utatumiwa na wanafunzi pekee.
Mkiambiwa mnakurupuka mnatupeleka senturo kuhojiwa. Sasa mimi nimetoka zangu Tarime leo, nimefika Dar naondoka keshokutwa, ukanikatishe kadi ya 5000 huko Tarime naenda kuifanyia nini?
 
hawa vichaa kabisa. Hata huko tulikogeza matumizi ya kadi kwenye usafiri kuna cash pia. Maana si kila raia anatumia usafiri wa umma daily; wapo wageni wanoingia Dar kwa siku chache na kuondoka na pengine hajui atarudi tena lini, wapo ambao wana usafiri wao binfasi lakini hupata dharura akatumia hayo mabasi may be once in a year kwa mifano hiyo ni upuuzi kulazimisha kila abiria awe na kadi. Pia matumizi ya credit card yanahitaji mtu mwenye kipato kinachoeleweka endelevu lakini wengi wa abiria wanaotumia usafiri wa umma hapa Dar wana vipato vya kuungaunga. UDART tangu waanze wanaonyesha ni watu ambao ni wavivu kufanya utafiti kabla ya kufikia maamuzi. Kubwa zaidi, huu usafiri bado unawatoa ushamba wengi wakazi wa Dar na wageni wa Dar sasa kuwaongezea hiyo kitu ni kuwavuruga zaidi. Hapo nahisi kuna mtu (mzabuni) wa hizo kadi analazimisha kazi
Akina Masaburi watapanda. Sisi wa tandale na uzurini tutaendelea na daladala as usual
 
USAFIRI MWENDOKASI: Uongozi wa UDART leo umetangaza kuwa kuanzia Agosti Mosi 2016, hakuna mtu mzima atakayepanda mabasi hayo bila kutumia Kadi, mfumo wa tiketi utatumiwa na wanafunzi pekee.
Kwanza niipongeze Serekali kwa kuanzisha huu mpango kwa kweli raha sana. Maana majuzi nilikuwa DSM nikajiona niko zaidi ya Uingereza maana ni raha sana! maana mwendo wa haraka kweli wa haraka. uenezwe maeneo yoote. Lakini watufahamishe sisi ambao si wakazi wa Dar-es-salaamu na wale ambao si wapandaji wa kila siku utaratibu utakuwaje?!?!
 
x2-4.jpg.pagespeed.ic.EfhEqBG53U.jpg


Uamuzi huo unalenga kudhibiti foleni za kununua tiketi za karatasi kutokana na idadi kubwa ya abiria; kati ya 150,000 na 200,000 wanaotumia usafiri wa mabasi hayo kwa siku.

“Kwa siku abiria wapatao laki moja na nusu hadi laki mbili wanatumia usafiri wa mabasi yaendayo haraka kila siku, sasa kumekuwa na foleni vituoni na pia tunakusanya magunia na magunia ya karatasi na kuna maeneo mengine uchafu unakuwa mwingi,” Mkurugenzi Mtendaji wa UDA-RT, David Mgwasa aliwaambia waandishi wa habari jana.

Hata hivyo, kusitishwa huko kwa tiketi za karatasi, kunalenga watu wazima pekee wanaolipa Sh 650. Wanafunzi wanaolipa Sh 200, wataendelea kutumia tiketi za karatasi ambazo zitakuwa zikipatikana kwenye vituo vya mabasi.
Mgwasa alisema licha ya hatua hiyo kulenga kupunguza foleni kwenye vituo, pia itaondoa uchafu unaotokana na tiketi za karatasi.

Wakati huo huo, alisema kutokana na mpango huo wa kusitisha tiketi, kuanzia leo kampuni imepunguza gharama ya ununuzi kutoka Sh 5,000 kwa tiketi za hadi Sh 2,000, Sh 500 itakuwa gharama ya kadi na Sh 1,500 ni nauli.

“Kuanzia kesho (leo) kadi zitauzwa kwa gharama ya Sh 2,000 kwenye vituo vyote vya mabasi ya mwendokasi,” alisema.

Mgwasa alisema tangu kuanza kuuzwa kwa kadi hizo kwa gharama ya Sh 5,000 tayari kadi 55,000 zimeshanunuliwa na kubakia kadi 150,000 ambazo ziko kwenye promosheni ya kuuza kadi kwa Sh 5000.

Alisema baada ya kadi hizo kuisha, abiria atalazimika kununua kadi hiyo kwa thamani ya Sh 5,000 bila kuwekewa fedha za nauli kama ilivyokuwa awali.

Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Maxcom Afrika (MaxMalipo), Deogratius Lazari alisema wamejipanga kuhakikisha tiketi za kadi zinapatikana kwenye vituo vya mabasi. Aliwataka wateja kuhakikisha wanaweka salio katika vituo hivyo.

“ Kampuni za simu ziko katika hatua ya mwisho za kukamilisha mifumo yao ili abiria aweze kuongeza salio kupitia mitandao ya simu ila kwa sasa abiria wanatakiwa kutumia vituo vyetu vya mabasi na wakala wa max malipo,” alisema.

Mabasi ya haraka yalianza kutoa huduma Mei mwaka huu kwa kuanza na tiketi za karatasi na baadaye, kuanzishwa
utaratibu wa kadi ambao haujaitikiwa kwa kiwango kikubwa.
 
Huyo Mkurugenzi ni mzembe anatakiwa atumbuliwe tu. Abiria wa kivukoni
wanalalamika usafiri kutoka fire kwenda kivukuni ni shida yeye mpaka sasa
amekosa ubunifu kidogo tu wa kutatua hilo tatizo?
 
Huyo Mkurugenzi ni mzembe anatakiwa atumbuliwe tu. Abiria wa kivukoni
wanalalamika usafiri kutoka fire kwenda kivukuni ni shida yeye mpaka sasa
amekosa ubunifu kidogo tu wa kutatua hilo tatizo?

Kabla ya hapo ulikuwa rahisi?
 
Tatizo ni uzembe tu kama abiria wanalalamika kukaa vituoni saa nzima
na kuna magari zaidi 100 maana yake hakuna ubunifu wanafanya kazi
kwa mazoea na huyo mkurugenzi atakuwa hana uzoefu wa usafirishaji.
Angekuwa na supervisor wa kufuatilia changamoto vituoni na kufanya
mawasiliano ya haraka kwa idadi ya hayo magari matatizo yangepungua.
 
Kwa hesabu ipi ?
Kama abiria kwa siku ni laki mbili wanapanda asubuhi na kurudi jioni
200,000 * 1300=260,000,000
wastani kwa siku wapata kati 200m. mpaka 240m. kuna wanafunzi pia.
 
Na wa mikoani tukija Dar tutatumia usafiri huo kwa utaratibu gani kama hawataki cash? Yaani hadi maamuzi ni ya mwendo kasi tu, shida ipo.
 
Poa 2. Tutapanda hizi dala dala za kawaida. Ila pia wakumbuke kadi zao sio roho. mtu huwezi tembea nayo kila wakati.
 
Jamaa ni hawana ubunifu hata Uingereza kwenyewe kwenye miji bus yao kuna option ya kulipa cash ndani ya bus, unaweza kata tiketi na kulipa cash...dumb Tanzanians....
 
Poa 2. Tutapanda hizi dala dala za kawaida. Ila pia wakumbuke kadi zao sio roho. mtu huwezi tembea nayo kila wakati.
 
Kwa hesabu ipi ?
Kama abiria kwa siku ni laki mbili wanapanda asubuhi na kurudi jioni
200,000 * 1300=260,000,000
wastani kwa siku wapata kati 200m. mpaka 240m. kuna wanafunzi pia.
Hii mbona ni pesa ndefu,daaah haya maisha kkweli hayapo fair.
Milioni 260 kwa siku ,ukizidisha mara 30 ,unaongelea bilioni 7.8. Kwa mwezi.
Anyway, acha tuendelee kuokota chupa na kulima mchicha ,sijui kama tutatoboa...!!?
 
Back
Top Bottom