CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 4,985
- 4,083
Rais Samia bila dhuluma wala kukimbiza wafanyabiashara ameweka rekodi mpya ya ukusanyaji mapato | TRA yakusanya kodi ya TZS 2T mwezi Sept 2021,kazi iendelee||
"Hakuna kama Samia "
Wakati Hayati Rais Mkapa anaondoka madarakani Serikali yake ya awamu ya tatu ilikusanya wastani wa Tshs 322BL kwa mwezi na Wakati Mzee Jakaya Mrisho Kikwete anaondoka madarakani Serikali yake ya awamu ya nne ilikusanya wastani wa Tshs 850BL kwa mwezi na Wakati Hayati Rais John John Joseph Pombe Magufuli anaaga dunia Serikali yake ilikusanya wastani wa Tshs 1.4trl kwa Mwezi hakika wanastahili pongezi sana wazee hawa,
Rais Samia Suluhu Hassan baada ya kuapishwa kuiongoza Serikali kwa awamu ya Sita aliapa kamwe hatokubali Serikali yake kukusanya Kodi ya dhuluma namnukuu "Niheri tukusanye kidogo lakini kiwe cha halali kitatufaa " alisikika kwa Upole na unyenyekevu akiwaasa wateule wake,Rais Samia alishangaa watu kudaiwa kodi za nyuma"Presumptive Tax accessment " wakati tayari wanazo "Tax Clearance " na waliothibitisha kwamba hawadaiwi ni haohao wanaowadai tena kwa mara nyingine ,Kitendo hiki Rais Samia Suluhu alikiita kuwa kwa Mujibu wa Mungu na dini huo ni "udhulumati au dhuluma "
Wakati Serikali ya Rais Samia Suluhu imepanga kutumia Jumla ya Tshs 36.33trl kwa Mwaka wa fedha 2021|2022 mwaka ulioanza tarehe 01|07|2021 ambapo mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa
Tshs 26.03trl, sawa na 71.7% ya bajeti yote. Kati ya mapato hayo, mapato ya kodi ni Tshs 22.18trl, sawa na 13.5% ya Pato la Taifa. Aidha, Serikali inalenga kukusanya
mapato yasiyo ya kodi ya Tshs 2.99trl na mapato kutoka
vyanzo vya Halmashauri ni Tshs 863.9BL hii ni bajeti ya maajabu,
Mungu ni mwema,kama kasi yetu ni Tshs 1.97trl au Tshs 2T kwa mwezi,Chukuaa 1.9trl zidisha kwa miezi 12 utapata jumla ya Tshs 22.8 tutavuka lengo kwa 3% naomba mfahamu tangu uhuru hakuna Rais aliwahi kutenga Tshs 36.33trilioni kwa aajili ya bajeti ni Samia and only Samia,
Watanzania wenzangu tuendelee kulipa kodi kwa hiari kwaajili ya maendeleo yetu na ya watoto wetu na yawatoto wao,Tanzania tuko vizuri Sana kwa sasa pengine tangu uhuru japo ni niukweli mchungu kwa wengine.
VIVA SAMIA VIVA || VIVA TANZANIA VIVA