Bila dhuluma wala kukimbiza wafanyabiashara, Rais Samia aweka rekodi ukusanyaji mapato

CM 1774858

JF-Expert Member
May 29, 2021
4,985
4,083

Rais Samia bila dhuluma wala kukimbiza wafanyabiashara ameweka rekodi mpya ya ukusanyaji mapato | TRA yakusanya kodi ya TZS 2T mwezi Sept 2021,kazi iendelee||​

"Hakuna kama Samia "​


Wakati Hayati Rais Mkapa anaondoka madarakani Serikali yake ya awamu ya tatu ilikusanya wastani wa Tshs 322BL kwa mwezi na Wakati Mzee Jakaya Mrisho Kikwete anaondoka madarakani Serikali yake ya awamu ya nne ilikusanya wastani wa Tshs 850BL kwa mwezi na Wakati Hayati Rais John John Joseph Pombe Magufuli anaaga dunia Serikali yake ilikusanya wastani wa Tshs 1.4trl kwa Mwezi hakika wanastahili pongezi sana wazee hawa,

Rais Samia Suluhu Hassan baada ya kuapishwa kuiongoza Serikali kwa awamu ya Sita aliapa kamwe hatokubali Serikali yake kukusanya Kodi ya dhuluma namnukuu "Niheri tukusanye kidogo lakini kiwe cha halali kitatufaa " alisikika kwa Upole na unyenyekevu akiwaasa wateule wake,Rais Samia alishangaa watu kudaiwa kodi za nyuma"Presumptive Tax accessment " wakati tayari wanazo "Tax Clearance " na waliothibitisha kwamba hawadaiwi ni haohao wanaowadai tena kwa mara nyingine ,Kitendo hiki Rais Samia Suluhu alikiita kuwa kwa Mujibu wa Mungu na dini huo ni "udhulumati au dhuluma "

Wakati Serikali ya Rais Samia Suluhu imepanga kutumia Jumla ya Tshs 36.33trl kwa Mwaka wa fedha 2021|2022 mwaka ulioanza tarehe 01|07|2021 ambapo mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa
Tshs 26.03trl, sawa na 71.7% ya bajeti yote. Kati ya mapato hayo, mapato ya kodi ni Tshs 22.18trl, sawa na 13.5% ya Pato la Taifa. Aidha, Serikali inalenga kukusanya
mapato yasiyo ya kodi ya Tshs 2.99trl na mapato kutoka
vyanzo vya Halmashauri ni Tshs 863.9BL hii ni bajeti ya maajabu,

Mungu ni mwema,kama kasi yetu ni Tshs 1.97trl au Tshs 2T kwa mwezi,Chukuaa 1.9trl zidisha kwa miezi 12 utapata jumla ya Tshs 22.8 tutavuka lengo kwa 3% naomba mfahamu tangu uhuru hakuna Rais aliwahi kutenga Tshs 36.33trilioni kwa aajili ya bajeti ni Samia and only Samia,

Watanzania wenzangu tuendelee kulipa kodi kwa hiari kwaajili ya maendeleo yetu na ya watoto wetu na yawatoto wao,Tanzania tuko vizuri Sana kwa sasa pengine tangu uhuru japo ni niukweli mchungu kwa wengine.

IMG-20210916-WA0009.jpg

VIVA SAMIA VIVA || VIVA TANZANIA VIVA
 
Serikali yakusanya kodi Sh1.9 trilioni Septemba
SATURDAY OCTOBER 02 2021


Summary

Serikali imesema imekusanya kodi ya Sh1.9 trilioni kwa kipindi cha Septemba mwaka huu ikiwa ni sawa na asilimia 93.

Morogoro. Serikali imesema imekusanya kodi ya Sh1.9 trilioni kwa kipindi cha Septemba mwaka huu ikiwa ni sawa na asilimia 93.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Jumamosi, Oktoba 2, 2021 Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema makusanyo hayo ni makubwa kulinganisha na kipindi kama hicho mwaka 2020.

“Tuliweka malengo ya kukusanya Sh2.1trilioni, ukusanyaji huu ni mkubwa ukilinganisha na mwaka jana kipindi kama hiki tulikusanya Sh1.7 trilioni ambazo ni sawa na asilimia 80 ya malengo tuliyojiwekea ya kukusanya Sh2.2 trilioni” amesema Msigwa.
 
Mbona mapema sana kuanza kampeni za urais, vipi hamna uhakika na mama enu kwamba atatoboa?
Ni kama vile kipindi kile tulivyoanza kumtengenezea mazingira Lisu mara oh atahutubia umoja wa ulaya, mara atahutubia un mara atafungua case katika mahakama ya kimataifa dhidi ya Magufuli nk. Lkn cha kushangaza uchaguzi mkuu wa 2020 ulipofika Lisu mwenyewe aliangukia pua. Yani propaganda zetu zote na uongo tuliotengeneza havikusaidia kuwashawishi wananchi wampigie kura. Hii ndo Tanzania ndugu.
 
Nawasalimu kwa Jina la JMT,


Wakati Hayati Rais Mkapa anaondoka madarakani serikali yake ilikusanya wastani wa Tshs 322BL kwa mwezi,Wakati Mzee Jakaya Mrisho Kikwete anaondoka madarakani serikali yake ilikusanya wastani wa Tshs 850BL kwa mwezi na Wakati Hayati Rais Magufuli anaaga dunia Serikali yake ilikusanya wastani wa Tshs 1.4trl kwa Mwezi,

Rais Samia Suluhu Hassan baada ya kuapishwa kuiongoza Serikali kwa awamu ya Sita aliapa kamwe hatokubali serikali kukusanya Kodi ya dhuluma namnukuu "Niheri tukusanye kidogo lakini kiwe cha halali kitatufaa " alisikika kwa Upole na unyenyekevu akiwaasa wateule wake,Rais Samia alishangaa watu kudaiwa kodi za nyuma "Presumptive Tax accessment " wakati wanazo tayari "Tax Clearance " toka kwa haohao wanaowadai tena,Kitendo hiki Rais Samia alikiita kuwa kwa Mujibu wa Mungu na dini huo ni "udhulumati "

Wakati Serikali ya Rais Samia imepanga kutumia Jumla Tshs 36.33trl kwa Mwaka wa fedha 2021|2022 mwaka ulioanza tarehe 01|07|2021 ambapo mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa
Tshs 26.03trl, sawa na 71.7% ya bajeti yote. Kati ya mapato hayo, mapato ya kodi ni Tshs 22.18trl, sawa na 13.5% ya Pato la Taifa. Aidha, Serikali inalenga kukusanya
mapato yasiyo ya kodi ya Tshs 2.99trl na mapato kutoka
vyanzo vya Halmashauri ni Tshs 863.9BL,

Mungu ni mwema,kama kasi yetu ni Tshs 1.9trl kwa mwezi,Chukuaa 1.9trl zidisha kwa miezi 12 utapata jumla ya Tshs 22.8 tutavuka lengo kwa 3% naomba mfahamu tangu uhuru hakuna Rais aliwahi kutenga Tshs 36.33trilioni kwa aajili ya bajeti ni Samia and only Samia,

Tuendelee kulipa kodi kwa hiari kwaajili ya maendeleo yetu na ya watoto wetu na yawatoto wao,Tanzania tuko vizuri Sana kwa sasa pengine tangu uhuru japo ni niukweli mchungu kwa wengine.


#Kazi iendelee kwa kasi & nguvu zaidi

Be blessed & Happy Sunday
=============================

VIVA SAMIA VIVA || VIVA TANZANIA VIVA

View attachment 1961007
Hongera raisi wetu.
 
Mifumo aliyoiweka Magu ndio inafanikish hayo, huyu mama enu within 6 months hawezi kufikia level ya ukusanyaji huo.
RIP JPM
Unapenda sana kubishana Mkuu,

Mifumo gani inayombeba Rais Samia leo?

Rekodi zinaonesha wafanyabiashara walikimbia sasa kukimbia ndio mfumo wa kumfanya Rais Samia avunje rekodi hizi?

Jifunze jufikiri Kizalendo mkuu wangu,



#KAZI IENDELEE KWA KASI & WELEDI ZAIDI
 
Back
Top Bottom