The Giantist
JF-Expert Member
- Dec 12, 2018
- 214
- 86
Ni ukweli tupu kuwa, watanzania wanahitaji maendeleo. Lakini haiwezekani ikawa kweli kuwa, maendeleo hayo yanaweza yakapatikana pasipo na demokrasi. Na inafahamika waziwazi kuwa, dhana ya maendeleo ni dhana iliyo pana sana, na kimsingi ni dhana ambayo mjadala wake ni bado unaendelea hata sasa. Kwa maana hiyo ni mjadala endelevu!
Hata hivyo, ili kuweza kuyafikia maendeleo hayo, ni dhahiri kuwa ni lazima kwanza tuweze kuendelea kwenye demokrasi. Ikumbukwe kuwa demokrasi ni hali ya kuwa. Hivyo, kwa jinsi hiyo mchakato wa kuhakikisha maendeleo ya kiuchumi yanapatikana ndani ya Tanzania kwa watanzania wote, basi ni lazima hali yetu ya kuwa na haki na usawa na uhuru binafsi ndani ya jamii, ipate kuwepo: Hali hiyo ni lazima nayo ipate kuwa nzuri, kwa maana ya demokrasi safi nchini.
Hata hivyo, ni kweli kuwa, kupitia demokrasi, nchi yetu itapata kuboreshwa na kujengwa na sisi sote, kwani ni demokrasi ya uwajibikaji na ya uzalendo ndio inataka hivyo: Kupitia demokrasi, kila raia atakuwa uhuru kwa kutoa nje mawazo yake ambayo ni lazima yawe na tija kwa taifa: Kupitia demokrasi, nchi haitaongozwa kwa utashi wa kiongozi pekee, ila ni kwa msingi wa utawala wa sheria (yaani katiba ya nchi). Kwa hiyo ni ngumu kuitenganisha demokrasi na maendeleo. Maendeleo ni tunda la demokrasi; na demokrasi ndio chachu ya ustawi wa maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii.
Na kwa jinsi hiyo tangu uhuru hata sasa, taifa letu chini ya serikali inayoundwa na CCM, ililitambua hilo. Na kwamba ili kwanza tuweze kuendelea, ilitakiwa kwanza tuipate demokrasi ya uhuru. Na hata baada ya kuwa huru, serikali za CCM za awamu zote zimeipa kipaumbele suala zima la demokrasi ili kuweza kulipatia taifa letu maendeleo katika nyanja zote muhimu. Ifahamike kuwa ni CCM inaamini kuwa, demokrasi kwanza kwa ajili ya maendeleo ya taifa.
Hata hivyo, ili kuweza kuyafikia maendeleo hayo, ni dhahiri kuwa ni lazima kwanza tuweze kuendelea kwenye demokrasi. Ikumbukwe kuwa demokrasi ni hali ya kuwa. Hivyo, kwa jinsi hiyo mchakato wa kuhakikisha maendeleo ya kiuchumi yanapatikana ndani ya Tanzania kwa watanzania wote, basi ni lazima hali yetu ya kuwa na haki na usawa na uhuru binafsi ndani ya jamii, ipate kuwepo: Hali hiyo ni lazima nayo ipate kuwa nzuri, kwa maana ya demokrasi safi nchini.
Hata hivyo, ni kweli kuwa, kupitia demokrasi, nchi yetu itapata kuboreshwa na kujengwa na sisi sote, kwani ni demokrasi ya uwajibikaji na ya uzalendo ndio inataka hivyo: Kupitia demokrasi, kila raia atakuwa uhuru kwa kutoa nje mawazo yake ambayo ni lazima yawe na tija kwa taifa: Kupitia demokrasi, nchi haitaongozwa kwa utashi wa kiongozi pekee, ila ni kwa msingi wa utawala wa sheria (yaani katiba ya nchi). Kwa hiyo ni ngumu kuitenganisha demokrasi na maendeleo. Maendeleo ni tunda la demokrasi; na demokrasi ndio chachu ya ustawi wa maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii.
Na kwa jinsi hiyo tangu uhuru hata sasa, taifa letu chini ya serikali inayoundwa na CCM, ililitambua hilo. Na kwamba ili kwanza tuweze kuendelea, ilitakiwa kwanza tuipate demokrasi ya uhuru. Na hata baada ya kuwa huru, serikali za CCM za awamu zote zimeipa kipaumbele suala zima la demokrasi ili kuweza kulipatia taifa letu maendeleo katika nyanja zote muhimu. Ifahamike kuwa ni CCM inaamini kuwa, demokrasi kwanza kwa ajili ya maendeleo ya taifa.