Big Brother Africa: What a waste!

Maxence Melo

JF Founder
Feb 10, 2006
4,196
13,187
Nimekuwa nikifuatilia Big Brother Africa kwa muda sasa lakini nilichokuja kugundua ni kuwa hili ni shindano moja chafu sana. Halipendezi kuingiwa na mtanzania.

Haya ni mawazo yangu binafsi. Sifurahishwi kabisa na kitendo cha cameras kumulika maeneo ya bafuni wakati wanaume na wanawake wanaoga. Huu ni udhalilishaji ili kupata milioni 100 tu. Binadamu anapoharibiwa utu wake kwa kiwango hiki nashindwa kuelewa nini maana yake kwa Afrika.

Mwanamke heshima yake ni kuficha maziwa yake na nyeti zake. Zinapoanikwa wazi wazi tena kwenye televisheni ni hatari sana. Hii ndiyo maana halisi ya Big Brother Africa? Wale wasiokuwa na Dstv hamwezi kuona ushenzi unaoendelea kwenye jumba hili hadi muoneshwe. Kwa wale wenye kubahatika kuona vema naamini watakubaliana nami kuwa udhalilishaji umezidi kiwango cha kawaida.

Napendekeza waandaaji kuondoa mara moja huu udhalilishaji wa kuonyesha vijana wetu wakiwa uchi na hata kuwahamasisha wengine kutamani kuingia kwenye jumba hili kufanya ufuska kama walivyoonekana kufanya karibuni.

Kwa bahati, tamaduni za nchi zetu Afrika karibia zinaelekeana, hakuna ambako vitendo hivi vinaungwa mkono hata kidogo.
 
Maxence, nakuunga mkono kwa tahariri yako,
hapo ni aibu, kijana mh sijui alikuwa anawaza nini?manake hilo pozi na nusu suruali...

Hivi limeshaisha au bado linaendelea?
wengine tulikojichimbia na majukumu ya kilasiku unashindwa kufatilia mambo kwenye net (ukiacha JF)

Ahsante
 
alikuwa anavaa suruali... mbaya zaidi aliwahi kutoa taulo lake kabla ya kuipandisha vizuri suruali... cha ajabu chupi kwake ni kimeo
 
alikuwa anavaa suruali... mbaya zaidi aliwahi kutoa taulo lake kabla ya kuipandisha vizuri suruali... cha ajabu chupi kwake ni kimeo

Tatizo sio mara moja moja. Imeonekana kuwa kawaida na kuna yule dada wa Uganda ndiye kabisaaa anakaa 95% uchi japo mnene sana kama mimi.

Inasikitisha. Hizi picha za Big Brother zinaonekana mbaya lakini naomba wadau tukemee hili shindano ikibidi vijana wetu wasiende.
 
Tatizo kubwa kila kitu ambacho mzungu anafanya kwa Afrika ni kitu kizuri, na huu mkumbo uko hata kwa viongozi wetu wa kitaifa hebu angalia rais wetu anavyowapapatikia wazungu utafikiri hajawahi kuona mzungu. Amelishwa peremende sasa matatizo ndio tunayapata na bado hadi siku ambapo WTZ wataona kuwa hawa viongozi hawafai. Hivi inaingia akilini kweli kuona rais anakwenda nje kuombaomba kama masikini anajenga taifa la ombaomba.

Matatizo ya Tanzania yatatatuliwa na WTZ wenyewe na si vinginevyo. Ulimbukeni umeingia kuanzia vipindi vya kijinga kama hivi n.k.
 
Maxence,

Huu ni ujinga, upuuzi na ufedhuli! Yaani ni ajabu jinsi hawa BBA wanavyowafanyia binadamu wenzao na kwa ujinga wao washiriki wanaona ni sifa!

Yaani Mil 100 ambayo kuipata kwake ni bahati tena kwa aibu kama ya huyo bwana mdogo. Yaani huyo MTZ anakubali wazazi wake na ndugu zake waone aibu yake? What a shame to this poor guy and others!

Mimi nadhani ni vizuri serikali itangaze shindano hili ni batili kwa Watanzania na Watanzania wasiruhusiwe kamwe kushiriki BBA.
 
Mkuu umenena! huyu akirudi kashinda au kawa wa pili au hata wa tatu atapewa mapokezi ya kitaifa na barabara kufungwa! Si ajabu somebody like Joel Bendera atakuwepo kumlaki shujaa alie peperusha bendera yetu...
 
lakini upande mwingine tuangalie,
wanaoenda kwenye hayo mashindano ni watu wazima wenye akili timamu,
na wanajua kuwa kuna camera kila kona hadi chini ya uvungu
ni wajibu wao kuwa makini wakati wote,........
 
Na kibaya zaidi, inaonekana kama mdudu wake ni mdogo sana, nadhani hii itamfanya atolewe haraka sana.Nadhani yeye atatolewa wiki iajayo.
 
Na kibaya zaidi, inaonekana kama mdudu wake ni mdogo sana, nadhani hii itamfanya atolewe haraka sana.Nadhani yeye atatolewa wiki iajayo.

Basi hatatoka peke yake maana hata huyu chini naye wale wale

ribidk-1.jpg
 
kweli haya mashindano ni waste of human dignity lakini kwenye kusaka pesa watu hudhalilika. Labda kwa ushauri tu, wengi hawayapendi basi na si muache kuangalia wakati juhudi za kukemea zikiendelea. Maana hauwezi kuzuia TV kuonyesha uchafu na huwezi zuia watu kushiriki the only way ya kutokukereka ni KUTOKUANGALIA.
 
Ndugu zangu wote milio changia.... Tanzani tumeshaharibika kwa kutaka kuiga uzungu.... rais wetu hawezi kukemea hili shindano wala serikari haiwezi kulikemea kwa sababu tu ni la kizungu.... Rais wetu mwenyewe ananyenyekea wazungu kama ndio waliompigia kura....... kila siku anatafuta misaada mara marekani, mara uk yaani kila nchi anaenda kuombaomba utafikiri watanzania tumekuwa matonya.PILI ajira ni kimeo tanzania ndio maana watoto wetu wanaamua kujitosa wadhalilike ili wapate pesa.... Tanzania yetu ukiamua KUJIAJIRI utavunjiwa kibanda chako eti wanasafisha jiji.... ukiuza mama ntilie mgambo watakula chakula chako na kukutilia mchanga.... je pesa ambazo ndio kila kitu kwa maisha ya sasa zitapatikana kwa njia ip??????????
 
navyowafahamu viongozi wetu kama kijana huyu akishinda,linaweza kupewa nafasi ya kitaifa ili kufunika wingu la kisiasa la sasa,hakawii kupelekwa hata bungeni.

ndio taifa tunalolijenga
 
jamani unachosema ni kweli bba ni takataka na inaaribu maadili, kwanza wahajali kipindi kile kinaangaliwa watu wa aina gani na wenye umri gani!!!! mtu huwezi uza utu wako kwa milioni 100???? wakati unaweza fanya kazi kwa bidii na ukapata pesa hizo??? matajiri wangapi wanamabilioni ya pesa na wamepata bila kuidhalilisha??? huyo rachard ni mtanzania na ni mume wa mtu!!! lakini hana haya wala adabu wala hamuogopo mungu wake waafrika tuamke!!! hao washiriki hawajadhalilisha wamajidhalilisha wenyewe kwa tamaa zao.... hakuna wototo hapo wote hapo ni mijitu mizima....
 
mtu huwezi uza utu wako kwa milioni 100???? wakati unaweza fanya kazi kwa bidii na ukapata pesa hizo???

you are kidding....
kazi ipi bongo itakulipa hizo hela kwa mkupuo? KCC ni 84,000

Kupanga ni kuchagua,
hwaibi wal kuhujumu uchumi..
wanachotakiwa ni kujisitiri vizuri.
 
Akirudi jamaa atakuwa kwenye Bongo celebrety http://bongocelebrity.com/ kama nyota wa kitanzania aliyepeperusha bendera ya taifa kwa mashindano ya nyuchi! Si mnakumbuka ya Mwisho Mwampamba? ilikuwa kama public holday maana sujaa wa kitanzania alikuwa anatua, mapikipiki na magari ya kumwaga msafara kama ule wa coming to America.
 
Wana JF hayo ndiyo maisha ya wazungu. Kama mdau alivyosema hapo juu, mara nyingi sisi waafrika huwa tunaona kila kitu ambacho mzungu anafanya basi ni cha kisasa na maendeleo.

Kwa kweli kawa mtindo huu, na watoto wetu wanaangalia hizo TV basi ni karaha tupu.

Nawasilisha
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom