Bidhaa kupanda bei baada ya Uchaguzi Mkuu!!!!!!

Kahamba

Member
Nov 1, 2010
58
16
Tulizungumza sana wakati wa uchaguzi kwamba CCM inachukua pesa kutoka kwa wafanya biashara iwe kwa mtindo wa kuchangia (kinafiki) au kwa kulazimishwa (kutishwa). Katika hali hii tulitazamia kuona bidhaa zinapanda bei ikiwa ni njia ya watu hawa kurejesha pesa zao walizotoa kwa ajili ya kampeni za CCM. Kitendawili hiki kimeteguliwa baada ya bidhaa mbalimbali kutangazwa kupanda bei katikati ya wiki iliyopita. Songea mfuko wa sementi unadaiwa kupanda kutoka 14,000/= hadi 18,500/=; Da es Salaam sementi ni 13,500/= kutoka 12,500/=. Kilo ya ngano sasa ni 1,000/= kutoka 800/=.
Katika hali hii, je, tutafika?
 
Sumbawanga bei ya mafuta ya petroli ni TZS 5000 kwa lita: Mpanda ni TZS 3000 kwa lita....

Tunaendelea kusonga nyuma!!!!
 
Back
Top Bottom