akashube
JF-Expert Member
- Dec 24, 2009
- 401
- 23
Enzi nikiwa naishi Manzese ndipo nilipojifunza kuwa Biblia ni kiboko. Sikuzote tulikuwa tunadhibiti panya bila matatizo, na walipokuwa wakitokea nyumba za jirani bado tulikuwa na sumu ya panya na mitego ya panya na hakukuwa na tatizo kuwadhibiti.
Siku moja usiku mchuzi ulidondokea kwenye biblia na tukawa tumeiacha chini bila kuiokota lakini ikiwa kwenye hali mbaya kwa kulowa na mchuzi. Tulipoamka asubuhi yake tukakuta biblia imeliwa karibu robo tatu. Tangu hapo hatukuweza kukamata panya tena na ilibidi tuuze nyumba kuwakimbia panya.
Mambo yenyewe yalikuwa hivi:
Kuna siku panya waliingia kupitia chini ya geti na nilipotoka na rungu kuwafukuza nikasikia wakisema 'kila mtakapopakanyaga nimewapa'. Nilikasirika nikarusha rungu nikamkosa yule panya akakaa pembeni akakunja nne akasema 'no weapon formed against me shall prosper'.
Baada ya siku mbili nikaweka mtego mkubwa na badala yake nikakuta kuku wetu wa mayai kanasa halafu wakati najaribu kutoa mzoga wake nikasikia panya anaimba 'shimo wamenichimbia mie watatumbukia wenyewe humo'...halafu panya wengine wanajibu.
Mwishowe nikaamua kufuga paka, siku iliyofuata usiku nikashangaa paka anafukuzwa na panya mkubwa (fuko) halafu panya ambaye nahisi ndiye aliyekula biblia akasema 'aliye ndani yetu ni mkuu kuliko aliye nje'.
Mwisho tukaamua kuhama nyumba...siku tunahama kila mtu alihamia anakokujua yeye, na wakati naondoka nikasikia yule panya aliyekula biblia anasema 'Adui zako watakujia kwa njia moja lakini watakimbia kwa njia saba'.
BIBLIA NOMA!!!
Siku moja usiku mchuzi ulidondokea kwenye biblia na tukawa tumeiacha chini bila kuiokota lakini ikiwa kwenye hali mbaya kwa kulowa na mchuzi. Tulipoamka asubuhi yake tukakuta biblia imeliwa karibu robo tatu. Tangu hapo hatukuweza kukamata panya tena na ilibidi tuuze nyumba kuwakimbia panya.
Mambo yenyewe yalikuwa hivi:
Kuna siku panya waliingia kupitia chini ya geti na nilipotoka na rungu kuwafukuza nikasikia wakisema 'kila mtakapopakanyaga nimewapa'. Nilikasirika nikarusha rungu nikamkosa yule panya akakaa pembeni akakunja nne akasema 'no weapon formed against me shall prosper'.
Baada ya siku mbili nikaweka mtego mkubwa na badala yake nikakuta kuku wetu wa mayai kanasa halafu wakati najaribu kutoa mzoga wake nikasikia panya anaimba 'shimo wamenichimbia mie watatumbukia wenyewe humo'...halafu panya wengine wanajibu.
Mwishowe nikaamua kufuga paka, siku iliyofuata usiku nikashangaa paka anafukuzwa na panya mkubwa (fuko) halafu panya ambaye nahisi ndiye aliyekula biblia akasema 'aliye ndani yetu ni mkuu kuliko aliye nje'.
Mwisho tukaamua kuhama nyumba...siku tunahama kila mtu alihamia anakokujua yeye, na wakati naondoka nikasikia yule panya aliyekula biblia anasema 'Adui zako watakujia kwa njia moja lakini watakimbia kwa njia saba'.
BIBLIA NOMA!!!