Biashara ya Vyombo vya Habari inadorora na kufa kutokana na upendeleo wa habari

Tulimumu

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
14,304
12,965
Biashara ya vyombo vya habari kama magazeti, redio na televisheni kwa sasa ina yumba kutokana na uendeshaji wa Vyombo hivyo ambao una walazimisha wamiliki kutoa au kuegemea upande mmoja wakati huko wanako egemea hakuna ruzuku wanayo pata ili kuendesha vyombo hivyo.

Kwa sasa kundi kubwa la wasomaji wa magazeti hali nunui tena magazeti badala yake wana tegemea mitandao ya kijamii. Hali kadhalika wengi hawategemei redio na TV za ndani kupata balanced story badala yake wanategemea vya nje kama DW na BBC. Kwa mtindo huo vyombo vingi vina kosa wasikilizaji wa habari na kwa hiyo kukosa mapato. Kwa sasa vyombo vyenye uhakika wa maisha ni vile vya chama tawala na serikali tu ambavyo hata vikikosea haviadhibiwi lakini wenzangu na mimi tia maji tia maji hali ni ngumu na wakati huo huo pingu ziko mlangoni zina wangoja mfanye kakosa kadogo tu nje ya kusifia.

Hali ilivyo sasa ni kuwa gazeti, redio na TV vina weza kufungiwa au kufutwa bila kupewa nafasi ya kujitetea kwa kuwa mlalamikaji ndiye polisi, hakimu na gereza pia. Poleni sana wamiliki wa Vyombo vya Habari
 
Yaani sasa hivi watu wanaosoma magazeti ni wachache, na wanaoangalia TV haswa habari wanazidi kupungua, wengi wanaangalia kwa mazoea na au kwa kukosa chaguo sahihi, kwani vituo vyote ni majanga. Waandishi wengi wa habari wanazidi kujikuta kwenye wakati mgumu na hawana pa kusemea. Zile habari tulikuwa tunasikia kwenye nchi za madictator, rasmi sisi ndio tuko kwenye hali hiyo. Tushukuru Mungu kuna mitandao ya kijamii, vinginevyo wote tungegeuzwa Mazezeta.
 
Yaani mpaka sasa kwa mambo yaendavyo wapinzani wakuu ndio washindi kinadharia
Tatizo itakua ngumu mno kutangazwa tarehe 28.
 
Hakuna mtu ambaye hajaumizwa na Huu Utawala wa One man show.

Ma dikteta wengi huwa wanapenda sana Kukandamiza Uhuru wa Vyombo.

Namnukuu
"Alisema na nyinyi wamiliki wa vyombo vya habari hampo huru kiasi hicho whatch out your not free to that extent whatch".
JPM.

Hakika huu ni utawala wa mkono wa chuma
 
Nawaona waandishi wanavyo ogelea maji ya shingo wakati wanasahau kuwa maji yanazidi kumsogeza kwenda mbele.
 
Back
Top Bottom