Biashara ya Uwakala na upotevu wa pesa

Pole sana mkuu! Ila mimi naona tu nikualert kuhusiana na ushauri walioutoa wadau hapo juu! Kuna mdau kakushauri kutumia daftari akimaanisha maybe unachanganya katika mahesabu yako, umemhakikishia kuwa huwa upo makini! Kuna mdau mwingine kakushauri uwe unaombea na kukemea sehemu yako ya kazi ili kuikabidhi katika ulinzi wa Mungu, ukamwambia sawa utafanya hivyo! Then kuna mwingine kakwambia weka na mkaa na ndimu kwenye droo au mfuko unamohifadhi fedha, naye pia ukasema sawa utajaribu kufanya hivyo!......Ok umefanya vizuri kwa kuwa muungwana wa kupokea kila ushauri! Sasa na mimi nakushauri kwamba, ukiamua kujikabidhi kwa Mungu kwa imani ya dhati kabisa, basi usijichanganye na nguvu za aina nyingine kwani utafanya nguvu ya Mungu ijitoe kwako! Mfano kama umeamua kuweka mkaa na Limau, Hata ukiomba ulinzi wa Mungu hapo ni kazi bure manake utakuwa unalinganisha nguvu ya Mungu aliyekuumba wewe na wewe ukalima limau na kuchoma mkaa, alafu unamlinganishana nguvu ya Limau na mkaa! Hapa simaanishi kuwa napingana na wadau waliotoa ushauri wa kutumia ndimu na mkaa, bali natahadharisha mazingira ambamo nguvu ya Mungu huwa inafanya kazi na mle ambamo Mungu hawezi kujichanganya hata kwa kumchanganya! Ukiweka ndimu na mkaa basi amini katika hivyo na ukijikabidhi kwa Mungu, amini katika yeye tu!

Mkaa unatengenezwa na mti,Je miti kaumba nani???

Mti unaotoa malimao umeumbwa na nani?

Hivi mnajua huko kanisani kuna vitu mnadanganyana ambavyo Mungu hajawahi kabisa kuviita uchawi??


Hivi miti aliyoumba Mungu kwa ajili ya kumkinga mtu na nguvu za kichawi nayo mnaiita uchawi???unadhani kwanini Mungu ameumba miti hii na kwanini kaipa nguvu ya kupingana na nguvu za giza?ina lengo gani?inasaidia kwa watu wake?think think think


Achenk kukalili jamani hapo mkifika kanisani mnapewa vitambaa vya upako mara mafuta ya upako lakini limao tu kwenye sehemu ya hela for good purpose tayari uchawi....
 
Tatizo lako unaelezwa loop holes za uhakika kabisa za fedha kuweza kupotea lakini wewe unabaki kubishabisha. Huo ubishi ndiyo unakufanya uibiwe. Na nimeshaona akili zako zilipolalia. Unataka uaminishwe imani potofu na ya uongo kabisa ya chuma ulete! Nakuhakikishia hakuna kitu kama chuma ulete. Ni uzushi wa kijinga kabisa. Fedha zinapotea kwa watu kutokuwa makini i.e. uzembe. Na tabia ya uzembe Tanzania imetamalaki kila kona. Sehemu za huduma unakuta mtu anahudimia watu watatu kwa wakati mmoja huku anazungumza na simu. Ushauri wangu: Fedha unazembea munawenyewe kwenye kuhesabu au mfanyakazi wako anakupiga (usiniambie ni mfia dini ni siku hizi ni kichaka cha maovu)
♥♥♥ Unaandikaga kwa kucement vyema Sana...Kuna sauti anayoitaka yeye ..sio advices...
Mkuu ni kweli biashara nyingi Sana zimefungwa..lakini apart kusinhizia Hali yetu ya uchumi % kubwa Sana ya wafanyabiashara/wajasiriamali wa kitz hatupo serious ..yaan nadhani ndo asili yetu ..walioamua kujinasua ndo hao unawaona wanapiga hatua..
Cheki huu Uzi had unawaza hivi tuko serious kweli na biashara??? Mtu analalamika ameibiwa zaidi ya 600k lakini amerelax akisubiria miujiza ...mtu unaibiwa daily hela hushtuki .unaanza tupia nyanya sijui limao dah🤸🤸!

Jamani biashara ni Kama dini....ifateni misingi yake. Be honest wapi unafeli...mbona utaona kaunafuu!! Way back 15yrs dingi alikua ananicrush mno mno nikimwambia nataka kuwa successful ..alikua ananiambia kitu kimoja ambacho Sasa hv napanbana nacho mnoo...
Alikua anasema huez kufanikiwa Kama utaendelea kuwa mzembe .unaacha hela popote tu mradi umeweka..nilikua namchukiaaaa.lakini Sasa hivi namwelewa Sana... Biashara sio mziki kusema utabadilisha steps utakapotaka wewe. Biashara ni maagano na dhamira yako unataka kufika wapi... Nadhan mitaji ya kupewa inatufanya tuone dunia ni rahisi tu ..! Yaani tupo tu hatujuelewi ..hizo droo zitawekwa mkaa ,limao..ndimu..majibu..chumvi, mapumba,mashudu lakininusipoamua kusimama na kuwa makini utajikuta kila mwaka umerudi kwenye zero...unalaumu kila mtu..serikali,Hali ya hewa,wateja,frame mbaya,etc etc..kumbe shida ni wewe mwenyewe KIMEO!🤸
 
Hakuna chuma ulete,shida iko kwako namna ya kutunza kumbukumbu. Hakikisha unapiga hesabu asubuhi wkt wa kufungua piga pia ukifunga jioni,alafu usisahau kuweka matumizi kama yapo utaona zinakoenda. Usisahau kuandika unazotumia hata iwe mia.
Nb: kwa kuanzia fanya mwenyew hata wiki bila ya kuwepo binti,utaona inakaa poa,mpe apige yeye asubuhi na jioni na mwambie ikipungua hata mia atalipa.
 
Sijarelax dear... naweza nikawaza hivyo naikawa tofauti huwezi muhukumu mtu tu .ndio maana nimeomba ushauri na nitafatilia huu ushauri ninaopata na bado ikawa hvyo basi ninahaki kumuhukumu nayeye pia
utachuma dhambi bure kwa kumuhukumu huyo binti bila ushahidi, hakikisha pesa zote unazicontrol mwenyewe. piga mahesabu ya pesa zote kila baada ya kufanya muamala mmoja , usisubiri jioni hapo utagundua tatizo, ukimuacha mwenyewe binti kabla ya kutoka piga hesabu , ukirudi piga hesabu, hata mara 50 kwa siku , utalijua tatizo
 
Itakuwa wazee wa "Ndele" wanapita na mashuka ya Mmasai! Muda wa kufanya kazi na wazee wa Bagamoyo umewadia. Biashara ni ngumu sana kibongobongo maana kanuni za vitabuni pekee hazitoshi. Lazma uende nje ya box kistaili. Wanasema vipande vya mkaa kwenye droo ya pesa husaidia.
Pia maji yaliyochanganywa na chumvi ya mawe kisha kuyamwagia kwenye mzunguko wa fremu ya biashara
 
...naomba uniajiri nikufanyie biashara kwa siku 2 tuuh....afu nitakwambia mchawi nani apo (Kati ya mtoa huduma au mteja)..

Hakuna ndumba apo.....ni uzoefu tu wa kucheza na miamala ya pesa.

The law of life is law of beliefs.
 
Malakyishu ofisi yako ipo maeneo gani hapa dar nikutembelee tuonebmpangikio wako wa kazi, lazima Kuna loophole mahala haswa kwenye record keeping e - money transactions93335"]
Kwa miamala ya kibank wateja huwa nawajazia fomu za bank husika nabaki na copy na miamala ya simu huwa siandikishi ....nakua makini kwa kila hatua ya kufanya muamala napesa cash mtu anapotoa lakini nikipiga hesabu jioni hasara inakuwa ipo
[/QUOTE]
 
Hapo kwenye fremu ya biashara una fanya wewe mwenyewe au Kuna watu wankudaidia umewaajiri?
Kwa jicho la kiuhasibu apo linaonekana tatizo lipo upande wake...anaonyesha anatabia za kuchanganya pesa au kujijengea mahusiano ya moja kwa moja na pesa za biashara yake...hii ni tatizo la wafanya biashara wengi na hupelekea fikra mbovu na kuua biashara..

Mfanyabiashara unatakiwa husijenge mazoea ya mojakwamoja na biashara yako,biashara yako ichukulie kama artificial person ambapo damu yake ndo hizo miamala...so unapochukua pesa au kitu ktk biashara huo ni mkopo jirikodi,na unatakiwa lazima ulipe...na vilevile unaweza ukaikopesha biashara yako pesa na ukaidai...

Unapoitumikia biashara yako jiwekee kiwango cha mshahara ambacho biashara yako itakuwa inakulipa...sio unajichukulia pesa kama upo bank....apo utakuwa unafanya drawing mwsho wa siku account haitabalance na cash yako itaisha kabsa.
 
Kwa miamala ya kibank wateja huwa nawajazia fomu za bank husika nabaki na copy na miamala ya simu huwa siandikishi ....nakua makini kwa kila hatua ya kufanya muamala napesa cash mtu anapotoa lakini nikipiga hesabu jioni hasara inakuwa ipo
Yale makato ya kodi/charges ya huduma unaziconsider?
 
Back
Top Bottom