hivi mama hawadonoi vifaranga ambavyo si wake kweli!!

Swali lako lilishaulizwa na mdau huko nyuma, ni kwamba kuna baadhi ya kuku ni wakali sana na huwa hawakubali kabisa kupokea kuku wa wengine, huwadonoa vifaranga wasiokuwa wakwake na kuwaua kabisa, lakini si kwamba anawatambua kuku wake bali ukichelewa kuweka vifaranga vya nyongeza tena ukiweka anashuhudia huwashitukia pengine kwa harufu yao na hapo hufanya maangamizi. Unapomuongezea kuku vifaranga vya ziada unashauriwa umwekee usiku.

Kwa hiyo ni wajibu wako kuwatambua kuku wakali usiwape kamwe jukumu la kulea vifaranga. Kuna kuku ambao ni wapole sana, inabidi uwatambue na uwatumie kwa kazi hiyo ya kulea vifaranga bila kubagua. Kwa hiyo kuku wakali hao ni budi wabakie kutaga tu wala wasipewe fursa ya kuatamia.
 
Ndugu zangu nina tafuta kuku wafupi sana.naomba kama kuna anayeweza nipatia au kuwa na taarifa wapi pa kuwapata anijulishe.eneo nililopo hawapatikani kabisa

Ndugu yangu itabidi usafiri tu uwafuate mkoani Morogoro ndiyo ikulu ya hao kuku. Labda hata pwani maeneo ya
Mlandizi kuelekea Chalinze sina uhakika.
 
mkuu Kubota ahsante sana, nitafanya kwa awamu ijayo nione matokeo yake nitajiandaa kuyapima. kuna kuku ambaye sikutoa mayai yake , nitaangalia imekuaje atakapofikia kutotoa, ila wasi wasi wangu kwa kuku huyu jana ameshinda nje kwa muda mrefu sana sijui ni kwa nini wakati chakula na kila kitu kiko karibu, ametoka saa mbili asubuhi amerudi ndani saa nane! sijui kama atatotoa vizuri. thanks.
Hiyo huwa inatokea hata mimi niliwahi kumshitukia kuku mmoja akifanya hivyo, niachokuomba weka kumbukumbu sawa juu ya huyo kuku tuone matokeo yake kuhusu utotoaji wake utakavyokuwa. Kama mayai yanamda mrefu toka aanze kuatamia yanaweza yasiathirike kwa kuku anaejisahau kurudi kiotani. Lakini ili kujiridhisha itabidi tuone matokeo yake yatakavyokuwa.
 
Kubota asante nimeiona na nimeielewa vizuri sana. Nitazidi kuifanyia kazi kwa kutafuta kwenye mitandao wauzaji wa used or refurbished green houses hasa kutoka China au India. Balton ni aghari sana. Tutazidi kupeana feedback Kubota.By the way thread yako ya kuku wa kienyeji ni chemsha bongo sana. Sijui hiyo elimu na hayo maujuzi kama inafaa kwa ufugaji wa kuku chotara? Hebu tujuze kama inawezekana.

Hizi mbinu za ufugaji wa kuku wa kienyeji zinaweza kutoa matokeo mazuri sana kwa kuku Chotara. Mbinu hizi hutumika hata kwa kufuga kuku wa mayai pia. Kwenye ufugaji wa kuku wa kienyeji tunajiepusha kuwekeza nguvu kubwa sana kama ilivyo kwa kuku wa kisasa kwa sababu kuku wakienyeji wanakua taratibu sana na hawatagi mayai mengi kama kuku wa kisasa. Vinginevyo kinachoamua yote haya ni soko na kutaka kupata faida kubwa, jiulize bei ya sokoni kwa kuku chotara ikoje, anachukua muda gani hadi kufikia kuuzwa.

Je, akifugwa kama Broiler gharama ya chakula italipa? Je akifugwa kama layer ule utagaji wa chotara kuna faida? Ufugaji huu huria tunaofuga kuku wa kienyeji ni wenye gharama nafuu kwa vile kiasi kikubwa cha lishe kuku hujitafutia wenyewe au hulishwa kwa vyakula visivyokuwa vya kwango kikubwa kama kile cha kuku wa kisasa na bado faida inakuwepo kubwa kwa vile gharama ya chakula huwa ndogo. Kwa hiyo unaweza kupata faida zaidi ukifuga kuku chotara kwa mazingira ya kuku wa kienyeji, bado pia unaweza kufuga hata kuku wa mayai kwa mazingira hayahaya ikiwa utawapatia nyongeza ya chakula chao maalumu.
 
Mama timmy, pole na kupata tabu ya kutengeneza funza.mimi nilikuwa natumia mbolea ile ile ya kuku na pumba za mahindi.kuna dumu la lita 20 nimelikata juu kote uwa naanza kuweka bolea kama nusu na juu na weka pumba nusu ya kiwango cha mbolea nilichoweka.Baada ya hapo namwangia maji hadi kunalowana kabisa, nafanya zoezi la kumwagia maji kwa siku 2 halafu siku ya 3 simwagii then siku ya 4 unakuta funza wameshapatikana wa kutosha naewapa kuku.Njia nyingine ambayo ina gharama kidogo ni ya kutumia pumba na utumbo au nyama zile ambazo hazifai kuliwa.unachanganya hizo nyama au utumbo na pumba halafu unamwagia maji kiasi hadi vilowane kwa siku 3 hadi 5.Karibu.


Mkuu Dafo kesho nataka nijaribu hili zoezi la kutengeneza funza, ntaleta majibu.
Ama kweli "JF NI KISIMA CHA KUONGEZA UFAHAMU"
 
Kwi kwi kwiiii kama ungeniona ungenionea huruma. Mkuu nilianzisha ka hobby kengine huko msituni kwenye mikaa yetu nikajikuta nimekuwa mteja wa Bwana Nyama, mkuu hawa jamaa wanachojua wao ni kupigisha kwata tu! Lakini nashangaa mbona tembo wanaisha tu. Hapa bado nakandwa maji hali mbaya!

Ha ha ha Mkuu umeniacha hoi na hiyo TEMBO WANAISHA TU!!!!
Pole mkuu
 
Mchungaji Masanilo Nashukuru kwa ushauri kuepuka jangwa nitajidhatiti kupanda miti na hata ikibidi naanzisha msitu wangu. Kuhusu kufuga vyote nguruwe na kuku hawa wa kienyeji inabidi uwe mwangalifu sana jinsi ya kutengeneza banda la nguruwe maana kuku huingia kwenye mabanda ya nguruwe kuokoteza mabaki ya pumba sasa nguruwe ni fundi sana wa kuwadaka kuku! Hadi nilipokuja kukuta manyoya bandani ndiyo niligundua kuwa nguruwe ni balaa!

Hapo sasa! hata mie nilikuwa nataka kuuliza mixing ya kuku na wanyama wengine nadhani mbuzi ni bora zaidi na ninampango huo kwa baadae, tutajuzana tu wadau.
 
Mkuu Kubota asante kwa uzi mzuri sana nimejifunza memngi sana hapa...
Nina kaswali kidogo naomba kuuliza.

Ukifuga kuku wa kienyeji kwa mtindo wa nusu huria na ukawa na kuku say 800 kwa heka kama mbili hivi na ukajitahidi kuzingatia lishe kwa vifaranga vidogo na VINYOYA, faida kwa kila kuku baada ya kuuza inaweza kufika shilling 4000 kwa kuku baada ya kutoa gharama zote za uendeshaji?

Cha pili ni kuhusu chakula cha CHICK MARSH, mfuko mmoja unaweza kuwalisha vifaranga wangapi mpaka uishe? Na kwa muda gani?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kubota asante kwa uzi mzuri sana nimejifunza memngi sana hapa...
Nina kaswali kidogo naomba kuuliza...

Ukifuga kuku wa kienyeji kwa mtindo wa nusu huria na ukawa na kuku say 800 kwa heka kama mbili hivi na ukajitahidi kuzingatia lishe kwa vifaranga vidogo na VINYOYA, faida kwa kila kuku baada ya kuuza inaweza kufika shilling 4000 kwa kuku baada ya kutoa gharama zote za uendeshaji???

Cha pili ni kuhusu chakula cha CHICK MARSH, mfuko mmoja unaweza kuwalisha vifaranga wangapi mpaka uishe??? na kwa muda gani???

Wadau nawarushia mpira huo! Anzeni kumjuza Asigwa mimi bado nakatakata magogo leo hadi niliwashe tanulu, easter inakuja hiyo.
 
LiverpoolFC umepotelea wapi? Ukimaliza kuwanywesha dawa vinyoya wako njoo umwage update mkuu! Ha ha haaa
 
Kubota na wengine nawashukuruni kwa kutoa habari nzuri juu ya ufugaji wa kuku wa kienyeji. mimi pia nafuga, wapo kama hamsini tu. Nina maswali yafuatayo, kuku wangu wakifika umri wa kama wiki3 baadhi yao huanza kunyonyoka manyoya na kuwa watupu kabisa, ingawa baadae huota, hii inasababishwa na nini? ni upungufu wa madini au ni ugonjwa? kama ni madini ni ya aina gani niweze kuwapa mapema.

Pia ninaweza chukua mayai kutoka katika kuku wa kizungu layers aliyepandwa na jogoo chotara alafu nikampa kuku pure wa kienyeji alalie, je yatatotolewa? Na pia ni wakati gani mzuri wa kuwaachia vifaranga wa kienyeji kurandaranda wenyewe bila ya mama yao baada ya kuwakuzia ndani, je wiki 3 mpaka nne zinatosha au zaidi? Asante
 
Kubota na wengine nawashukuruni kwa kutoa habari nzuri juu ya ufugaji wa kuku wa kienyeji. mimi pia nafuga, wapo kama hamsini tu. Nina maswali yafuatayo, kuku wangu wakifika umri wa kama wiki3 baadhi yao huanza kunyonyoka manyoya na kuwa watupu kabisa, ingawa baadae huota, hii inasababishwa na nini? ni upungufu wa madini au ni ugonjwa? kama ni madini ni ya aina gani niweze kuwapa mapema. Pia ninaweza chukua mayai kutoka katika kuku wa kizungu layers aliyepandwa na jogoo chotara alafu nikampa kuku pure wa kienyeji alalie, je yatatotolewa? Na pia ni wakati gani mzuri wa kuwaachia vifaranga wa kienyeji kurandaranda wenyewe bila ya mama yao baada ya kuwakuzia ndani, je wiki 3 mpaka nne zinatosha au zaidi? Asante

Ahsante kwa uzi huu Mkuu Kubota na wadau wengine wanaochangia kuelimisha, Hapo penye RED namimi napenda kujuzwa tafadhali.
 
Kubota na wengine nawashukuruni kwa kutoa habari nzuri juu ya ufugaji wa kuku wa kienyeji. mimi pia nafuga, wapo kama hamsini tu. Nina maswali yafuatayo, kuku wangu wakifika umri wa kama wiki3 baadhi yao huanza kunyonyoka manyoya na kuwa watupu kabisa, ingawa baadae huota, hii inasababishwa na nini? ni upungufu wa madini au ni ugonjwa? kama ni madini ni ya aina gani niweze kuwapa mapema. Pia ninaweza chukua mayai kutoka katika kuku wa kizungu layers aliyepandwa na jogoo chotara alafu nikampa kuku pure wa kienyeji alalie, je yatatotolewa? Na pia ni wakati gani mzuri wa kuwaachia vifaranga wa kienyeji kurandaranda wenyewe bila ya mama yao baada ya kuwakuzia ndani, je wiki 3 mpaka nne zinatosha au zaidi? Asante

Mkuu Kuku wa Kizungu labda Parent, lakini haa wa Mayai hawafai na hata kiutalaamu haishauriwiingawa yanaweza totolewa lakini hivyo vifaranga watakua dhaifi na wanaweza kufa.

Kwa kuku wa kizungu ni lazima ununue Parents, Vifaranga au Kuku wazima na Vifaranga parents wanaagizwa kutoka South Africa, Uholanzi na Ugeruman, Ila kwa Africa mashariki Kenya ndo pekee kwenye kampuni inayo zalisha Vifaranga Parents wa kuku nyama na kuk mayai.
 
Ahsante kwa uzi huu Mkuu Kubota na wadau wengine wanaochangia kuelimisha, Hapo penye RED namimi napenda kujuzwa tafadhali.

Vifaranga hata wa siku moja unaweza kuwaachisha mama yao kama utakua unawapa chakula kizuri(hasa chick marsh) na kuwafunika na matenga(kama ni wachache) na kuwa na uhakika wa joto.

Ila kama ufugaji wako bado ni wa kuku wachache unaweza kuwaacha na mama yao mpaka wakafikia wiki mbili au tatu hivi halafu unawaachisha.
 
Mkuu Kubota asante kwa uzi mzuri sana nimejifunza memngi sana hapa...
Nina kaswali kidogo naomba kuuliza.

Ukifuga kuku wa kienyeji kwa mtindo wa nusu huria na ukawa na kuku say 800 kwa heka kama mbili hivi na ukajitahidi kuzingatia lishe kwa vifaranga vidogo na VINYOYA, faida kwa kila kuku baada ya kuuza inaweza kufika shilling 4000 kwa kuku baada ya kutoa gharama zote za uendeshaji?

Cha pili ni kuhusu chakula cha CHICK MARSH, mfuko mmoja unaweza kuwalisha vifaranga wangapi mpaka uishe??? na kwa muda gani???

Mkubwa asigwa maswali yako yako deep sana na ni ya msingi sana. Kusema kweli faida inategemea bei uliouzia na gharama ulizoingia. Kwa kweli kwa ufugaji huria sina uhakika na figure halisi ya gharama za ufugaji maana kila mtu anatunza kuku kivyake. Kwa wale ambao gharama yao ni zero, yaani ni kufungulia asubuhi na kufungia usiku faida yao ni kubwa sana kupita 4000/=.

Lakini kadri kundi linavyokuwa kubwa faida kwa kuku mmoja mmoja inapungua kutegemea na ulishaji, ukuaji na udhibiti wa vifo. Swali lako hili linahitaji utafiti mkubwa sana kuweza kupata jibu la uhakika kuona faida ya kuku afugwae huria imekaaje, ila ninaimani JF imesheeni wataalamu watatusaidia kwa hili.

Kuhusu sehemu ya pili nadhani cha msingi kujua ni mfuko wa chick marsh mmoja unatosha kulisha vifaranga wangapi hadi wanapofikia kuachishwa chick marsh. Saidieni hapa wadau.
 
Kubota na wengine nawashukuruni kwa kutoa habari nzuri juu ya ufugaji wa kuku wa kienyeji. mimi pia nafuga, wapo kama hamsini tu. Nina maswali yafuatayo, kuku wangu wakifika umri wa kama wiki3 baadhi yao huanza kunyonyoka manyoya na kuwa watupu kabisa, ingawa baadae huota, hii inasababishwa na nini? ni upungufu wa madini au ni ugonjwa? kama ni madini ni ya aina gani niweze kuwapa mapema. Pia ninaweza chukua mayai kutoka katika kuku wa kizungu layers aliyepandwa na jogoo chotara alafu nikampa kuku pure wa kienyeji alalie, je yatatotolewa? Na pia ni wakati gani mzuri wa kuwaachia vifaranga wa kienyeji kurandaranda wenyewe bila ya mama yao baada ya kuwakuzia ndani, je wiki 3 mpaka nne zinatosha au zaidi? Asante

Kuhusu kumwekea kuku wa kienyeji mayai ya kuku chotara ni kwamba sina uhakika kama kuna matokeo ya utafiti yaliyoonyesha kinyume na ninavyofahamu. Ni kwamba kuku wamewahi kuwekewa mayai ya kanga yakatotolewa, na historia inasema kuwa huko nyuma watumwa Afrika kusini walikuwa wakilazwa juu ya mayai ya mbuni yaliyofunikwa kwa blanketi na kuzuiliwa kinamna yasivunjike na mayai ya mbuni yalitotolewa.

Kuna nchi iitwayo Bali huko kuna utaalamu watu hutotolesha mayai kwa kuyaanika juani kwa masaa kadhaa yapate joto, kisha na huyafunika kwa kitu kama blanketi kuhifadhi joto na huyaweka ndani ya tenga, kitaalamu inajulikana baada ya siku 2 au 3 mayai huanza kutoa joto lake ambalo kama mayai ni mengi hilo joto hutosha kuyafanya yajipashe joto yenyewe. Hiyo ndiyo historia ya utotoleshaji ilikotokea kabla hazijaanza kutengenezwa mashine za kutotolesha.

Kutotoa yai hutokea wakati yai likipatiwa mazingira fulani ikiwamo joto, hewa, kuyageuza geuza na vitu vingine, ndiyo maana hata mashine zinatotoa sembuse kuku wa kienyeji? Nakubaliana inawezekana njia nyingine za kutotolesha si zenye ufanisi mzuri wa kutotolesha vifaranga.

Kwa hiyo kukujibu swali lako ni kwamba Kuku wa kienyeji anaweza kutotolesha mayai ya kuku mwingine. Kitu kama hiki ni rahisi tu kujaribu wakuu si unatupia mayai kwenye kiota uone kama hayatotolewi!

Kuhusu muda wa kuwatenganisha vifaranga kwa jinsi ulivyouliza mimi husubiri hadi kifaranga amefikia kumea manyoya ya kikubwa mwili mzima. Ni baada ya kuku kuwa na muonekano wa kuku halisi na si kama kifaranga tena. Kufikia kipindi hiki kinyoya huwa mwepesi sana kukimbia na kujificha dhidi ya maadui.

Hao kuku wanaonyonyoka manyoya kabisa inawezekana ni aina yao nadhani tutajulishwa hapa iwapo ni ugonjwa.
 
Habari zenu wana JF,
Hongera sana Kubota kwa kuanzisha huu uzi pia na wachangiaji wote.

Umegusia Kuwa unafikiria kuanza ufugaji kwa kuanza na kuku 250 Ndan ya ekari moja na baadaye ekari nne. Swali langu ni namna gani utapambana na maadui mf: paka, panya, Mbwa, n.k yaan Wale wote wanaoweza kuwadhuru kuku.

Asante!

Wadau JF nawashukuru sana kwa michango yenu na likes mnazonyunyizia hapa tangu nianze kusimulia hii kitu, nawashukuru sana na viewers wote mnaofungua uzi huu maana mmenipa courage niendelee kusimulia haya niliyoshuhudia. Nyie wote mmenipa moyo sana nimeona kwamba sipotezi muda bure, labda story hii inaweza kumsaidia yeyote ambaye alishakata tamaa au yule aliyekosa pa kuanzia.

Mojawapo ya siri kubwa kufanikiwa kwenye ujasiria mali, enyi wakuu, ni kung'ang'ania kile roho yako imependa kukifanya, wewe ng'ang'ania tu huku ukiendelea kujifunza kwa kila mweleka utakaopiga. Huo mweleka uliopiga leo ukijisahihisha inaweza ikawa ndiyo mweleka wa mwisho kuelekea kufaulu! Kunga'ngania kwangu na kujiuliza kila ninapopiga mweleka ndiyo kulinisaidia kujifunza zaidi baada ya kubaini ninapokosea! Ukiingia kwenye uwekezaji wowote kwa mara ya kwanza elewa hapo ni kipindi cha kujifunza tu na siyo vema kukata tamaa na kujitoa pindi mieleka ikianza!

Huwa kila nikikumbuka jinsi nilivyowahi kutupa vifaranga kwa wingi kipindi fulani wakati nikipitia kile kipindi cha kujifunza hadi leo nasikia uchungu. Lakini leo hii ninajiamini kuwa ninaweza kufuga kuku wa kienyeji bila shaka na sasa ninampango wa kufungua shamba na safari itakapo anza nitashusha updates hapa JF na wenye nauli mtakuja kushuhudia maana ni Morogoro kijiji fulani hivi kando kando ya kimsitu fulani ambako pia ninavitanuru vyangu nafyatua mkaa. Bwana miti akizidisha fujo zake nitahamia kwenye matofali ya kuchoma kwa pumba za mpunga hahahaaa.

Niliahidi kuendelea kusimulia jinsi ambavyo nilimudu kupambana na maadui wala kuku! Unapoanza kufuga kuku unakuwa kivutio kikubwa kwa kila aina ya midomo, kuna nyoka, vicheche, paka pori, tai, kenge, mbwa koko, nyani, nguruwe wakiwemo na watu pia.

Nyoka na kenge walikuwa wakija kwa vipindi fulani fulani hilo halikuwa tatizo la kila mara. Kenge walivizia zaidi mayai, nyoka walikuwa wanaua sana kuku. Nyoka anapokuja bandani ambapo mara nyingi ni usiku huwa ni rahisi kujua maana ..... INAENDELEA
 
Habari zenu wana JF,
Hongera sana Kubota kwa kuanzisha huu uzi pia na wachangiaji wote.

Umegusia Kuwa unafikiria kuanza ufugaji kwa kuanza na kuku 250 Ndan ya ekari moja na baadaye ekari nne. Swali langu ni namna gani utapambana na maadui mf: paka, panya, Mbwa, n.k yaan Wale wote wanaoweza kuwadhuru kuku.

Asante!


Niliahidi kuendelea kusimulia jinsi ambavyo nilimudu kupambana na maadui wala kuku!
Unapoanza kufuga kuku unakuwa kivutio kikubwa kwa kila aina ya midomo, kuna nyoka, vicheche, paka
pori, tai, kenge, mbwa koko, nyani, nguruwe wakiwemo na watu pia.

Nyoka na kenge walikuwa wakija kwa vipindi fulani fulani halikuwa tatizo la kila mara. Kenge walivizia zaidi mayai, nyoka walikuwa wanaua sana kuku. Nyoka anapokuja bandani ambapo mara nyingi ni usiku huwa ni rahisi kujua maana kuku hupiga kelele sana. Kudhibiti nyoka inawezekana kwa kupambana na kuwauwa kila wanapokuja, na hii inahitaji ujasiri maana usipokuwa makini unaweza kuua sana kuku badala ya nyoka mwenyewe. Njia ya kujihami ni kuhakikisha mabanda hayatoi mianya ya nyoka kupenya na kuingia bandani mara baada ya banda kufungwa. Nimewahi kusikia na nitakuja kutoa taarifa hapa bado ninafuatilia, kwamba kuna aina ya mti fulani ambao ukitumika kwa namna fulani huzuia nyoka wasifike kwenye eneo!

Ndege wa angani kama tai na kunguru wanatamba sana kama kuna uwazi hakuna vichaka vya kujifichia. Kuku ambao hushambuliwa zaidi ni vifaranga na vinyoya. Lakini hawa wote ni hodari sana kujificha iwapo kuna kitu cha kujifichia.
Kadharika ndege mara nyingi hutua kwanza kwenye mti kabla hawajachukua kasi ya kwenda kufanya mashambulizi. Uwepo wa miti mirefu kwenye eneo la ufugaji hukaribisha balaa. Unaweza kujenga kama mfano wa chanja fupifupi kama futi moja toka chini sehemu tofauti tofauti za eneo lako wanakochungia kuku. Hii itawazaidia kukimbilia chini yake pale mwewe au kunguru akianza kuleta shida.

Kuku wanaishara ambazo hutoa mara mwewe akiwasili na vinyoya hukimbia mara moja chini ya chanja hizi. Chini ya chanja hizi ni sehemu nzuri pia kuweka chakula cha nyongeza na maji. Zinaweza kuwa nyingi kadri wingi wa kuku ulivyo na kwa kutumia common sense.

Funga kazi ya yote, katika kudhibiti viumbe wengine waliosalia nilioorodhesha hapo juu nilikuwa ninatumia mbwa. Ufugani wa kuku ndiyo uliofanya kubaini kuwa mbwa ni kifaa kikubwa cha ulinzi ambacho kinaufanisi mkubwa sana kikihudumiwa vizuri na kutumika vizuri. Ujuzi huu wa kutumia mbwa niliupata kwa mfugaji kuku mwanamama ambaye ndiye aliyeniuzia kuku wa mbegu.

Mazingira yake ya kufugia yalifanana na mazingira yangu, alikuwa amepakana na eneo lenye uwazi kubwa sana amabako kuku walikuwa wakisambaa na kwenda mbali sana. Kulikuwa na points mbili ambako ndiko huko maadui wengi walikuwa wakiingilia kuleta midomo yao kuvizia kuku. Huyu mfugaji alinisimulia mbinu yake akijiamini bila mashaka ambapo nami niliichukua na kuitumia na kuleta mafanikio makubwa.

Kwa hiyo mfugaji huyo mwanamama shupavu alikuwa amefuga mbwa watatu tu wenye maumbile ya kawaida ya mbwa wetu wa kiswahili. Mbwa wawili kila mmoja alimfunga aliwafunga kwenye kivuli kwenye zile points ambako ndiyo huijia maadui! Kama nilivyosema yeye kwa jiographia ya eneo lake alikuwa ametambua sehemu mbili kuu ambako ndiko huko vicheche, mbwa koko, paka n.k walikuwa wakiingilia eneo wanakochungia kuku.

Mbwa mwingine wa tatu yeye alikuwa anamwacha free kuzunguka huku na kule. Kwa hiyo alikuwa amewafundisha kwamba inapotokea................. INAENDELEA
 
Habari zenu wana JF,
Hongera sana Kubota kwa kuanzisha huu uzi pia na wachangiaji wote.

Umegusia Kuwa unafikiria kuanza ufugaji kwa kuanza na kuku 250 Ndan ya ekari moja na baadaye ekari nne. Swali langu ni namna gani utapambana na maadui mf: paka, panya, Mbwa, n.k yaan Wale wote wanaoweza kuwadhuru kuku.

Asante!

Kwa hiyo mfugaji huyo mwanamama shupavu alikuwa amefuga mbwa watatu tu wenye maumbile ya kawaida ya mbwa wetu wa kiswahili. Mbwa wawili kila mmoja alimfunga peke yake kwenye kivuli kwenye moja ya zile points ambako ndiyo huijia maadui! Kama nilivyosema yeye kwa jiographia ya eneo lake alikuwa ametambua sehemu mbili kuu ambako ndiko huko vicheche, mbwa koko, paka n.k walikuwa wakiingilia eneo wanakochungia kuku. Mbwa mwingine wa tatu yeye alikuwa anamwacha free akizunguka huku na kule. Kwa hiyo alikuwa amewafundisha kwamba inapotokea kwenye point moja kuna adui anaanza kujivuta kuingia kwenye eneo huyu mbwa aliye karibu anabweka sana na kuruka ruka kama mjuavyo, kwa kufanya hivyo kokote kule alikokuwepo yule mbwa ambaye hajafungwa alikuja mkuku kama faru kuja kufukuzana na huyo adui ambaye alikuwa anaanza kuingia. Na wakati wa pilika zote hizi tayari kuku walikuwa wameshajua kuwa kuna adui na hivyo mesheni ya adui kuvizia inakuwa imeshatibuka.

Kwa vile makazi yangu nimepakana na pori kwa upande mmoja na makazi kwa upande mwingine mimi nilikuwa na point moja tu ambako hao mapaka walikuwa wakiingilia. Nilifuga mbwa wawili tu. Mmoja nilikuwa nikimfunga mbali huko kwenye hiyo sehemu ambayo hao vicheche walikuwa wakiingilia.

Mwingine nilimwacha free kupiga doria huku na kule. Utaratibu huu ulifanikiwa sana. Adui hawakuweza kupenya ngome hii. Sikuwa na haja kufikilia kuwa na fensi. Nilijikuta ninawapenda sana mbwa wangu kwa huduma kubwa waliyokuwa wananipatia. Usiku kama ilivyo kwa hali ya kawaida mbwa ndiyo walinzi wa makazi ikiwa pamoja na kudhibiti zaidi wanyama maadui wa kuku. Kutokana na hilo niliona ilikuwa ni lazima kutenga fungu la bajeti kwa ajili ya kuhudumia mbwa kwa ajili ya chakula na matibabu.

Ufugaji wa mbwa una changamoto zake na unahitaji nidhamu kubwa kuwadhibiti hasa wanapokuwa wakali! Nyumbani kwangu kulikuwa kunatisha kiasi kwamba wezi wadogo wadogo ambao wana allergy ya mbwa walikuwa wala hawafikirii kufika kwangu.

Mbwa kwenye nchi zetu wanatazamwa kwa kupuuzwa sana, lakini huduma anazoweza kuzifanya mbwa endapo ingekuwa ni mtambo wa kutengenezwa na binadamu huo mtambo ungeuzwa kwa bei kubwa sana. Mbwa kama rafiki wa binadamu ni mlinzi mwema ambaye binadamu amepewa na muumba wetu. Fikiria mtambo ambao unaweza kunusa na kufahamu iwapo adui anavizia au ameingia kwenye mazingira yako ungeuzwa shilingi ngapi!

Nchi zilizoendelea wanatengeneza sensors ambazo zinatambua uwepo wa mtu na huwasha taa au kupiga kelele, bei ya mitambo hiyo ni kubwa na bahati mbaya mitambo mingi ni fixed. Mitambo hiyo haiwezi kutembea na haiwezi kupambana kama mbwa. Mbwa ni alarm na pia hupambana kwa nguvu zote. Vinginevyo ukiamua kuajili mlinzi ni gharama kubwa sana kama kitu chenyewe anacholinda ni kuku tu halipi kwa ufugaji mdogo. Na huyo mtu anaweza kukugeuka akakuhujumu ingawa mara nyingine mbwa hula mayai pia anyway.

Kwa kutazama kinamna hii na hasa kwenye ulinzi wa kuku, binafsi nimekuwa nikiheshimu sana matumizi ya mbwa kama mlinzi mbadala wa kuku katika ufugaji huria. Na watumikapo hawa walinzi mbadala wanastahili kutengewa bajeti ili wapate chakula na huduma ya afya vizuri. Kwa hiyo ninaimani kwa kuwa vile sina uwezo kifendha za kuweza kulizungushia fensi shamba langu tarajiwa, nitaweza kulinda shamba hilo la kuku huria bila mashaka kwa kutumia mbwa kwa idadi yao itakayoendana na mazingira yatakavyokuwa. Ninajua maadui-watu ni kazi sana kuwadhibiti hao nitapambana nao mbele kwa mbele kadri hali itakavyojitokeza.
 
Back
Top Bottom